Angekuwa ndiyo Lowassa...

Angekuwa ndiyo Lowassa...

kila uongozi una weakness zake na kila kitu kinachofanyika kina impact zake pia,either positive.negative or both.....hata magufuli ana weakness nyingi sana tatizo linakuja wapinzani wana address vipi hizo kasoro wananchi wote tukaelewa vivyo hivyo ingetokea kwa lowassa endapo angeshinda.....
 
Nchi aieleweki vp, unafukuzwa kazi kivip?huwezi fukuzwa kazi bila sabb,chanjo gani inatafutwa kwa tochi?mlizoe dezo mno fanyeni kazi acheni kulia lia mlizoea wizi wizi tu kila mahali mmebanwa sasa iliyobaki ni kelele na bado
 
Leo watoto wa wakulima wasingebeba mabegi na kurudi makwao kwa kukosa boom wangesoma bure, unafikir nan angempinga kwa hlo.
 
Mkuu Nyani Ngabu, wala usipate shida kupata jibu la swali lako? Je Lowasa alipokuwa CCM si walimtangaza kwenye Majukwaa kuwa ni Fisadi? Hawakufanya hivyo? Muulize John Mnyika, Saed Kubenea, Peter Msigwa, Godbless Lema, Tundu Lissu nk.

Je baada ya kuhamia CHADEMA wameendelea kuimba wimbo wa ufisadi? Thubutu! Nadhani mpaka hapo umeshapata jibu la swali lako. Hawa ndio upinzani
Kweli mkuu! Mwambie pia jinsi ccm walivyokuwa bize kumsafisha kuwa si fisadi,mwambie pia jinsi ulivyotaabika kumtetea huku mitandaoni usiku na mchana! Uliwapa mtihani mgumu kweli pale ulipowaambia Mwenye ushahidi kuwa lowassa ni fisadi aende mahakamani!! Mpaka leo hakuna kibwengo yeyote aliyethubutu kutia pua yake mahakamani!! Ina maana walikuwa wanamzushia tu!! Kweli hawa walikuwa mabingwa wa uzushi! Ila kuhusu Nani anaweza kufanya nini kesho ni some sort of Ushirikina!! Hivi Rungwe angefanikiwa kuinusa ikulu Mnajua angeweza kufanya nini na nini? Hivi kabla ya uchaguzi muliwasikia wananchi wakilalamikia nini zaidi? Upungufu wa aeroplane? Poa basi tunawaongezea nyingine saba!!tena kubwa kuliko meli! And after that tusisikie mtu akinon'gona tena!!
 
kuna binti namfahamu, alijifungua miezi miwili iliyopita kwenye hospitali ya chama ( sory ni ya serikali) akaambiwa chanjo hakuna arudi baada ya wiki, aliporudi akaambiwa chanjo bado hazijaja aache mawasiliano zikija ataaitwa, wiki haijaisha tukazika mtoto.
RIP Kichanga.
 
Hampendi Lowassa wenu asemwe eh?

Halafu hapo hapo usikute nyie ndo mlikuwa mstari wa mbele kumlaani wakati alipokuwa CCM.
Mkuu! Wala hatukuwa kwenye mstari,bali tulisimama out of crowd ili tusikike vyema!! Wewe ulikuwa wapi? Leo uko wapi? Lowassa was a centre of political gravity! Aliyeshinda alishinda kwa sababu ya Lowassa,aliyeshindwa alishindwa sababu ya Lowassa!! Kuna Na wengine tumewajua rangi zao halisi kupitia Lowassa! [HASHTAG]#ulipotupo[/HASHTAG] na hata sasa naendelea kupata mtiririko mpya wa uhalisia wa fikra za wengine kupitia jina lake!! Na Mimi ni sehemu ya hao Wengine.
 
Mkuu! Wala hatukuwa kwenye mstari,bali tulisimama out of crowd ili tusikike vyema!! Wewe ulikuwa wapi? Leo uko wapi? Lowassa was a centre of political gravity! Aliyeshinda alishinda kwa sababu ya Lowassa,aliyeshindwa alishindwa sababu ya Lowassa!! Kuna Na wengine tumewajua rangi zao halisi kupitia Lowassa! [HASHTAG]#ulipotupo[/HASHTAG] na hata sasa naendelea kupata mtiririko mpya wa uhalisia wa fikra za wengine kupitia jina lake!! Na Mimi ni sehemu ya hao Wengine.
Nawe ulizungusha mikono?
 
Sabalkheri wanaJF na Alhamisi njema kwenu nyote na popote pale mlipo pembe ya dunia hii.

Sasa leo hebu tulonge kidogo ki-nadharia tete. Nimekaa kwa muda mrefu sana sasa nikijiuliza juu ya swali hili bila kupata jibu la uhakika.

Tuseme ingetokea mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA ndo angeibuka mshindi wa kinyang'anyiro cha urais mwaka jana.

Halafu baada ya kuanza kazi akafanya mengi kama aliyoyafanya rais wetu wa sasa MTUKUFU Dkt. John Pombe Joseph Magufuli...

Yaani akapiga marufuku safari za hovyo hovyo za nje ya nchi, akaagiza baadhi ya sikukuu za kitaifa tubadili namna tunavyozisherehekea kitaifa, akawa ni mtu wa kukaa nchini muda mwingi na kutuma wawakilishi pale inapobidi, akatumbua majipu hadharani na faraghani, akanunua ndege mpya kwa lengo la kufufua shirika letu la ndege, na kadhalika na kadhalika.

Swali ibuka ni je, watu wanaompinga rais Magufuli sasa hivi, pia wangempinga Lowassa kama angekuwa ndo yeye anayafanya hayo anayoyafanya Magufuli?

Au wangemmiminia sifa kemkem na kusema kwamba acha awanyooshe maana walikuwa wamezoea?
Hivi jipu la LUGUMI kalitumbua? Bandari hatuishi kwenda kwa mikwara lakini "MASHETANI" bado Makontena yanawekwa kwenye mifuko ya suruali inasepeshwa
IPTL, ESCROW ACCOUNT kila siku "Wanjanja " wana draw kila uchwao pesa za MALOFA Kweli kwa madhaifu haya unataka "TUMUOMBEE"?
 
Ki-nadharia tete, mkuu Nyani Ngabu ingekuwa leo ni tar 31 Disemba 2016 usiku saa sita kasoro dakika chache, ningekuambia hii thread yako ni ya kufungia mwaka kwa ubovu. Sijawahi kuona unaandika thread ya ajabu kama hii. Hata Lowasa angekuwa rais hakuna mwenye uhakikia angefanya nini, kwani hata JPM hakuna aliyejua kama angefanya haya.anayofanya. Nimeandika ki-nadharia tete si unajua tarehe 31 Disemba bado!?
 
Mbona husemi kama

Asingefanya maongezeko ya mishahara kwa watumishi mikataba inavyotka,kudidimiza demokrasia,
Bunge kutooneshwa live..
Uhakiki kila wa mwezi.
Kutoonesha wapi nchi inaenda..tupo na jongoo style
 
Back
Top Bottom