Anne Makinda: Sitogombea tena ubunge 2015

Anne Makinda: Sitogombea tena ubunge 2015

Anaeweza kumshauri amshauri ajiuzulu sasa hivi asisubiri 2015.
Mh. Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano amesema kuwa hato gombea ubunge chaguzi mkuu ujao. Amesema anataka kukopa pesa arudi kujenga nyumba.

Sorce: ITV, HABARI YA SAA MBILI
 
Huyu mama Kiroboto ameshaingia kwenye ufalme wa wateule wachache wa nchi hii.
Hilo la kukopa na kujenga nyumba ni CHANGA LA MACHO.

Kumbuka BUNGE ni MHIMILI mwingine wa dola. Ambao kulingana na
katiba yetu ni SPIKA NI KIONGOZI wa KITAIFA ambaye ataendelea
kuhudumiwa na kodi zetu maisha yake yote. Na hata atakapofariki
basi watoto wake, wajukuu wake, vilembwe vyake vitaendelea kuhudumia
na kodi zetu kama Nyerere, Kawawa, Sokoine etc . Hivyo asidanganye
yeye, ana UKWASI mkubwa.

Kulingana na sheria ya mafao ya viongozi wa Kitaifa akiwemo SPIKA
kama atastaafu basi atapata 80% ya mshahara wa spika aliyeko madarakani,
mishahara ya wasaidizi wawili, dereva mmoja, ofisi, mafuta ya gari @ mwezi,
kutembea nje ya nchi at least mara mbili kwa mwaka, kutibiwa nje ya nchi atc.

Sasa anataka kutudangaya nini? Mimi siwezi kuhudhulia mikutano ya viongozi
wa CCM kwa jinsi wanavyomwaga pumba. Ninaweza kukosa uvumilivu nikamzaba kibao
kama yule kijana aliyemzaba Alhaji Alli Hassan Mwinyi, Yaani wanakera ni pumba
kwa kwenda mbele!

SIJUI LINI TUTAPATA KATIBA MPYA TUONDOE HUU UOZO!
 
huyu ni muongo yale mabasi ya SUPER FEO DAR- SONGEA NI YAKE PESA KAZIONA WAPI?
Nakusanya ushahidi kuhusu mali zake nikiukamilisha nitaumwaga hapa jamvini.

haya mkuu tunausubiri
 
hatumuhitaji,akapumzike asubirie kupewa ukuu wa mkoa maana ndiyo zao
 
Siamini maneno ya wanasiasa kuhusu kugombea. 2015 atakuja na kusema wapiga kura wake wamemwomba agombee tenna!!
 
teheteheteheehetehetttotjtothtithttthtthttitititiiiiiiikwkikwikwiwkwiwkwiwkwiwkwiwwiwiiiiiiiiiiiiiiii
 
Mh. Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano amesema kuwa hato gombea ubunge chaguzi mkuu ujao. Amesema anataka kukopa pesa arudi kujenga nyumba.

Sorce: ITV, HABARI YA SAA MBILI

:A S embarassed:AKOPE HELA???? HUYU BIBI SIJUI TU
 
Nani angemchagua?????? Bora amelijua hilo mapema kukwepa aibu??? Mwache akalee wajukuu.
 
Mimi nafikiri huyu mama hakutafakari kwa makini suala hili na pengine tu amalijibu kutokana na jaziba ya kushutumiwa ile posho waliyoamua kujilipa ambayo imekuwa ndio gumzo.Lakini angeangalia suala hili kwa mapana zaidi au wabunge wengine wenye mtazamo kama wake,kwanini kuwe na matabaka nchini yaani wengine ni muhimu zaidi kuliko wengine? Je Walimu,Madakatari na watumishi wengine wa umma tunawaweka katika nafasi gani?
Nafahamu hali ya uchumi ni mbaya na hii inatokana na nchi kutozalisha bidhaa ambazo zinaweza kucompete na bidhaa za nje,pia kila mtu katika nafasi yake awajibike ipasavyo kwani utamaduni wetu sisi wabongo hatupendi kufanya kazi,Hebu tujaribuni kuangalia jirani zetu kama wakenya jinsi wanavyojituma tumekalia tu porojo nyingi,siasa hata mahali pasipohusika,malalamiko ndio usiseme.
Hebu chukulia mfano katika familia moja kama mzazi ambayo ndio serikali anawatreat wanawe tofauti aidha kwa kuangalia sura au vipaji je hakutakuwa na malalamiko? na je huyu mzazi kama kipato chake kitakuwa kimeongezeka hataweza kuwaridhisha hawa wanawe na kuondoa tofauti iliyopo?
Basi tuondoe ubinafsi (Ufisadi) tushirikiane wote kwa pamoja kwa kidogo tulichonacho,tufanye kazi kwa bidii tuone kama kutakuwa na malalamiko.
Hatuwezi kuchukua mfano mmoja tu wa wabunge wa Tanzania na tukajilinganisha na maslahi ya wabunge wa nchi zingine tutakuwa tumepotoka chamsingi angalia kipato cha mwanachi kwa mwaka hata kama mbunge angepata mamilioni ya pesa dhidi ya wananchi je kuna faida gani?
 
mama huyu alishindwa kujua hadhira yake ikoje tena inaonekana anamfadhaiko wa kiakili kwa kuwa alikuwa akiongea na wananchi wakemasikini, wamechoka kimwili n kiroho naye akiwa hoi kiakili akaishia kusema maneno yakiingereza wabunge ni frastrated group n mimi naongea fact tu kama Mkristo.

ameonyesha ukomavu katika jambo moja kusimamia posho na kuitetea hivyo ninaona kuna ulazima wakuzipitia posho hizi nakuona tija yake kwakuwa wabunge kama wawakilishi wetu wameona hicho ndicho kiasi kitakachowawezesha kuwa na maisha bora ila walisahau tu kutetea posho zao na posho za watumishi wengine wa umma kwa wakati mmoja wakidhani kuwa Watanzania bado tumelala usingizi wa pono.

wanapaswa kujipanga naakuja kwa upya na mkakati wakuboresha maslahi ya watumishi wa umma na mashirika ambapo moja kwa moja itapelekea kuongezeka kwa kipato kwa makundi mengine kama wafanyabiashara, wakulima etc.
 
anasema ubunge ni umaskini sasa sijui kwa nini wanautafuta kwa gharama kubwa

Alishasoma alama za nyakati, 2015 CDM wakichukua nchi kweli ubunge utakuwa ni umasikini maana mbunge atakuwa mtumishi wa watu na wala sio bwana ka ilivo kwa magamba sasa....
 
Mh. Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano amesema kuwa hato gombea ubunge chaguzi mkuu ujao. Amesema anataka kukopa pesa arudi kujenga nyumba.

Sorce: ITV, HABARI YA SAA MBILI

Atalipa huo mkpo na pesa gani?
 
Mh. Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano amesema kuwa hato gombea ubunge chaguzi mkuu ujao. Amesema anataka kukopa pesa arudi kujenga nyumba.

Wajameni, kujenga nyumba gani tena? Kwani ya kule Sinza/Kijitonyama alikowafungia wananchi njia wakati akijenga, hiyo siyo nyumba? Au haimtoshi?Wanashindana kujenga nyumba hawa?
Namtakia heri katika maisha yake ya kustaafu na kula pensheni, ambayo kwa mwezi ni kubwa kuliko kipato cha madaktari 200 kwamwezi!
Nenda Makinda! Nenda kajipumuzikie! Nenda Anna! Nenda!
 
Back
Top Bottom