Anguko la CHADEMA lipo njiani

Mnapotoa tathmini ya jumla kwa CDM kukosa kajimbo kamoja tu kwa nchi yote hii ni kuonesha uwezo mdogo wa kufikiria.
 
Mnapotoa tathmini ya jumla kwa CDM kukosa kajimbo kamoja tu kwa nchi yote hii ni kuonesha uwezo mdogo wa kufikiria.

umesahau uchaguzi wa maiwani, kata 3 kati ya kata ngapi mkuu, na bado mtaanguka chalinze, huko msije kabisa endeleeni na porojo tu, ukifika wakati wa reality huwezi epuka,
 
Mamndenyi; MwanaDiwani; Ritz; Mleta Thread na wengineo wenye mtazamo unaofanana ni lazima muelewe kuna aina mbili za Schools of Thought: Bold Spirits na Timorous Souls. Nyiye ndiyo Timorous Souls yaani mawazo mgando i.e. You don't see beyond your noses. Watu wenye fikra pevu kama Jaji Warioba; Jaji Augustino Ramadhani; Tundu Lissu et el ni Bold Spirits.
 
Kinachowamaliza ndio hiki;
hamjakomaa kisiasa;
hivi unafikiria kuwa naogopa matusi mimi?

na utatukanwa tu 7bu huna tofauti na yule anaesimama pale mkwajuni akijinadi kwa buks 1 or jerrooo
 

CCM hamjawahi kusema ni kwa VIPI CDM wanaendesha Chama Kidini.Zaidi sana mnadhani ni propaganda nzuri ya kupambana na CDM kumbe mnaigawa Nchi katika vipande vya kidini kitu ambacho kitaleta machafuko hapo baadae.Mwanzilishi wa Udini Tanzania 1). Mh.Alhaji Ally Hassani Mwinyi, 2) Ndg.Jakaya Mrisho Kikwete. Wamekuwa wakitumia misikiti kutoa ahadi kwa dini yao, na watu wao, na bado haikutosha, wameitumia CUF kueneza propaganda za kidini kupitia misikiti, ushahidi ulishawekwa jukwaani ukimwonesha Lipumba alichokuwa akikiongea msikitini. CDM haijawahi kupita, au kutumia Jukwaa lolote la kidini kuahidi chochote kwa jukwaa hilo la kidini.

kuhusu unayemwita dogo Mheshimiwa wa Kigoma, hilo suala ni la kipuuzi sana. CDM imefukuza wengi tu,kabla ya huyo Dogo, hatukuwaona CCM mkilalamika na kuwatetea, tunaomba kujua mna maslahi gani na huyu dogo wa Kigoma?Mmekuwa mstari wa mbele kumtetea, na kuona maamuzi ya CDM yalikuwa mabaya, yalikuwa yanawahusu nini hayo maamuzi?Pilipili usiyoila yakuwasha nini?Au mnataka tucopy na kupaste kile CCM wanachoshindwa kukifanya kwa kina EL na wengine ndani ya CCM?Dogo haki yake itaonekana Mahakamani, na Kamati kuu ya Chama kama ipo, kama haipo basi aangalie ustaarabu mwingine.

kuhusu kung'ang'ania madaraka, nadhani CCM imeng'ang'ania madaraka tangu 1964, hilo hamlioni?hatujawahi kuwasikia CCM wakimwongelea Lipumba ama Mbatia kwenye hili suala la Uongozi.CCM kuna watu ni viongozi tangu kabla ya baadhi yetu kuzaliwa hadi leo.Mzindakaya alikaa kwenye ubunge kwa zaidi ya miaka 40.Kingunge yupo serikalini tangu lini?Ina maana CCM ina watu wachache sana wenye sifa za kiuongozi hadi kupelekea watu kukaa madarakani muda wote huo?Niambie, CCM mnapochagua Mwenyekiti Taifa huwa anapambana na nani?Kwa nini?Uchaguzi ni suala ambalo pia linaweza kuahirishwa, kama ambavyo CDM wamesema watafanya mwakani baada ya uchaguzi, kuna kosa gani?Uchaguzi wa CDM una madhara gani kwa CCM au ndo mlishaandaa watu wa kuiua CDM?

Kujisahau kivipi?

Mwisho,kama mnategemea CDM kufa, endeleeni kujaza maji kwenye gunia.Haifi.Matokeo mliyoyapata ni sehemu tu ya changamoto zinazopitiwa na CDM. Kwa Taarifa yako, hakuna Anguko lolote la CDM, nionacho ni propaganda kwamba CDM imeanguka. Tunasubiri Anguko rasmi la CCM.Msidhani kuwa hatujui kinachoendelea ndani ya CCM.MLICHOFANIKIWA ni kuufunika moto unaowaka ndani yenu ila sisi tunaona moshi.

Naamini hakuna mahali nilipokutukana Mamndenyi!
 
CHADEMA haitakufa hata siku moja kama mdhaniavyo. Kinachohitajika sahz ndani ya chama ni malekebisho ya kiujumla.
Wanahtaji viongozi wapya wenye mpango mkakati kuanzia ngazi ya shina na katika kila tarafa pawepo na pionners watakaokuwa wanapata full support mara kwa mara kuzinadi sera za chama na kutoa elimu ya uraia kuhusu democracy na uhuru wa mtu kushiriki uchaguzi pasipo ushawishi au shinikizo.
Mtaji wa CCM ni umbumbu na umasikini wa wananchi hasa wanawake na wazee. Mtaji wa CDM ni vijana ambao kwa mjibu wa takwimu za sensa ndio wengi zaidi. Kinachotakiwa kwa CDM ni kudhibiti mifarakano ndani ya chama na tuijenge nyumba yetu juu ya mwamba.
 
Pamoja na maneno ya kashfa uliyoongeza (ni jadi yenu) ila
jibu lako lina mambo muhimu sana kwa kukiimarisha chama hicho.

 
kumekua na kauli nyingi dhidi ya chadema,wapo waliosema chadema yapukutika,chadema yameguka,chadema yasambaratika,chadema yavurugwa,chadema yagawana mbao,chadema yaweweseka. wewe unasema ' anguko la chadema latimia'. ni mipasho ya kawaida tu,ni kama kulitabiria kifo jiwe la pembeni
 
LENDEYSON nimekusoma hapo juu,
Jitahidini kuimarisha chama chenu walau mkitoe huko icu
kinakopumulia dripu.
 
Aliendika thread hii bila shaka ana mimba changa, naombeni tumsamehe bure.
 

Wachaga wanakimalza chama
 
Hiki ni chama cha mtei na Mbowe hiyo mikakati haina nafasi
 
Mpaka watz waelewe wanavyonyonywa na kunyanyaswa na CCM ni ngumu sana
 
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…