Angellah Kairuki: Tanzania tunapoteza takribani eneo la misitu hekta 469,000 kila Mwaka. Upandaji wa miti ya Mianzi utaleta tija

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
20240219_194706.jpg

Waziri wa Maliasili na Utalii, Angellah Kairuki amesema hayo wakati akitoa Hotuba katika Uzinduzi wa Mkakati wa Kitaifa wa Mianzi (Bambos) kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Chuo Cha Utalii Dar es Salaam, leo Februari 19, 2024.

Amesema “Natambua kwa takwimu za sasa, Tanzania tunapoteza takribani eneo la misitu lenye ukubwa wa hekta 469,000 kila Mwaka.
20240219_194702.jpg

“Hali hii si nzuri kwani kama juhudi za pamoja hazitachukuliwa basi kasi ya kuenea kwa jangwa zitaathiri Nchi yetu na hatimaye kuchangia kwenye kuathiri dunia katika siku za usoni. Hivyo, juhudi hizi za kuendeleza miti ya mianzi ni jambo la muhimu na la kila Mtanzania kuhakikisha kuwa misitu inaendelezwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.”

Ameongeza “Napenda kuwahimiza wadau wote wa Misitu kusoma kwa umakini Mkakati na Mpango Kazi wa Kitaifa wa Mianzi ili kupata picha ya tulipo sasa na kuhakikisha kuwa unatekelezwa ipasavyo ili kuendeleza misitu hapa Nchini.”

Aidha, ameto maelekezo kwa Chuo Cha Viwanda vya Misitu Moshi kwa kushirikiana na SIDO na wadau wengine washirikishwe kutafuta teknolojia za kisasa za kuchakata mazao ya mianzi ili kuyaongezea mnyororo wa thamani na kupata fedha nyingi kwa kuuza mazao hayo ndani na nje ya nchi.
20240219_194657.jpg

Amesisitiza “Ninaielekeza Taasisi ya Utafiti wa Misitu kufanya tafiti za kutambua maeneo sahihi ya kupanda aina mbalimbali za mianzi pamoja na kuiagiza Idara ya Misitu na Nyuki ifanye tafsiri ya nyaraka hizi mbili kwa lugha ya Kiswahili na kuzisambaza. Serikali itaweka mazingira wezeshi kwa wadau wote wa zao la mianzi ili kuhakikisha linaleta tija kwa Watanzania na Taifa kwa ujumla.”
 
Serikali imezindua mkakati wa kitaifa wa mianzi na mpango kazi wake ikiwa ni hatua ya kulinda viwanda vinavyotumia mianzi kama malighafi na pia kulinda uhifadhi wa maliasili nchini.

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki amezindua mkakati huo na utelekezaji wake huku akisema mkakati huo utasaidia upatikanaji wa malighafi kwenye viwanda vinavyozalisha bidhaa zitokanazo na miti ya mianzi.

Kwa upande wake katibu Mkuu wa wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abassi amezungumzia umuhimu wa kutunza misitu na kuwataka wananchi kuendelea kupanda miti kibiashara ili kujiongezea kipato na kulinda uhifadhi.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mianzi Duniani (INBAR) Balozi Ali Mchumo amesem zao la mianzi linaweza kuleta tija kwa Taifa kutokana na kuongezeka kwa matumizi ya mazao yatokanayo na miti hiyo.

GGs_bmNXoAAmH-a.jpg
GGs_djoXoAADlu8.jpg
GGs_fXxW4AAB-8s.jpg
GGs_hd5WIAEKhx2.jpg
 
Wangepambana na kushusha kabisa bei ya gesi ya kupikia ili matumizi ya kuni na mkaa yaishe, hasa katika miji, ingesaidi sana kuokoa misitu.
Angeingea hivi ningemuona wa maana sasa anasema miti ya mianzi? Inatija gani hiyo?
 
View attachment 2909269
Waziri wa Maliasili na Utalii, Angellah Kairuki amesema hayo wakati akitoa Hotuba katika Uzinduzi wa Mkakati wa Kitaifa wa Mianzi (Bambos) kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Chuo Cha Utalii Dar es Salaam, leo Februari 19, 2024.

Amesema “Natambua kwa takwimu za sasa, Tanzania tunapoteza takribani eneo la misitu lenye ukubwa wa hekta 469,000 kila Mwaka.
View attachment 2909270
“Hali hii si nzuri kwani kama juhudi za pamoja hazitachukuliwa basi kasi ya kuenea kwa jangwa zitaathiri Nchi yetu na hatimaye kuchangia kwenye kuathiri dunia katika siku za usoni. Hivyo, juhudi hizi za kuendeleza miti ya mianzi ni jambo la muhimu na la kila Mtanzania kuhakikisha kuwa misitu inaendelezwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.”

Ameongeza “Napenda kuwahimiza wadau wote wa Misitu kusoma kwa umakini Mkakati na Mpango Kazi wa Kitaifa wa Mianzi ili kupata picha ya tulipo sasa na kuhakikisha kuwa unatekelezwa ipasavyo ili kuendeleza misitu hapa Nchini.”

Aidha, ameto maelekezo kwa Chuo Cha Viwanda vya Misitu Moshi kwa kushirikiana na SIDO na wadau wengine washirikishwe kutafuta teknolojia za kisasa za kuchakata mazao ya mianzi ili kuyaongezea mnyororo wa thamani na kupata fedha nyingi kwa kuuza mazao hayo ndani na nje ya nchi.
View attachment 2909271
Amesisitiza “Ninaielekeza Taasisi ya Utafiti wa Misitu kufanya tafiti za kutambua maeneo sahihi ya kupanda aina mbalimbali za mianzi pamoja na kuiagiza Idara ya Misitu na Nyuki ifanye tafsiri ya nyaraka hizi mbili kwa lugha ya Kiswahili na kuzisambaza. Serikali itaweka mazingira wezeshi kwa wadau wote wa zao la mianzi ili kuhakikisha linaleta tija kwa Watanzania na Taifa kwa ujumla.”
Alikua mrembo kipindi cha JK na Magu ila sasa hivi kawa bibi

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Mianzi ina faida gani hasa labda kwa wagema ulanzi! Badala ya kuzungumzia misitu ya maana tunazungumzia mianzi? Au ndio project za watu like parachichi and the like wanamwingiza kingi waziri kuzindua?
 
Let me reserve my comment... Mianzi really 🎧, Dodoma anaionaje na hali ile kama Waziri je ni ngumu kuifanya iwe green city? Wataalamu wa Miti hebu njooni mtupe moja na mbili tafadhali
 
Mianzi ina faida gani hasa labda kwa wagema ulanzi! Badala ya kuzungumzia misitu ya maana tunazungumzia mianzi? Au ndio project za watu like parachichi and the like wanamwingiza kingi waziri kuzindua?
Mkuu ingia youtube tafuta bamboo products utaona faida nyingi sana za mianzi. Kwa ufupi ni dili sana kwa Wachina na watu wa Asia kwa ujumla. Sisi huku tumelala sana na umasikini wetu ni mtaji kwa wanasiasa.
 
Back
Top Bottom