KERO Apps za mikopo mitandaoni, serikali ipo wapi?

KERO Apps za mikopo mitandaoni, serikali ipo wapi?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Zinachotwa wizarani zinazungushwa huku, na kuanzisha kampuni za betting. Ni zao hizo, wana riba kubwa sana,mi nilirudi kwenye mikopo ya kampuni za simu.
Sema wape pesa yao alafu temana nao
 
Kwa ulimwengu tuliopo sasa, ni vigumu kwa mtu/jamaa kukukopesha hela kirahisi, ndipo umuhimu wa hizi apps, microfinances, banks zinakuwa na umuhimu.
Kwa mazingira hayo, tatizo si wao, tatizo liko kwako; umechukua cha watu, warudishie ndani ya muda mlio kubaliana.
Vinginevyo, hao unao waomba wakusaidie kuwafungia hao, ndio ulitakiwa uwafuate mwanzoni ili wakukopeshe.​
Mkuu shida yao,siyo wa kweli,kwenye regulation zao wanasema mengine na kwenye utekelezaji wanafanya vingine,wanaweza kukuambia wanakupa 50 na riba wanakata mapema sana 10, na utarejesha baada ya siku 30,
-badala ya 40 wanakupa 30, IDADI unayodaiwa inabaki 50kamili,na muda wa kurejesha unakuwa siku SITA TU,badala ya siku 30.
HII NDIYO SHIDA YAOI KUBWA.-UTAPELI TU.
 
Mkuu shida yao,siyo wa kweli,kwenye regulation zao wanasema mengine na kwenye utekelezaji wanafanya vingine,wanaweza kukuambia wanakupa 50 na riba wanakata mapema sana 10, na utarejesha baada ya siku 30,
-badala ya 40 wanakupa 30, IDADI unayodaiwa inabaki 50kamili,na muda wa kurejesha unakuwa siku SITA TU,badala ya siku 30.
HII NDIYO SHIDA YAOI KUBWA.-UTAPELI TU.
Kweli kabisa, halafu ukiwaauliza kwanini ni kinyume na kilichoandikwa mwanzo wanatukana tu.
 
Majority ya Izo namba almost zote ni Airtel,

Hii kampuni ya simu ya Wahindi Kwa kweli ni shida sana hata wale wazee wa ile Hela tuma kwenye namba hii nao wengi Wana simcards za Airtel

Airtel unaweza kuwa una mazungumzo ya issue za Hela either Kwa call or text na mtu wako credible tu ila ukimaliza tu Kufanya ayo mazungumzo inakuja sms kutoka Kwa tapeli kuwa ile Hela tuma kwenye namba hii
 
Back
Top Bottom