Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Vermaleeeeeen!!
Naona Dk ya 88 kama kawaida yetu tumesawazisha!!
 
Kunaweza kukawa na extra time hapa wakati huo ARSENAL watakua wameshaizoea baridi ya YORKSHIRE coz iko mainazi 3
 
Dah kazi kweli kweli ..... Arsenal Out
Wenger aliambiwa awaandae vijana incase ikitokea wanafika kwenye penalty!! Babu kama kawaida akabisha, akidai mpira unaishia kwenye dk 90!

Bradford wameendeleza rekod yao ya unbeaten kwenye 11 consecutive penalty shoot out!!
 
Reading vs arsenal 22/12/2012

wigan vs arsenal 26/12/2012

arsenal vs newcastle 29/12/2012

southampton vs arsenal 01/01/2013

arsenal vs man city 13/01/2013

chelsea vs arsenal 20/01/2013

KAZI IPO HIZI NDO NEXT GAMES ZA WASHIKA BUNDUKI WA KASKAZINI MWA LONDON

Sijui fans wakoje huko 5hours safari ya kutoka BRADFORD kurudi makwao london
 
Kunaweza kukawa na extra time hapa wakati huo ARSENAL watakua wameshaizoea baridi ya YORKSHIRE coz iko mainazi 3

Baridi Mchezo? Haizoeleki mkuu leo ndugu zangu wa Kisiwani wanasema Asenaliii miguu imetetemeka kwa hizo Mainazi 3.
 
siku zote huwa nasema lakini leo nimeona kweli Babu keshazeeka hata kuona sijui kama anaona vizuri Ramsey hakuwa akifanya lolote kipindi kizima cha kwanza babu alikuwa akisubiri ushahidi,
Arsenal kama ikifika # 4 basi UK hakuna mpira tena lazima babu aondoke ndio timu inaeza badilika huezi cheza mpira hata kama una wachezaji wazuri vipi ikiwa formation yako ni ile ile
Mimi nimefurahi leo Arsenal kufungwa na bado tutafungwa na vibonde wengi mwisho wa wiki tutaona
 
Arsenal ya sasa imekua ni timu ya kawaida sana, zamani timu ndogo zilikua zikicheza na Arsenal zinacheza defensively, wanajaza defensive midfielder kibao katikati lakini sasa hivi kila mtu anajua akicheza na Arsenal kushinda ni rahisi, unawashambulia tu. I used to buy Arsenal tops, I used to go to the emirates lakini siku hizi nimegoma, nimesusa kabisa hadi waanze kutumia mamilioni wanayopata kununua wachezaji wa maana na kuacha kuendekeza child labour, and I agree its time for Wenger to go now, his best days are behind him. Hata Bradford jamani? A team that is 65 places below us? Tena wala hatuna excuse coz tulikua na kikosi kamili, shame, shame...
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Yaani Mkuu KKN we acha tu!!! Natamani kungekuwa na wapenzi wenye msimamo kama wako na kususia kwenda kuziona mechi za Arsenal au kununua bidhaa mbali za Arsenal ili kuwashinikiza owners na management kutoridhishwa na muelekeo wa timu.

Arsenal ya sasa imekua ni timu ya kawaida sana, zamani timu ndogo zilikua zikicheza na Arsenal zinacheza defensively, wanajaza defensive midfielder kibao katikati lakini sasa hivi kila mtu anajua akicheza na Arsenal kushinda ni rahisi, unawashambulia tu. I used to buy Arsenal tops, I used to go to the emirates lakini siku hizi nimegoma, nimesusa kabisa hadi waanze kutumia mamilioni wanayopata kununua wachezaji wa maana na kuacha kuendekeza child labour, and I agree its time for Wenger to go now, his best days are behind him. Hata Bradford jamani? A team that is 65 place below us? Tena wala hatuna excuse coz tulikua na kikosi kamili, shame, shame...
 
Yaani Mkuu KKN we acha tu!!! Natamani kungekuwa na wapenzi wenye msimamo kama wako na kususia kwenda kuziona mechi za Arsenal au kununua bidhaa mbali za Arsenal ili kuwashinikiza owners na management kutoridhishwa na muelekeo wa timu.

Unajua kinachowapa jeuri jamaa ni the fact kwamba Arsenal ni timu inayopendwa na neutrals wengi, kuna watu wengi ambao sio mashabiki wa Arsenal lakini wanapenda kuwaangalia wakicheza, pia location yao ya london inawasaidia sana coz watalii wengi wanapenda kwenda kuwaona so hawa jamaa hawategemei sana mashabiki damu kama sisi. One of the most expensive club (kama sio the most expensive) to watch. Kinachoudhi ni kuwa uongozi unajali zaidi balance sheet na kusahau kuwa hiyo kitu haina maana yoyote kwa mashabiki, wao wakimaliza kwenye top 4 tu, hilo ni bonge la achievement coz wanajua mamilioni ya champions league yataingia, mimi nasali sana tumalize nje ya hiyo top 4 ili wakose hela na wao wapate uchungu, na hiyo hasara itawalazimisha wanunue wachezaji wa maana.

Strategy ya AW ya kununua watoto ingefanya kazi kama tungekua hatuuzi, watoto wanakuja wakikaa few seasons na kuwa finished articles wanapigwa bei! Ni kama vile unajenga nyumba halafu ukifika juu badala ya kupaua unapiga kozi kadhaa chini halafu unaanza tena kujenga, huo ujenzi hauishi! Naamini kama tungekua hatuuzi wachezaji wetu, hakuna timu ingekua inatia mguu kabisa! Achilia waliouzwa zamani, rudisha tu Clichy, Fabregas, Nasri, RVP na Song kichwani mwako uone hii timu ya sasa inavobadilika..And did I say Theo and Sagna wanaondoka next month??
 
Mna shida na hako katim kenu, huyo wenger si mumfukuze? Timu haina hata mchezaji mmoja wa maana. Eti vermaleen ni captain wa timu, sijui aliwahi kucheza mpira lini na wapi.timu zote kubwa ili uwe captain lazima uwe umecheza premier league mechi si chini ya 300, sasa huyo vermaleen hata mechi 70 hajafikisha mnampa u-captain? Ataongoza vipi timu? Kaulizeni Kompany, Terry, Ferdinand, Evra, Gerald wamecheza mechi ngapi kwenye timu zao ndio wakapewa u-captain.
 
Mna shida na hako katim kenu, huyo wenger si mumfukuze? Timu haina hata mchezaji mmoja wa maana. Eti vermaleen ni captain wa timu, sijui aliwahi kucheza mpira lini na wapi.timu zote kubwa ili uwe captain lazima uwe umecheza premier league mechi si chini ya 300, sasa huyo vermaleen hata mechi 70 hajafikisha mnampa u-captain? Ataongoza vipi timu? Kaulizeni Kompany, Terry, Ferdinand, Evra, Gerald wamecheza mechi ngapi kwenye timu zao ndio wakapewa u-captain.

Najua unahitaji kuponda na wewe uonekane ila sidhani kama uko sawa unaposema kuwa captain uwe umecheza mechi 300. Na kumtaja kwako Kompany inaonesha we ni mshabiki maandazi tu. Hata hujui Kompany alikuja lini EPL.

Halafu ni hii Arsenal ambayo mnasema haina hata mchezaji mmoja wa maana ila wakihama mnaanza kuwasifia. Mf. RvP. Hebu jipange..
 
Back
Top Bottom