Angekuwa ndiyo Lowassa...

Angekuwa ndiyo Lowassa...

Lowasa angekua rais ekimu ingekua bure mpk chuo kikuu,haya malakamiko ya watu kukosa mikopo eti kubana matumizi yasingekuwepo,ajira kwa vijana angelivalia njuga swala hili,sio huyu sera yake ni kutumbua hakuna analofanya ni kuongea sana na kufoko foka tu!..mzee lowasa ana hekima na busara
 
Lowasa angetendaje kama Magufuli? Yaan mwanasanaa atende kama mhandisi,swali la ajabu kabisa vile tu umesema mwenyewe unafikiri kinadharia basi sawa!


😳😳😳
Nyani Ngabu Kuna tofauti kubwa sana kati ya watu hao wawili.Mmoja ni Mwanasiasa na Mtafutaji vs Mwanasiasa kwa Bahati tu na Mtendaji. Sasa tusije Kariri kanuni isiyosahihi kwenye Mikwamo yetu ya Kimaendeleo.

Umesikia wapi watu wanamlaumu kwa mengi aliyokwisha ya fanya zaidi ya lawama kwenye issue ya uhuru wa shughuliza za kisiasa.
 
Mkuu Nyani Ngabu, wala usipate shida kupata jibu la swali lako? Je Lowasa alipokuwa CCM si walimtangaza kwenye Majukwaa kuwa ni Fisadi? Hawakufanya hivyo? Muulize John Mnyika, Saed Kubenea, Peter Msigwa, Godbless Lema, Tundu Lissu nk.

Je baada ya kuhamia CHADEMA wameendelea kuimba wimbo wa ufisadi? Thubutu! Nadhani mpaka hapo umeshapata jibu la swali lako. Hawa ndio upinzani
 
Mkuu Nyani Ngabu, wala usipate shida kupata jibu la swali lako? Je Lowasa alipokuwa CCM si walimtangaza kwenye Majukwaa kuwa ni Fisadi? Hawakufanya hivyo? Muulize John Mnyika, Saed Kubenea, Peter Msigwa, Godbless Lema, Tundu Lissu nk.

Je baada ya kuhamia CHADEMA wameendelea kuimba wimbo wa ufisadi? Thubutu! Nadhani mpaka hapo umeshapata jibu la swali lako. Hawa ndio Nyumbu

Aliesema atawapa mikopo wanafunzi wote watakao ingia Chuo kikuu imekuaje?
 
Lowasa angekuwa rais angekuwa na mfumo wake. Sera zake zilikuwa zipo ndani ya mpangilio na utaratibu mfano alikuwa na sera nzuri sana kwenye elimu walimu, elimu bure na wanafunzi wa chuo wasingelalamika na kutaabika mikopo.
 
Uko wapi unafiki wangu?
Binafsi nadhani ana nia nzuri.

Lakini sidhani anajua anakoelekea.....

Yupo yupo tu.

Signature
Miafrika Ndivyo Tulivyo.

My love is bank alert!


Huo hapo juu ndio unafiki wako....hiyo ni comment yako katika moja ya posts in May. Kweli "miafrika ndivyo tulivyo"!Typical mitanzania!
 
Kwakua kazi ya chama cha siasa ni kushikilia dola kama ingekua kama nadharia yetu inavyosema sasa hivi CCM ndiyo ingekua inaonesha mbadala bora wa mambo ambayo yanafanywa na aliyeko madarakani na ubovu wake, yaani wangekua ni watchdog wa Edward Lowasa na utawala wake.

Kuna watu hawapo chama chochote, wangeongea, kuna watu wapo ndani ya chama lakini siyo wanafiki, wangeongea na media zipo zingeongea pia.

Sioni kama kungekua na tofauti yoyote.
 
Lowasa angetendaje kama Magufuli? Yaan mwanasanaa atende kama mhandisi,swali la ajabu kabisa vile tu umesema mwenyewe unafikiri kinadharia basi sawa!
Wapi uhandisi ulipoonekana? Kwa wanafunzi kuitwa vilaza na wengine kukosa mikopo? Kwa mahosipitali kukosa dawa? Plz be realistic & objective stop being so much in love with your Party.
 
Hii thread yako inaonyesha haujui halli halis unaleta mzaha..
Rudi kwenye threads za us election..
 
Humu zingejaa thread za kusifiana tu! Mpaka ingetia kichefuchefu!
 
Kinyume chake ni sahihi, hakuna binadamu asiye na mpinzani! !labda swali lingekuwa hayo anayofanya ya impact kiasi gani kwa watanzania tulio wengi?
 
Kweli hii ni nadharia unataka kusema inawezekana Mwanasiasa na kiongozi(leader) lowasa akafanya kama Mkemia na meneja Magufuli kweli?.

Hivi Lowasa alipokuwa Waziri mkuu uliona akitenda kama Magufuli?

Asingeweza kutenda kama Magufuli yeye angetenda kwa namna yake kwanza hata ilani zao na namna ya utekelezaji ni tofauti!

Wanampenda Lowasa wanampenda jinsi anavyofanya mambo yake angefanya kama magufuli angekuwa si yeye tena
 
Wanaomshangilia Magufuli wangempinga Lowasa, simple.
Wanadamu huwa na sababu zao.
 
Angepingwa panapostahili kupingwa, angekosolewa panapostahili kukosolewa, angepongezwa anapostahili kupongezwa. Ila kwa hulka yake asingewaona ni maadui wale wanaompinga na kumkosoa sana sana angezifanyia kazi zile changa moto ili awape wananchi wake utumishi uliotukuka.
 
Kwa hiyo kumbe ingekuwa ni politics as usual!

Ngabu, sio kuwa Magufuli ayafanyayo yote hayafai hapana. Mengi anayofanya ni mazuri ila namna anavyofanya sio sahihi hivyo kama hata Lowasa naye angefanya kwa style hii anayotumia Magufuli wapo waliokuwa wanamuunga mkono wangempinga.
Kwa taarifa yako huku Tanzania mitaani na maofisini wapo waliokuwa wanamuunga mkono Magufuli wakati wa kuwania nafasi hiyo sasa wanampinga kutokana na namna anavyo yapeleka hayo mambo mazuri kwa njia mbaya.
Usihadaike na misimamo ya watu isiyobadilika hapa JF kwani wengine wako kazini hivyo wanatetea bila kuchoka kwa kutimiza wajibu wao na kulinda maslahi yasipotee ila moyoni wako vingine.
 
Back
Top Bottom