App ya kupokea Wageni toka Nje (Couchsurfing) : Hivi ndivyo ninavyopokea wageni na kutengeneza pesa

GLOBAL CITIZEN

JF-Expert Member
Jun 5, 2014
767
1,655
Greetings everybody?

I trust you are good.

Leo kama ilivyo kawaida yangu kutoa maarifa bila uchoyo kabisa nataka nikufundishe jinsi unavyoweza kutumia app ya CouchSurfing kupata wageni toka nchi nyingine (Europe, North America, Africa, Asia, Brazil etc)....lakini pia jinsi unavyoweza tumia opportunity hii kutengeneza pesa au hata kuwa mwanzo wakuunda kampuni yako ya utalii.

Kwa kuanza naomba niseme CouchSurfing ni nini?

CouchSurfing ni mtandao unaosaidia wageni wanaosafiri kwa budget ndogo kupata nafasi yakulala hapo nyumbani kwako iwapo wametembelea mji/kijiji unachoishi.

Kwa kawaida baada ya kujiunga katika site ya CouchSurfing utapokea request kila mara wasafiri toka nje watakapokuwa katika mji unaoishi na wanahitaji uwapokee hapo kwako kwa siku chache.

How amazing that is?

Angalia mfano wa baadhi ya wageni ambao nimewapokea kwangu.

IMG_6310.JPG



Huyo ni mgeni toka Croatia. Alikaa kwangu siku 2.

Mwingine ni dada wa Kichina toka Shandong, China.

IMG_6312.JPG


Hao ni baadhi tu.

I have so many references.

Nimetaka nikuonyeshe kwa mifano dhahiri na si blah blah.

Ok.

Sasa twende nikuonyeshe jinsi unavyoweza tumia opportunity hii kutengeneza pesa au hata kufungua kampuni.

Ready?

1 • Fahamu sehemu zote zinazofaa kupeleka wageni katika mji au kijiji unachokaa.

Hapo vipi?

Kama wewe unaishi let say Arusha au Dar es Salaam au Iringa hakikisha unafahamu sehemu chimbo zote za utalii.

Hapa simaanishi hotels au restaurants.

Namaanisha sehemu kama vile waterfalls, msitu mdogo wakufanya hiking, lake, sehemu ya makumbusho, sehemu wanazopika vyakula vya asili, sokoni na kadhalika.

Ukifahamu sehemu amazing zakumpeleka mgeni wako inamaana atakuona wewe ni mjuzi wa eneo lako la hii inaweza baadae kufungua njia ya kufanya business.

Inabidi uwe smart.

Uwe na uwezo wa kuona mbali na kushawishi potential investors.

Ukikutana na wageni usiongee ujinga. Shusha nondo.

Hapa JF tunasema “ficha upumbavu, onyesha weledi wako”

2 • Usiogope kuuza service yako kama local guide.

Yes.

Kama tayari una ufahamu mkubwa wa eneo unaloishi unaweza kuwauliza wageni wako iwapo watakuwa tayari kukulipa fedha ili uwapatie service yako kama local guide.

Kumbuka watu hawatokupa pesa iwapo hujawauzia kitu.

Usijifanye utaonekana vipi. Uza huduma na muda wako.

Hivyo ndiyo tunavyofanya kwenye hii industry.

Kwamfano wewe unafahamu waterfall fulani na wageni wanataka waende hapo. Hiyo ni opportunity ya wewe kuuza hiyo kazi.

Unachotakiwa kufanya ni kuandaa maelezo ya sehemu unayotaka uwapeleke na bei unayopendekeza.

Do you get the point?

Ok hapa kuna mbinu ninaweza kukufundisha namna yakuandaa hii. Niandikie makingmoneyonlinetz@gmail.com nitakusaidia.

3 • Jitahidi ku-improve kuongea Kiingereza ili uwasiliane vema na wageni wako.

Ngoja nikwambie kitu.

Ili watu wakuelewe zaidi inabidi uwe na uwezo wakujieleza vizuri katika lugha mnayo tumia kuwasiliana.

Lakini nikutoe hofu kupokea wageni kupitia CouchSarfing ni mwanzo waku-improve Kiingereza chako kwasababu utapata nafasi yakuongea na wageni direct.

Usiogope kukosea au kujiona huwezi.

Haya mambo hayahitaji degree.

Ni kuwa tayari tu.

Kama bado hujui utaanza vipi usisite kuniandikia.

4 • Kila unapopata mgeni hakikisha amekuandikia review baada ya kumaliza muda wakukaa hapo kwako.

Hizo picha nilizoonyesha hapo juu ni reviews.

Kadiri unapopata review nzuri ndivyo wageni wanakuamini zaidi.

Pia kumbuka kama utawaibia au kuwakwaza wageni watakuandikia review mbaya na hakuna mtu atakayekuamini.

Kwahiyo jitahidi kuwa mkweli katika mambo yako yote.

Binafsi mgeni akisoma reviews zangu nyingi na zote ni positive lazima atanitumia ujumbe tu.

Na hapo ndiyo mwanzo wa mimi Kutengeneza pesa.

5 • Tumia muda wako wa free ku-hung out na wageni walipo kwenye mji wako lakini hawajafikia kwako.

Yes.

CouchSurfing inatoa nafasi ya wageni kukutana na locals labda mkapata lunch au kahawa.

Lengo ni Kutengeneza urafiki lakini pia wewe mwenyewe kumfahamisha mgeni mambo mengi kuhusu mji unaoishi.

Mambo yapo mengi yakuonge wakati mnapata lunch au coffee.

Inaweza kuwa tamaduni ya watu wako, sehemu za utalii katika mji wako au hata mipango yako ya maisha tu.

Kamwe usiwe kama baadhi ya watu wakikutana na wageni wanaanza kubonyeza bonyeza simu.

Kuwa mcheshi.

Usiwe awkward ukiwa mbele ya watu wapya.


Ok, kwa leo ngoja niishie hapa. Tukutane tena siku nyingie katika darasa amazing kama hili.
 
Thought one.

Vijana Tz inabidi waamke.

Internet imetoa nafasi kubwa tumia kwa manufaaa.

Kuwa mkweli lakini pia Jifunze kuona opportunity.

Hapa inabidi uwe na entrepreneurial mindset.

Lakini pia Emotional Intelligence.

Ukisubiria ajira utazeekea nyumbani.

Anza kutengeneza opportunity zako mwenyewe.

Does that make any sense to you?
 
Kawaida... Ila hongera... Na wewe Fanya ufunge safari uweze kupokelewa na wao huko makwao... Ulale usiku miwili... Kwa budget ndogo...

Uzi wa watafuta maisha nje wa lusungo na izzo na wenzie ulieleza mengi haya unayo yasema...

I’m sharing my experience.

I don’t know people you mentioned.

I think many people will find this thread helpful.

Kama wewe ulishafahamu je, knowledge uliyopata imekusaidiaje?

Can you share please?
 
Umesomeka mkuu ila naomba unisaidie kitu vijana wengi bado hatujasimama vizuri kiuchumi kitu kinachopelekea kuishi maisha local sana mfano kuishi chumba kimoja kwenye Nyumba ya kupanga.. Je kwenye hiyo site hawajaweka vigezo na pia masharti ya mazingira yanatakiwa yawe au unapiga picha mazingira unayoishi then unaupload ili mtalii awe huru kuchagua mazingira anayotaka? In short nahisi umeandika machache wakati kuna mengi ya kutujuza.
 
Hongera, mimi ni memba wa hilo group. Ila kuna wajinga watakuja jitokeza baka wasichana.

Si rahisi sana.

Wageni wengi wanafahamu namna gani wanaweza jilinda.

Pia Wageni wengi na “smart” sana kufahamu kwa haraka iwapo kuna hali fulani ambayo si sawa.

Energy yako inakutambulisha kila kitu.

Trust me ukikaa na watu toka mataifa tofauti utaona hili wazi.
 
Ili uwe verified unatakiwa kulipa 138000. Haya hajasema. Naona harufu ya utapeli hapa

Sasa wewe unakurupuka huelewi lolote unaniita tapeli.

Hiyo inalipwa CouchSurfing na pia si lazima.

Kila unapopokea mgeni na kukaa kwako unapewa muda wakuendelea kuwa mwana chama bure.

Mimi nipo toka 2016 na sijalipa hata senti.

Pia kuwa verified unaweza tumia number yako ya simu tu.

You are so stupid young man.
 
Back
Top Bottom