Anne Makinda: Sitogombea tena ubunge 2015

Anne Makinda: Sitogombea tena ubunge 2015

Huuu unafiki mkubwa kweli anasema akakope ili ajenge haya ni ya kweli au kutudharau tunasubiri mikopo ili tujenge? Makinda ni kweli hadi leo hana hata nyumba? alishakuwa mkuu wa mkoa,mbunge na leo spika.....kweli bibi kiroboto ameamua kututukana....Na hili ndilo lifanywalo na viongozi wa Tanzania wakidhani kuwa sisi hatuna akili......mi nimeona kama yule mama sasa kachanganyikiwa...
Niliwahi kusikia mwaka jana kwenye vyombo vya habari na magazeti kuwa mama huyu amefunga njia inayopita kwenye nyumba yake ya ghorofa mjini DSM (sikumbuki ni eneo gani)!
 
Mh. Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano amesema kuwa hato gombea ubunge chaguzi mkuu ujao. Amesema anataka kukopa pesa arudi kujenga nyumba.

Sorce: ITV, HABARI YA SAA MBILI

mbunge kwa 30yrs+ halafu anasema nini kuhusu kujenga nyumba?

Au alikuwa anatumia ujira wake wote kutafuta ubunge?
Huu ni ukenge, anatuona sisi makenge wenzie!!
 
nimesoma kwa tahadhari taarifa ya Mama Makinda kuhusu kutogombea tena ubunge huko kwake njombe, lakini hakuna mahali popote pale aliposema ataachana na siasa. wengi mwameanza kumpa hongera, lakini ukweli ni kuwa hatagombea tena ubunge wenye maslahi duni bali USPIKA


katiba ya nchi yetu inatamka wazi kuwa spika si lazima awe mbunge, na anajua kuwa anaweza kugombea uspika bila kugombea ubunge.

hii haitakuwa mara ya kwanza. mnamo mwaka 2000, piuce msekwa alitangaza kuwa asingegombea tena ubunge wa jimbo la ukerewe, na kweli hakugombea ubunge kiti kile akamwachia mama mongela getrude, yeye aligombea uspika na alikuwa spika kwa kipindi cha 2000-2005 bila kuwa mbunge.

nawsilisha
 
pengine anafuga majini kwa hiyo yanamgarimu sana.we vijana wameingia juzi maisha yao juu
 
Patachimbika bila jembe, huyu mama hatakiwi kuwa spika tena, inabidi wananch tuingilie kati
 
Bora aachane na siasa kabisa,akalime zake chai na kuendeleza biashara zake ndogondogo kule kwao!itakuma afadhali.
 
unajua mpaka kufika 2015 upepo utakuaje kisiasa nchini kumbuka maamuzi yanakwenda pamoja na hali halis ya makati huo
 
  • Deo Mwanyika mbunge 2015 Njombe

Let us support him because of his inspirational ideas, CREATIVE STRATEGIES!

DEO MWANYIKA HOYEE! OUR 2015 MP NJOMBE, AS A FAVORABLE REPLACEMENT TO MAKINDA.

Take further note: TUMUUNGE MKONO JANANI WANYALU!
Peleka kampeni zako za kijinga kwa wajinga wenzako. Huna hata aibu kumkampenia huyo kibaka wako hapa kwa Great Thinker?
 
aNASEMA NUSU YA WABUNGE WANATAKA KUACHA uBUNGE. Hivi huyu mama amewahi gombea Ubunge hata mara moja kweli?
 
Dear 'Kimboka one' inaonekana ni mbumbu wa sheria.Katiba yetu inampa kila mtu fursa ya kutoa maoni yake ili mradi tu havunji sheria nyingine za nchi. Je nimekukosea nini katika mchango na maoni yangu? Makinda ameshasema hatagombea tena Njombe kusini.Mimi nimeleta pendekezo langu la MP mtarajiwa. Kama wewe una nia njema na jimbo letu leta pendekezo la mtu wako tumjadili, not otherwise.
 
Ningefurahi kama Mama Makinda angetangaza KUJIUZULU nyadhifa zoote kabisa katika safu ya utawala wa nchi hii. Miaka minne ni mingi mno kuendelea kuwa na uongozi mbovu kama wa huyu mama ndani ya bunge. Makinda alizuia mjadala wa mgomo wa madaktari SIX times! Amebadilisha kanuni za bunge ili iwe rahisi ku-rubber stamp mambo! Amegeuza bunge kuwa taasisi ya serikali, amesimamia/amelazimisha upitishwaji wa sheria mbovu kama ule muswada wa kutunga katiba mpya. Kama sio busara ya CHADEMA tungekuwa na sheria mbovu kabisa. Miaka minne ataharibu mangapi?

Halafu huyu mama anaishi dunia gani? Kwa mliomuona huyu mama wakati anaongea na wakazi wa Njombe mtakubaliana na mimi kuwa wale wazee wamechoka, wamepauka kama ilivyo kwa sehemu nyingi Tanzania. Makinda anapata wapi ujasiri wa ku-park shangingi lake pembeni na kuwahutubia watu kuhusu umaskini wa wabunge? Watu waliochoka vile? Given the choice naamini wale wazee watachagua umaskini wa wabunge any day! Viongozi wetu waache kujikweza.

In -fact ningeshauri kwenye katiba ijayo, katiba ya wananchi, wabunge waitwe NDUGU. Vituko vilianza tangu pale walipoijiamulia kujiita WAHESHIMIWA. Tukakate kabisa hii tabia ya kujikweza. Neno msheshimiwa lizikwe na hii katiba ya CCM.
 
Wakati fulanii iliripotiwa kuwa alizuia barbara eneo fulanni Dar akijenga au alikuwa mkandarasi?
 
Watanzania wanatukanwa kisha wanapiga makofi.Kauli ya Makinda kuhusu kujenga nyumba ni matusi
 
kama miaka yote hakujenga, atawezaje kujenga sasa na huo mkopo ataulipaje. danganya wanakijiji.............
 
Kwenye mpira na michezo kwa jumla, Mzee Rukhsa alisema Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu - alikuwa sahihi.
Na sasa kutokana na tabia ya magamba kukimbilia vyombo vya habari kumwaga u.h.a.r.o wao, sasa wamekuwa na "vinywa vya wendawazimu".
 
Yaani baada ya miaka 17 ya kuwa mbunge leo ndio anakumbuka kuwa ni ubunge ni umasikini..sitaki kuliamini hili hata kwa mtutu wa bunduki.
 
Back
Top Bottom