Anne Kilango alazwa Hospitali Dodoma

Anne Kilango alazwa Hospitali Dodoma

Mwiba

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2007
Posts
7,607
Reaction score
1,764
kilangohospital.jpg


Mwenye nyepesi atujuvye amesibika na nini ?
 
Ahhh, Mwiba,
Tayari ni mahututi? Hata mirijamirija hana hapo pembeni, mwenyewe kapumzika tu.
Labda ni ile JKT inasemwa "... ana C ya matron....."
 
Kilango alazwa hospitali Dodoma

  • Afanyiwa operesheni chap chap


Kilangop%20hsp.jpg

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda (kushoto) na mkewe Tunu (kulia), wakimfariji, Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela ambaye amelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa matibabu.


Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anna Kilango Malecela, amelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma baada ya kufanyiwa operesheni ndogo.

Mbunge huyo alilazwa juzi jioni mara baada ya kupitishwa kwa Bajeti ya Wizara ya Mali Asili na Utalii.

Ilikuwa ni baada ya hoja yake ya makontena yaliyokutwa na nyara za serikali yaliyokamatwa nchini Vietnam na Ufilipino kujibiwa.

Akizungumza na waandishi wa habari hospitalini hapo Kilango alisema tatizo lilililomfanya afanyiwe operesheni lilikuwa linamsumbua kwa muda mrefu.

“Ni tatizo dogo tu lililonisumbua na ndilo lililonifanya nifanyiwe operesheni, a hata jana pale nje nilipokuwa nazungumza nanyi, niliwaambia kuwa nawahi hospitalini kwa sababu nilikuwa na ahadi ya kuonana na daktari wangu juu ya suala hili,,” alisema.

Hata hivyo, alisema anaendelea vizuri baada ya kufanyiwa operesheni hiyo.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mkewe Tunu, walimtembelea Mbunge huyo kumjulia hali.

Naye Spika wa Bunge la Jamhuri Samuel Sitta ambaye pia alikwenda kumjulia hali Mbunge huyo, alisema hali ya mbunge huyo ni njema na kwamba tatizo lililomfanya afanyiwe operesheni ni dogo.

Wengine waliokwenda kumjulia hali Mbunge huyo ni Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda pamoja na wabunge mbalimbali.

Mbunge Kilango amekuwa ni mwiba mkali katika mapambano dhidi ya mafisadi hapa nchini.

Wiki iliyopita, Mbunge huyo aliitia kiwewe Wizara ya Mali Asili na Utalii baada ya kutoa kauli kuwa atawasilisha hoja bungeni ya kutaka kuundwa kwa kamati itakayochunguza wizi wa nyara za serikali zilizobainika nchini Vietnam na Ufilipino hivi karibuni iwapo hatapewa maelezo ya kuridhisha na Waziri wa wizara hiyo, Shamsa Mwangunga.

Hoja hiyo iliungwa mkono na wabunge wengi ambapo wakati wa kujibu hoja za wabunge, Waziri Mwangunga alimsihi Mbunge huyo kutowasilisha hoja hiyo kwani tayari serikali ilikwishaanza kuchukua hatua juu ya suala hilo.


CHANZO: NIPASHE
 
Hicho chumba cha mgonjwa ni VIP Room nini ? Yaani we wacha tu.
 
Hicho chumba cha mgonjwa ni VIP Room nini ? Yaani we wacha tu.
wki wki wki Ustake ncheke mie
Maana unaona hapo hata mama PM Tunu Pinda imebidi akae kwenye kitanda cha mgonjwa, amenikumbusha vile vituo vyetu vaya afya huko kijijini, utofauti hapo mashuka yamefuliwa na amelala kitandani badala ya sakafuni
 
Ngoja nivute pumnzi kwanza maana zitakuja story nyingi za ajabu ajabu kuhusu huyu mama.
 
wki wki wki Ustake ncheke mie
Maana unaona hapo hata mama PM Tunu Pinda imebidi akae kwenye kitanda cha mgonjwa, amenikumbusha vile vituo vyetu vaya afya huko kijijini, utofauti hapo mashuka yamefuliwa na amelala kitandani badala ya sakafuni
tetetetetetetetetethhhhhhhhhhhhh
Sasa nambie ungelikuwa wewe Mbogela hali ingekuwa vipi?
Hospitali zetu zinatia huruma. Ndio sababu wote wanakimbilia nje.
Hapa uonavyo ujue ndio ilani za chama zimetekelezwa. Tetetetetetehehehehehehe
 
tetetetetetetetetethhhhhhhhhhhhh
Sasa nambie ungelikuwa wewe Mbogela hali ingekuwa vipi?
Hospitali zetu zinatia huruma. Ndio sababu wote wanakimbilia nje.
Hapa uonavyo ujue ndio ilani za chama zimetekelezwa. Tetetetetetehehehehehehe

Ndio ninachosema mkuu huyo mgonjwa na hadhi ya diplomat, na anayemwona hapo ni PM kachumba ndio hako. Unajua wenzetu wa ulaya magharibi wameendelea kwasababu wote wanatibiwa katika mazingira sawa, na wote wanakuwa coverred na insurance, kwa hiyo ilikuwa ngumu insurance kumpeleka mwingine nje na mwingine kumwacha ndani. Ikawalazimu kujenga huduma ya afya itakayowapa nafasi sawa wote. Ije itokee tuamua kuwa ukienda nje uende kwa pesa yako mfukoni kwani kama ni pesa ya serikali kwanini wanegine wawe na haki ya kutibiwa nje na wengine ndani???
 
Ndio ninachosema mkuu huyo mgonjwa na hadhi ya diplomat, na anayemwona hapo ni PM kachumba ndio hako. Unajua wenzetu wa ulaya magharibi wameendelea kwasababu wote wanatibiwa katika mazingira sawa, na wote wanakuwa coverred na insurance, kwa hiyo ilikuwa ngumu insurance kumpeleka mwingine nje na mwingine kumwacha ndani. Ikawalazimu kujenga huduma ya afya itakayowapa nafasi sawa wote. Ije itokee tuamua kuwa ukienda nje uende kwa pesa yako mfukoni kwani kama ni pesa ya serikali kwanini wanegine wawe na haki ya kutibiwa nje na wengine ndani???

Mbogela,
Hata West wana grade. Nina jamaa zangu wawili ma Dr. huko UK na wote wanasema wazi kabisa kuwa kuna classes.

Ila ukweli ni kuwa tofauti zao ni ndogo na si kubwa sana kama zetu. Sanasana anasema kuwa kule kuwaona wale Madr. bingwa ndiyo kimbembe. Sanasana utaishia huko kwa akina dr........... Yale majina makubwa yamewekwa kwa ajili ya watu wenye hela zao, majina yao na labda USUBIRI na tena kwa kipindi kirefu.
Ila ukweli ni kuwa heri utibiwe UK kwenye low class kuliko Tanzania kwenye high class. Hii ndiyo tofauti iliyopo..........
 
Mods,
Badilisheni heading ya hii topic. Hayuko mahututi!
 
Mbogela,
Hata West wana grade. Nina jamaa zangu wawili ma Dr. huko UK na wote wanasema wazi kabisa kuwa kuna classes.

Unajua sisi watanzania wengi tuna habari nyingi za marekani na UK. na kwa ujumla marekani hawafanyi vizuri kwenye eneo la afya, wanafanya viabaya sana. lakini Ukiangalia western Europe kama uholanzi, ubelgiji, wana mfumo mzuri sana wa afya, nchi za scandnavia zina mfumo ambao hauna tabaka kabisa, wanaongoza kwa kutoa haki sawa kwa watu wote. UK huduma yao ni Public lakini bado kuna mapungufu, lakini huwezi kufananisha na huduma yangu ya Muhimbili au ya Kijijini kwangu Makete ninakohitaji kutembea kilomita Kumi hadi ishrini kuweza kumwona Clinical officer (Form IV na miaka 2 ya medical class)
 
Hizo ndizo Hospital zetu na tena hapo alipolazwa Mheshiwa Mbunge Kilango ni pa zuri saaana.

Nenda Ilala Hosp au Mwanyamala achilia mbali za mikoani Utatoa chozi
 
Mbogela,

Ila uzuri wa UK, wanatibu mtu yeyote. Waswidi washenzi sana. Kama huna BIMA basi utaenda kula POLISI. Ila uzuri wa Waswidi ni ile sheria yao ya mtu asilale nje wala asilale na njaa. Wakati sidhani kama UK inafanya kazi. Kila sehemu kuna mapungufu yake. Juu ya Holand na Belgium sina habari ingawa mshikaji wangu mmoja akija huku mwezi ujao basi atanipa habari kamili jinsi wanavyofanyafanya huko Holland.

Nakumbuka mwaka fulani mama aliugua, basi ikabidi twende kwanza Sikonge Moravian Hospital umbali wa maili nane na kuomba kuchukua ambulance. Wakati huo ikatengenezwa machela na kuanza kumbeba na wakakutana na ambulance njiani. Kweli Mipingo tunaofikisha miaka 20, basi ni well selected genes.
 
MUNGU amponye mama arudi kwenye mapambano mpaka kieleweke.
 
Mbogela,

Ila uzuri wa UK, wanatibu mtu yeyote. Waswidi washenzi sana. Kama huna BIMA basi utaenda kula POLISI. Ila uzuri wa Waswidi ni ile sheria yao ya mtu asilale nje wala asilale na njaa.

Yaa lakini la msingi ni kuwa kila mtu ana BIMA, hata walala hoi, Utaratibu umewekwa kuwawezesha watu wote kuipata hiyo BIMA. Ndivyo ilivyo hata Uholanzi na ubelgiji. Shida ya wadau wengi wanaotoka Bongo huwa nataka kuishi huko mamtoni bila kufuata taratibu hizi, watu wao wote wanalipia BIMA, wabantu tunatafuta mianya ya kukwepa, na ukikwepa kwa kweli hapo hakuna cha nini wala nini utakufa wanakuangalia. TIMIZA WAJIBU DAI HAKI. Kwa Mfano uholanzi kutoa viungo kama Ini, Figo, Moyo ni jukumu la kila raia na watu karibu wote wamejiandikisha kuwa donors, na inapokuja kuwa unahitaji kiungo kama hicho huhitaji kutngaza magazetini kuwa unataka kununua, ni wajibu wa madakatari kutafuta donor akupe kwani hata wewe ni Donor. Lakini Angalia Utaratibu wa benki ya damu hapa Nyumbani, inatakiwa kila anyetoa damu awe na cheti na siku akipungukiwa damu apewe bure na haraka, lakini bado utaambiwa tafuta ndugu akutolee damu, hata kama umepta ajali Bukoba na wewe umetokea Makete.
 
Mbogela,
Hata West wana grade. Nina jamaa zangu wawili ma Dr. huko UK na wote wanasema wazi kabisa kuwa kuna classes.

Ila ukweli ni kuwa tofauti zao ni ndogo na si kubwa sana kama zetu. Sanasana anasema kuwa kule kuwaona wale Madr. bingwa ndiyo kimbembe. Sanasana utaishia huko kwa akina dr........... Yale majina makubwa yamewekwa kwa ajili ya watu wenye hela zao, majina yao na labda USUBIRI na tena kwa kipindi kirefu.
Ila ukweli ni kuwa heri utibiwe UK kwenye low class kuliko Tanzania kwenye high class. Hii ndiyo tofauti iliyopo..........

Mkuu Sikonge,

Hapa UK kama uko NHS hakuna grades, huyo aliyekuambia labda alikuwa anaongelea kitu kingine.

Kuna baadhi ya hospitali wana baadhi ya vyumba vichache kama unataka kulala chumba peke yako basi unalipia kidogo na unalala peke yako. Baadhi ya magonjwa unapewa chumba chako kwahiyo wala hata sio muhimu.

Pesa unayolipia ni ndogo sana kiasi kwamba hata sisi walala hoi tunaweza kama unataka kusiwe na usumbufu wa watu wengi.

Viongozi karibu wote wa serikali hapa wanatibiwa NHS, ni matajiri na wafanyabiashara ambao baadhi yao wanaenda private.

Katika miaka yangu yote ya kukaa hapa sijaona grades. Kingine kilichopo ni kwamba baadhi ya hospitali ni nzuri kuliko zingine. Kwa mfano ukiwa London kwasababu ya watu wengi huduma inaweza kuwa mbaya ukilinganisha na mikoani lakini hospitali kama ni mbaya inawahusu wote maskini mpaka matajiri.

Mtu asikudanganye kama wewe ni maskini UK ni best kwa huduma ya afya, hakuna cha insurance au nini, kila mtu ana haki ya kutibiwa. Hata USA wanatuonea wivu kwa hilo.

Hiyo ya Tanzania ni aibu tupu; hiyo mizee inaunguza mabilioni hapa UK na SA kwa matibabu fake huku hospitali zetu zinakufa. Hata huyo mama Kilango angelazwa tu kule kwa wengine ili labda waone kwamba hizo pesa wanazounguza Ulaya kwa kisingizio cha matibabu ndizo zingetakiwa kutengeneza hospitali zetu.

Operation kama yake hiyo ilitakiwa hata atoke hapo hapo kama tungekuwa tunafanya investment kubwa kwenye huduma za afya. Wanasiasa wa Tanzania ni wajinga mno, kuanzia CCM mpaka upinzani. Ambacho hawajui ni kwamba mpaka ukimbizwe kutibiwa Ulaya tayari ugonjwa unakuwa umeshazagaa na wanaishia kufa tu.
 
Back
Top Bottom