Apple Iphone 12 is finally here

Apple Iphone 12 is finally here

kuna iship mmoja aliponda sana 5g sa samsung kwamba ni gimic.kwa vile 5g haijaenea sana apple hawawezi kuiweka.


apple wanajua soko kuliko wafuasi wake wanaowasemea.

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
Yaani isheep wao apple akisema hiki hakitaki au hakiweki basi na wao wanasema apple hajaweka sio cha muhimu.

Isheep apple akiwaambia this time mpigwe mashine watatugawia sana makalio bure kwa sababu apple kasema.

Chochote atakachokisema apple wao wanakipokea kama kilivyo. Apple akisema 5G sio ya muhimu isheep wote wanakubali, kesho akisema ni muhimu wote wanakubali.

Hivi hizi simu mbona hawaweki battery capacity? Sioni RAM, sioni 120hz display.

Mwakani Apple ataongeza tu 120 display na RAM kidogo tu halafu atawapiga bei kondoo wake na wao wanachekelea.

Leo anawaambia hatoi charger kwa sababu ya kimazingira lakini anasema ukiihitaji unaweza kununua. Kwamba ukinunua seperate huharibu mazingira ila ikija na simu inaharibu mazingira na makondoo yanachekelea tu. Halafu watu kama hao wanawacheka waumini wa mzee wa upako au wa Gwajima.
 
Mwenye pesa huwa anafanya kwa vitendo tu, zimetengenezwa ili ziuzwe, najua zitanunulika saana tena sana tuu.

Jengeni uchumi wa USA wengine wanajenga china na Moscow
 
Hawa jamaa bhana camera zao huwa wanafanyaje? utakuta 12mp camera kali kuliko 108mp za simu zingne naelewa somo la mega pixels...ila wao huwa wanafabyaje nauliza
Hata google pixel hua yuko hivo. Mp chache ila ubora uko juu
 
Leo anawaambia hatoi charger kwa sababu ya kimazingira lakini anasema ukiihitaji unaweza kununua. Kwamba ukinunua seperate huharibu mazingira ila ikija na simu inaharibu mazingira na makondoo yanachekelea tu. Halafu watu kama hao wanawacheka waumini wa mzee wa upako au wa Gwajima.
Kwamba simu inauzwa bila charger? Sasa utachajia nini?
 
Mkuu chief ndo nimemaliza kusoma reviews mbalimbali za wadau kuhusu hiyo brand mtandaoni.

Asilimia 95 wamelaumu sana kukosekana kwa 120hz display hii ni nini? Na ni upi ubora wa hyo 120hz maana hata sielewi japo kila mchangiaji kashangaa... kingine wamelaumu kuhusu battery na notch wewe wazungumziaje?
Mkuu suala la battery usiangalie namba subiri reviews maana linaangalia vitu vingi sana ikiwemo quality ya display na processor. Ni kawaida sana simu yenye 2700mah kuikimbiza yenye 4000mah.

Kwenye Notch mimi binafsi zisipendi, na sijawahi kumiliki simu ya Notch. Sema kama unamiliki iphone kila mwaka utakuwa umeshaizoea kuanzia iphone X mpaka leo ipo.

Kuhusu 120hz huo ni uwezo wa picha (frame) ambao simu inaweza kuonesha kwa sekunde. Kwa simu faida kubwa ni pale unapo scroll inakuwa smooth sana. Pia inasaidia kwenye games zinazosuport 120hz. Na pia simu za kisasa zina kitu kinaitwa variable refresh rate, kwa maana display inaji adjust kutokana na matumizi mfano unascroll inaenda hadi 120hz ila ukisimama kuangalia picha inashuka hadi 10 ama 20hz. Hapa watakuwa Apple wanasave cost kama kawaida yao.
 
Kwanza. Iphone za wadada vidume Ngoja tuendelee kutumia TECNO

ad65caf3-a163-42d1-899a-c302cdb80807.jpg
 
Back
Top Bottom