Angekuwa ndiyo Lowassa...

Angekuwa ndiyo Lowassa...

Mkuu hiyo ingekuwa vise versa .

Namaanisha wale wanaomsifia Mtukufu wa sasa wangekuwa ndio wakosoaji wakubwa kwa Raisi wa mioyo ya watu. Na wale wanaompinga Mtukufu kwa sasa ndio wangekuwa wasifiaji wakubwa kwa Raisi wa nyoyo za watu.
 
Mkuu hiyo ingekuwa vise versa .

Namaanisha wale wanaomsifia Mtukufu wa sasa wangekuwa ndio wakosoaji wakubwa kwa Raisi wa mioyo ya watu. Na wale wanaompinga Mtukufu kwa sasa ndio wangekuwa wasifiaji wakubwa kwa Raisi wa nyoyo za watu.

Kwa hiyo kumbe ingekuwa ni politics as usual!
 
Aaah wapi? Lowassa angesifiwa sana...kwani wangesema ndio mabadiliko,sababu ukawa walisema kuwa inatakiwa kila kitu kibadlishwe tuanze moja. yaani watu wote teuzi zao zitenguliwe!...Lowassa huyu 'kamanda' 'raisi wa mioyo'..''anayesingiziwa ufisadi''...''mwenye maamuzi magumu''....''mwenye busara''.....
 
Kama yepi kwa mfano?

Nadhani parameters zao kisiasa haziwezi kulingana hata siku moja. JPM anayafanya hayo kwa kuwa yuko CCM na Lowassa hayuko tena huko. Nadhani yeye EL angeanza na aidha visasi (huu ndio woga wa wana CCM wengi) au angeamua kuwathibitishia doubters wake kuwa wako wrong kwa kujaribu kufanya yale aliyotaka kuyafanya na JK.Tatizo la wote waili ni watu wanaowazunguka kama peers na advisors.
 
kuna binti namfahamu, alijifungua miezi miwili iliyopita kwenye hospitali ya chama ( sory ni ya serikali) akaambiwa chanjo hakuna arudi baada ya wiki, aliporudi akaambiwa chanjo bado hazijaja aache mawasiliano zikija ataaitwa, wiki haijaisha tukazika mtoto.
 
Ungeuliza hilo swali miezi ya mwanzoni ya utawala wa bosi wako kipindi anaanza kung'aa ningekujibu vizuri sana but its too late kuanza kufukia makaburi ambayo wafu wao washakuwa majivu..jikite kwenye mada endelevu kwa taifa na sio mambo yasiyo na tija kama haya kwani ni sawa na kuuliza nyerere angeamka leo angemfikiriaje bosi wako something wich is impractical and insane. Narudia tena,kuna changamoto lukuki za kuongelea ambazo zinawakabili watanzania almost wote regardless ya itikadi na vyama.watu kama hao hawahitaji mifano mfu kama hii bali wanahitaji solutions to their problem...try to be critical comrade.
 
Lowasa alishaga lalamika kuwa wafanya biashara wake wanaonewa hapendi walipe kodi kwanini serikali ya awamu ya 5 inawaonea sana awajazoea shida hiyo, na viongozi wa chadema walisha tuonya mapema kumpa Lowasa nchi ni hatari sana.(Tundu Lisu)
 
Angekuwa lowassa sidhani kama wanafunzi wa chuo kikuu wangekuwa wanateseka hivi! huyu msema ukweli aliapa mbele ya halaiki kuwa wanafunzi wa elimu ya juu hawatapata tabu! Sidhani kama hayo anaweza yarudia leo
 
Kwa hiyo kumbe ingekuwa ni politics as usual!
Ndivyo hivyo mkuu...
Wakosoaji wa serikali tawala hawakoseakani popote pale katika dunia hii. Hata zile nchi za kidikteta wanakosoana kama sio wale wa ndani ya nchi watakosolewa na mataifa jirani tu.
 
Lowasa alishaga lalamika kuwa wafanya biashara wake wanaonewa hapendi walipe kodi kwanini serikali ya awamu ya 5 inawaonea sana awajazoea shida hiyo, na viongozi wa chadema walisha tuonya mapema kumpa Lowasa nchi ni hatari sana.(Tundu Lisu)


Aliyasema haya wapi?
 
anacho miss magu ni sapoti ya watanzania wengi.

angekuwa na sapoti angefanya mengi, kwa sasa ataishia kugombana na upinzni.

huwezi fanikiwa kama huungwi mkono kwa ulifanyaro
 
Lowassa hana mizuka wala mihemko hyo' Mzee ana hekma yule mambo yangekua murua"
Elimu kwanza
 
Sabalkheri wanaJF na Alhamisi njema kwenu nyote na popote pale mlipo pembe ya dunia hii.

Sasa leo hebu tulonge kidogo ki-nadharia tete. Nimekaa kwa muda mrefu sana sasa nikijiuliza juu ya swali hili bila kupata jibu la uhakika.

Tuseme ingetokea mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA ndo angeibuka mshindi wa kinyang'anyiro cha urais mwaka jana.

Halafu baada ya kuanza kazi akafanya mengi kama aliyoyafanya rais wetu wa sasa MTUKUFU Dkt. John Pombe Joseph Magufuli...

Yaani akapiga marufuku safari za hovyo hovyo za nje ya nchi, akaagiza baadhi ya sikukuu za kitaifa tubadili namna tunavyozisherehekea kitaifa, akawa ni mtu wa kukaa nchini muda mwingi na kutuma wawakilishi pale inapobidi, akatumbua majipu hadharani na faraghani, akanunua ndege mpya kwa lengo la kufufua shirika letu la ndege, na kadhalika na kadhalika.

Swali ibuka ni je, watu wanaompinga rais Magufuli sasa hivi, pia wangempinga Lowassa kama angekuwa ndo yeye anayafanya hayo anayoyafanya Magufuli?

Au wangemmiminia sifa kemkem na kusema kwamba acha awanyooshe maana walikuwa wamezoea?

Naunga mkono hja,cna chama
 
Sabalkheri wanaJF na Alhamisi njema kwenu nyote na popote pale mlipo pembe ya dunia hii.

Sasa leo hebu tulonge kidogo ki-nadharia tete. Nimekaa kwa muda mrefu sana sasa nikijiuliza juu ya swali hili bila kupata jibu la uhakika.

Tuseme ingetokea mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA ndo angeibuka mshindi wa kinyang'anyiro cha urais mwaka jana.

Halafu baada ya kuanza kazi akafanya mengi kama aliyoyafanya rais wetu wa sasa MTUKUFU Dkt. John Pombe Joseph Magufuli...

Yaani akapiga marufuku safari za hovyo hovyo za nje ya nchi, akaagiza baadhi ya sikukuu za kitaifa tubadili namna tunavyozisherehekea kitaifa, akawa ni mtu wa kukaa nchini muda mwingi na kutuma wawakilishi pale inapobidi, akatumbua majipu hadharani na faraghani, akanunua ndege mpya kwa lengo la kufufua shirika letu la ndege, na kadhalika na kadhalika.

Swali ibuka ni je, watu wanaompinga rais Magufuli sasa hivi, pia wangempinga Lowassa kama angekuwa ndo yeye anayafanya hayo anayoyafanya Magufuli?

Au wangemmiminia sifa kemkem na kusema kwamba acha awanyooshe maana walikuwa wamezoea?
Lowassa asingeweza kufanya mambo kama haya ya sasa
 
Back
Top Bottom