Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Jirani mambo vipi.
Najua kabisa Walcott kiwango chake kimedumaa, hata mimi ningemwambia aondoke....Tatizo langu ni huu utamaduni unaojitokeza kwa baadhi ya washabiki especially wa Arsenal, wanakuwa wakali kupita kiasi kwa wachezaji walioondoka Arsenal. Utakuta mtu anaongelea mapungufu tu bila kuonyesha kwamba yule mchezaji alitoa mchango wowote alipokuwa Arsenal. Mapungufu haya hayasemwi wakati mchezaji hajaamua kuondoka. Kwanini tusijifunze kusema "ahsante kwa mchango wako kwenye club na tunakutakia mema huko uendako"....huu ndio ustaarabu. Kumbuka mchezji ni binadamu kama walivyo wengine, anazo haki zote za msingi ikiwa ni pamoja na kufanya maamuzi kuhusu career yake.
Nadhani ni aina ya uondokaji wa wachezaji wenyewe ndo huwa inawaumiza wadau wenzangu wa Gunners,wengi huondoka kwa sababu ya maslahi duni ndani ya Arsenal(kitu ambacho kuna kipindi mimi huwa nawaunga mkono)...Hata ningekuwa mimi,najiona kabisa nina mchango kwa timu na ndiye injini ya timu(mfano Song) nalipwa Pauni elfu 50 wanakuja Barca na dau la elfu 80 kwa kweli siwezi kulaza damu.......Lazima nitaondoka maana mpira ndo kazi yangu nammfanyakazi yeyote yule huangalia wapi kuna maslahi mazuri....Tusiwaone wachezaji ni wasaliti kwa kukimbilia sehemu zenye maslahi mazuri na kuwaita majina ya ajabu ajabu.....Tukae chini na kuangalia tatizo liko wapi.....Tujiulize kwa nini kila siku/msimu ni Arsenal tu?, 'Why always Arsenal'?....

Kuna siku nilisema kwamba "Tatizo ni mfumo wa ulipaji mishahara uliopo Arsenal.....Wachezaji wengi wanaondoka Arsenal kwa sababu ya mishahara duni ukilinganisha na timu nyingine.......Bodi ya Arsenal inapaswa kubadilika na kubadili mfumo wa ulipaji mishahara,tofauti na hapo Arsenal itaendelea kuwa feeder club kila mwaka......Kazi yetu itakuwa ni kutengeneza wachezaji na kuwajengea umaarufu na kuwauza hivyo habari ya vikombe itabidi tusahau......

AW hapaswi kulalamikiwa katika hili la wachezaji kuondoka,anapaswa kuonewa tu huruma......Wa kulalamikiwa ni board wa Arsenal........

Najivunia kuwa Mshika Bunduki.........

Once a Gunner, always a Gunner......

Gunners for life...................No matter what....."
 
Binafsi kuna wachezaji ambao naomba kila siku waondoke Arsenal......

Hawa ni pamoja na Walcott, Diaby, Djourou, Fabianski, Arshavin, Squillaci na Chamakh......Hawana msaada wowote kwa timu......Ni bora wauzwe tu wote na kusajili hata wachezaji wawili ama watatu wa maana....
Na hakuna dalili za kuuzwa
 
Na hakuna dalili za kuuzwa

Tena hapo ni afadhali huyo Diaby na Arshavin wanaweza kutumika lakini hao wengine wameambiwa ni "surplus to requirement".

Du! mzee Wenger kiboko, amewaambia Bendtner na Chamakh watafute timu kabla ya Ijumaa na wao wamewaagiza mawakala wao watembeze CVs zao kutafuta timu.
 
Kesho ni Draw ya Chamapions League.

Kesho Arsenal pamoja na timu zingine 31 zitakuwa zikisubiri kufahamu matokeo ya "draw" itakayofanyika kisiwani Monaco kwenye kituo maarufu cha mikutano kiitwacho Grimaldi Forum.

Timu 27 ikiwemo Arsenal zilifuzu kucheza michuano hiyo pamoja ni timu zingine tano ambazo zitakuwa zimefaulu leo jioni katika miji mbalimbali barani Ulaya.

Arsenal ikiwa na rekodi nzuri kwenye mashindano hayo itapangwa kwenye fungu moja linaloitwa "pot one" pamoja na timu za Chelsea, Barcelona, Manchester United, Bayern Munich, Real Madrid, Porto na AC Milan.

Draw hiyo itaonyeshwa moja kwa moja na Sky Sports news na ESPN pamoja na vituo vingine barani Ulaya na itakuwa ni saa 12 jioni za Monaco au 11 jioni kwa wale wa UK.

In Arsene we trust.
 
Arsenal transfer news: Upadates

Nicklas Bendter anafanya mazungumzo na Juventus ya Italy na huenda akaondoka jioni hii kuelekea Italy kwa "medical".

Park-Chu Young anakwenda Celta Vigo ya Spain kwa mkopo kwa mwaka miezi 12 na ameishaondoa vifaa vyake kabatini kwake na kusema kwaheri.
 
Bado timu mbili na tunaomba zisiwe za mbali -yaani Ulaya mashariki.
 
Update:

Group B

Arsenal

Schalke (Germany)

Olympiakos (Greece)
 
Kundi la Arsenal kwa ujumla.

Kundi B

Arsenal

Schalke (Germany)

Olympiakos (Greece)

Montpellier (France)

Raha kwelikweli.
 
Bendtner anaenda Juventus. Park anaenda Celta Vigo. Wote kwa mkopo lakini kuna option ya kuwanunua mwisho wa msimu.
 
Pia jioni hii Arsenal walikuwa wakiangalia offers kutoka Besiktas na Malaga kwa ajiliya Chamakh, inawezekana akawa akienda kwenye moja ya timu hizo.
 
Pia jioni hii Arsenal walikuwa wakiangalia offers kutoka Besiktas na Malaga kwa ajiliya Chamakh, inawezekana akawa akienda kwenye moja ya timu hizo.

Chamakh to Malaga on loan has gone through. I think we need to bring in a striker now
 
Chamakh to Malaga on loan has gone through. I think we need to bring in a striker now

Itakuwa ni bora maana Chamakh analipwa 70000K kwa wiki na Malaga hawana uwezo huo kwahio watakuwa wamekubaliana na Arsenal kwamba wasaidiane kumlipa hicho kiasi.
 
Acha unafiki wewe. Wenger amesajili wachezaji watatu tayari mbona unasahau mapema?
Sasa povu la nini mkuu MwafrikaHalisi? Wala sikatai, ulisoma alivyoosema kuhusu usajili hata baada ya kuwasajili kina Podorsky? Kama tunakwenda kwa hoja wala hatupaswi kulumbana mkuu. In short tarehe 22/8/2012 alisema hivi "We are expecting to have two more players in the Squad before the deadline" Kwanini aseme hivyo wakati alishasajili hao "watatu"? Ukiona mtu anatumia nguvu kutetea hoja ujue uzito wa hoja yake ni mdogo!!!!!!
 
Last edited by a moderator:
schalke na olympiakos si mchezo hapo...Arsenal itabidi wajitahidi angalau washinde home games zao.. maana na hivi your experienced players wamewakimbia i fear for you guys in the champions league this season but good luck anyway
 
Back
Top Bottom