Anne Kilango Malecela awa bubu ghafla

Mkuu,hoja ya awali haikuhusiana na swali wapi alipo ndugu Kilango kwa sasa.
Hoja ilikuwa ni zipi zaweza kuchukuliwa kama sababu za ukimya wake kadiri mada inavyoeleza.

- Wakati wa kusaini karatasi ya Zitto, hakuwepo alikuwa Same kwenye kutayarisha kufungua kiwanda alichokijenga kw ajimbo lake, na sasa bado yupo huko, mara ya mwisho aliipinga hoja ya Serikali ya kuwaondoa ma-DC kwenye katiba mpya, na akafanikiwa kuiondoa!

William.
 
- Wakati wa kusaini karatasi ya Zitto, hakuwepo alikuwa Same kwenye kutayarisha kufungua kiwanda alichokijenga kw ajimbo lake, na sasa bado yupo huko, mara ya mwisho aliipinga hoja ya Serikali ya kuwaondoa ma-DC kwenye katiba mpya, na akafanikiwa kuiondoa!

William.
Kwa hiyo mkuu unaamini kabisa ndugu Mbunge alipanga vyema vipaumbele hapo.wakati taifa linajadili ripoti nyeti yeye yupo Same!
Kazi za mbunge ni kujenga viwanda kweli!!hiyo inapatikana wapi katika majukumu ya kikatiba ya mbunge!Kwa mwendo huo hatashindwa kuwagawia wananchi kanga na chumvi!
Moja ya majukumu ya Kikatiba ya mwakilishi wa wananchi ni kuiwajibisha serikali..Kushiriki majadiliano juu ya ropoti ya CAG ni moja ya majukumu hayo.Sasa ana tofauti gani kimsingi na Mkulo kwenda Marekani wakati wizara yake inajadiliwa...wabunge wote wakiamua kuiga ubunifu wa Ndugu Kilango nani atabaki bungeni kuiwajibisha serikali!Wabunge wakishindana kuzindua viwanda nani ataibana serikali ijenge viwanda!
Kuhusu msimamo wake kuhusu nafasi ya wakuu wa wilaya,ni kama alikuwa analenga kuwatetea wakuu wa wilaya na CCM na si wananchi.
Anaelewa ,nawe waelewa ,kuwa wengi wa wakuu wa wilaya ni makada wa CCM wasio na elimu wala uwezo wa kutosha kuongoza wananachi...Anajua ,kama nawe ujuavyo, kuwa wengi wa ma DED si makada wa CCM,wengi wao ni technocrats na wasioyumbishwa kirahisi na watawala.Siamini kama kweli alitenda haki kwa wananchi wa SAME katika hili.
 
Kwa hiyo mkuu unaamini kabisa ndugu Mbunge alipanga vyema vipaumbele hapo.wakati taifa linajadili ripoti nyeti yeye yupo Same!
Kazi za mbunge ni kujenga viwanda kweli!!hiyo inapatikana wapi katika majukumu ya kikatiba ya mbunge!Kwa mwendo huo hatashindwa kuwagawia wananchi kanga na chumvi!
Moja ya majukumu ya Kikatiba ya mwakilishi wa wananchi ni kuiwajibisha serikali..Kushiriki majadiliano juu ya ropoti ya CAG ni moja ya majukumu yake ya msingi kabisa.Sasa ana tofauti gani kimsingi na Mkulo kwenda Marekani wakati wizara yake inajadiliwa...wabunge wote wakiamua kuiga ubunifu wa Ndugu Kilango nani atabaki bungeni kuiwajibisha serikali!
Kuhusu msimamo wake kuhusu nafasi ya wakuu wa wilaya,ni kama alikuwa analenga kuwatetea wakuu wa wilaya na CCM na si wananchi.
Anaelewa ,nawe waelewa ,kuwa wengi wa wakuu wa wilaya ni makada wa CCM wasio na elimu wala uwezo wa kutosha kuongoza wananachi...Anajua ,kama nawe ujuavyo, kuwa wengi wa ma DED si makada wa CCM,wengi wao ni technocrats na wasioyumbishwa kirahisi na watawala.Siamini kama kweli alitenda haki kwa wananchi wa SAME katika hili.

- Duh!

William.
 
Hadi sasa kwa mujibu wa katiba yetu kazi za mbunge si kutumia pesa zake binafsi kujenga miundombinu ya kiuchumi ikiwemo viwanda ,madaraja na visima.
Majukumu muhimu na halali kabisa ya wawakilishi wetu ni kuibana serikali itunge sera,mipango,sheria na mikakati mbalimbali ikiwemo ya maendeleo ya viwanda nchini na wala si jimboni kwake pekee.
Yaelekea Ndugu Kilango anataka kuvaa joho la muwekezaji ama mfadhili!
Iwapo ungepata ubunge wa EAC siamini kama moja ya mikakati yako ingekuwa ni kujenga viwanda Tanzania!
Badala yake ungezibana serikali za EAC kuweka mkazo katika ujenzi wa viwanda katika nchi za EAC.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom