Anguko sasa ni dhahiri

Anguko sasa ni dhahiri

Hizi ngonjera ni vyema angeimbiwa Seif siku aliyokataa mkono wa Shein sababu ile ilikuwa kuutangazia umma kuwa ana chuki isiyo elezeka.

Cha kushangaza ni kuwa wale wale waliompongeza Seif kuwa siyo mnafiki ndiyo wanalialia baada ya hii count attack.

Mwisho wa siku dawa ya bishoo ni kuwa bishoo zaidi yake ni vyema Magufuli naye apongezwe kwa kutokuwa mnafiki kama alivyopongezwa Seif.

Wahenga walisema boss hanuniwi.
 
Visasi vya watu kaskazini vitawatoa roho. JPM kaza uzi watanyoka tu!
Siwezi kukulaumu kwa mtazamo wako huu...naamini wala hujui hata madhara ya hiki ulichoandika
 
...mtu anayejisifia rohombaya wazi wazi sio kwamba hana tu hekima lakini pia hana saburi na hatafakari matokeo ya kauli zake..
.....ningekuwa mimi zaidi ya robo wangepotea...
...mtu akikushinda niambie ndani ya dk.5 uone...
...ningekuwa mimi nisingesaini..
...ningekuwa mimi....
...ningekuwa mimi....

hizi kauli za 'ningekuwa mimi' siyo nzuri... ni dalili ya mtu hatari ambaye anaweza kufanya kitu chochote.
 
.....ningekuwa mimi zaidi ya robo wangepotea...
...mtu akikushinda niambie ndani ya dk.5...
...ningekuwa mimi nisingesaini..
...ningekuwa mimi....
...ningekuwa mimi....

hizi kauli za 'ningekuwa mimi' siyo nzuri... ni dalili ya mtu hatari ambaye anaweza kufanya kitu chochote.
Uhalisia wenye kutia shaka sana
 
Chuki za namna hii hazijengi na zina madhara makubwa.
Jirekebishe...na urudie kusoma post ya Mshana jr.
Ina manufaa kwako pia na inakuhusu moja kwa moja.
John Pombe Magufuli ana chuki na visasi sembuse mimi.
 
Nadhani mnaona upande mmoja wa shilling wale wajomba wameshazoea viboko,sijui kama waliwahi kutia visima,wamefyeka mashamba lakini hukuonyesha kulaani!
 
Kila nikiamka, siioni ile Tanzania yenye kuelekea kwenye matumaini nilio itazama jana.
Kila nikiamka, naitazama Tanzania yangu ikiwa imejaa nyuso zilizo anza kupoteza matumaini na kukata tamaa.
Kila nikiamka, nazidi kupoteza matumaini ya kile chema nilicho kitarajia kesho ya jana ambayo ni leo.
 
Lakini binadamu wanafiki sana:

Huku bara Kubenea alitoa Tamko akiwataka wabunge wa UKAWA kutokushirikiana na wale wa CCM na hata wenye uhusiano wa kimapenzi wauvunje, watu humu walimpongeza sana lakini leo hii ndiyo wanajitia kulaani kauli zenye kuashiria utengano.

Magufuli naye apongezwe pia kwa kutokuwa mnafiki.
 
John Pombe Magufuli ana chuki na visasi sembuse mimi.
Kama unaamini JPM anayanya jambo baya basi isiliige.....
Jitafakari na ujirekebishe...utapata shida maishani wala zisizo na lazima.
Tatizo la chuki, humuumiza zaidi aliyeibeba moyoni.
 
Hizi ngonjera ni vyema angeimbiwa Seif siku aliyokataa mkono wa Shein sababu ile ilikuwa kuutangazia umma kuwa ana chuki isiyo elezeka.

Cha kushangaza ni kuwa wale wale waliompongeza Seif kuwa siyo mnafiki ndiyo wanalialia baada ya hii count attack.

Mwisho wa siku dawa ya bishoo ni kuwa bishoo zaidi yake ni vyema Magufuli naye apongezwe kwa kutokuwa mnafiki kama alivyopongezwa Seif.

Wahenga walisema boss hanuniwi.
1472971550503.jpg
 
Kama unaamini JPM anayanya jambo baya basi isiliige.....
Jitafakari na ujirekebishe...utapata shida maishani wala zisizo na lazima.
Tatizo la chuki, humuumiza zaidi aliyeibeba moyoni.
1.Isiliige
2.Ananyanya(maana ya haya maneno tafadhali)
Wewe ni division five pita mbali na mimi.
 
Huyu mtu wetu anatuangusha hata baba yangu ni kichwa cha familia ila hata mpaka na utu uzima wangu sikupata kumsikia akinena jambo ama lugha ya kufadhaisha familia yake namkubali sana mzee wangu. Ni tafakuri yangu tuu juu ya jambo hili lenye kutia madhila ya kila namna nahisi ukimfwatilia kuanzia kwenye chimbuko kama la mzee wangu hapo juu inaonekana huyu mdau hakuwa wa kuweka umoja toka hapo kwenye ngazi ya chini. Ndivyo ilivyo kuongoza njiti za kiberiti zilizojaa kwenye kasha lake tena zenye baruti za saizi tofauti na zenye milipuko tofauti ni kazi tuu hakuelewa. Nina nyongo niishie hapa tuu .
 
Mtoa maada ameiandika vizuri sana lakini jambo la kusikitisha wachangiaji wanatanguliza ushabiki badala ya hoja,lo that is so sad
 
Anguko la Chama Dola? Hahahahah hahahaha haahah hahah hahahahhhhahah hahahhhhh hahaaahhhhh !!!!
Ngoma ikivuma sana hupasuka na mwenye kiburi akishupaza sana shingo huvunjika mara
Tuwe na tuo tuwe na tafakuri kwenye maneno yetu...mtu anayejisifia rohombaya wazi wazi sio kwamba hana tu hekima lakini pia hana saburi na hatafakari matokeo ya kauli zake..huyu ni mwovu
Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri, bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu, huchochea ghadhabu huchochea visasi chuki na ubabe....dhima ya kiongozi ni kuleta umoja na maridhiano sio kuchochea chuki na visasi
Kiongozi mwenye hekima kamwe hawezi kuongea karaha..karaha huleta simanzi na majonzi, mtu wa karaha hana ogofyo lolote, ni kiburi na kiburi chake ni anguko
Nuru ya mtu mbaya huzimika ghafla bila tahadhari bila taarifa...mtu wa hekima hutengeneza patano kwa njia ya mashauriano
Je tunatengeneza ama tunabomoa?
Je tunahubiri amani ama visasi?
Je tunaeneza ustawi au anguko?
Je Tunafundisha hekima au upuuzi?
-hakuna kitu kibaya kama kuruka mkojo na kukanyaga kinyesi
Kwani hekima ni nini? Inategemea na tafsiri ya kila mtu na mazingira aliyopo. Hekima kwa mwingine siyo lazima iwe hekima kwa kila mtu. Tusidanganyane. Ni mtazamo tu wa kila mtu na kila mtu yuko huru kufikiri atakavyo. Watu wanategemea wanyenyekewe hali wao hawana unyenyekevu wowote. Lazima wavune wanachopanda.
 
1.Isiliige
2.Ananyanya(maana ya haya maneno tafadhali)
Wewe ni division five pita mbali na mimi.
Haya mama nimekupisha.
Spelling errors tu.
Lakini Division Five haiondoi busara ya maneno ninayosema.
Usiangukie katika lile shimo la kudhani Division Five hawezi kujua jambo au kuwa na busara zaidi ya Prof.
Wewe unamtukana matusi na kumkosoa Magufuli (PhD).
Nawe atakujibu pisha hapa huna elimu....
Kwa mtizamo wako huu ni nani atakuwa na kiwango cha elimu kinachostahili kumkosoa au kumshauri Magufuli???
Jirekebishe tena jirekebishe sana.
 
Back
Top Bottom