Unajua kinachowapa jeuri jamaa ni the fact kwamba Arsenal ni timu inayopendwa na neutrals wengi, kuna watu wengi ambao sio mashabiki wa Arsenal lakini wanapenda kuwaangalia wakicheza, pia location yao ya london inawasaidia sana coz watalii wengi wanapenda kwenda kuwaona so hawa jamaa hawategemei sana mashabiki damu kama sisi. One of the most expensive club (kama sio the most expensive) to watch. Kinachoudhi ni kuwa uongozi unajali zaidi balance sheet na kusahau kuwa hiyo kitu haina maana yoyote kwa mashabiki, wao wakimaliza kwenye top 4 tu, hilo ni bonge la achievement coz wanajua mamilioni ya champions league yataingia, mimi nasali sana tumalize nje ya hiyo top 4 ili wakose hela na wao wapate uchungu, na hiyo hasara itawalazimisha wanunue wachezaji wa maana.
Strategy ya AW ya kununua watoto ingefanya kazi kama tungekua hatuuzi, watoto wanakuja wakikaa few seasons na kuwa finished articles wanapigwa bei! Ni kama vile unajenga nyumba halafu ukifika juu badala ya kupaua unapiga kozi kadhaa chini halafu unaanza tena kujenga, huo ujenzi hauishi! Naamini kama tungekua hatuuzi wachezaji wetu, hakuna timu ingekua inatia mguu kabisa! Achilia waliouzwa zamani, rudisha tu Clichy, Fabregas, Nasri, RVP na Song kichwani mwako uone hii timu ya sasa inavobadilika..And did I say Theo and Sagna wanaondoka next month??