Angalia Haki ya Mtumia Umeme Ghana

Mtoboasiri

JF-Expert Member
Aug 6, 2009
5,101
1,946
Wana JF - especially wana MAGAMBA,

Wakati mgao wa umeme umeeanza nchini kwetu (na imekuwa jambo la kawaida si geni tena) Ghana kuna sheria zifuatazo zinazomlinda mteja wa umeme:


  • Umeme hautakiwi kukatika zaidi ya saa 48 (kwa mwaka) kwa miji mikubwa na 72 kwa miji midogo (kwa mwaka).
  • Ukikatika umeme kwa siku isizidi saa 8 mfululizo, na hiyo isizidi siku 7 katika mwaka.
  • Ikiwa kuna hitilafu inayosababisha kukatika umeme sheria hizo hazitatumika ISIPOKUWA ikitokea hitilafu ikakiuka sheria KAMPUNI YA UMEME INALIPA FAINI.
Hawa ni waafrika wenzetu, MAGAMBA mnasemaje juu ya hili?
 
kaka miaka hamsa eti ya uhuru(km kweli upo) hata nusu ya hapo hatujafika na chini ya akina kagasheki hatufiki kokote!
 
siwezi kuielewa hii serikali iliyopo madarakani Tz
umeme nusu mwaka sasa gizani??kweli?
na ivi vipindi vya tv na wakurugenzi sijui wa tanesco..shida tupu

na presidaa wala mshipa haumshtuki
 
Hata mimi nimeshangaa sana,kumbe somewhere under the son here in Africa(i mean african country),wanaweza kufanya mambo ambayo nchi yetu wanasingizia umaskini na uafrica wetu kwamba eti haiwezekani,.....nimefunguka macho sana na habari hiyo ya bbc jana,...sasa nafikiria nini ntafanya ili kukabiliana na uzembe huu wa viongozi wetu.
 
msilalamike huku mmelala!!

Tanzania imelazwa, watanzania tumelazwaaaaaaa pia!!
 
Kupanga ni kuchagua..

Tumeshindwa kuyapa kipaumbele mambo ya muhimu..Kuanzia 1992 tunahangaika na tatizo hili
 
Kama ni kweli wenzetu wamepiga hatua kubwa kueka mazingira yanayotabirika ktk sekta hiyo muhimu. Sisi hku tunazidi kwenda backwards na hatuna baseline wala dira yeyote kwene kutatua tatizo lolote.
 
Dah hizo sheria zikiletwa hapa tz ndani ya mwaka tanesco watakuwa wamefilisika kabisa
 
Wenzetu hizo sheria walizitafuta..sisi tumezubaa! jamani haya mambo wanachi wenyewe ndio wanayatafuta, jaribu kuangalia historia ya maisha yao..halafu angalia na bongo sisi vijana tunaishia kuimba nyimbo za halaiki tu juani...! Yethu wangu
 
ishu si CCM...ishu ni THE LAW IS BLIND....LAW MAKERS ARE BLIND....LAWYERS ARE BLIND...!
LAWYERS INCLUDE.....MARANDO,LISU,MWAKYEMBE,MKONO,SITTA .....THE SO CALLED LEARNED BROTHERS .....! ARE THEIR LEARNED BROTHERS OUT HERE?
 
Watanzania tu wakarimu sana. Mtu anakuingiza kidole machoni, hata kabla hajaomba msahamaha tumeshamsamehe 7x70.
Jamani, TANESCO kuwasha umeme imekuwa kama ni upendeleo.
Sijui tunasubiri masihi aje kutukomboa tena?
Hatuwachagui, wanashinda, hatuwapigii kura, wanapata asilimia sabini!
Jiulize na ujijibu!
 
Lishirika likubwa ukiritimba uliokithiri rushwa isiyomithilika lakini huduma ziro. Pamoja na ukubwa wote na huduma hafifu nchi nzima inapata umeme usiozidi asilimia kumi na saba kwa maana nyingine Tanzania iko gizani. Hapo ndipo najiuliza ghilba za Idrisa Rashid wakati ule aliposema tusiponunua mitambo ya Dowans baada ya muda kitambo taifa litakuwa gizani wakati ukweli ni kwamba tuko gizani! Na kwa mtaji huu tutakuwa gizani milele and the blessed few who are now enjoying the poor services rendered by Tanesco will continue paying through their nose indefinately. Mungu ibariki Tanzania Musa anahitajika kutukomboa waja wako
 
Wana JF - especially wana MAGAMBA,&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Wakati mgao wa umeme umeeanza nchini kwetu (na imekuwa jambo la kawaida si geni tena) Ghana kuna sheria zifuatazo zinazomlinda mteja wa umeme:&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
&lt;ul&gt;&lt;li&gt;Umeme hautakiwi kukatika zaidi ya saa 48 (kwa mwaka) kwa miji mikubwa na 72 kwa miji midogo (kwa mwaka).&lt;/li&gt;&lt;li&gt;Ukikatika umeme kwa siku isizidi saa 8 mfululizo, na hiyo isizidi siku 7 katika mwaka.&lt;/li&gt;&lt;li&gt;Ikiwa kuna hitilafu inayosababisha kukatika umeme sheria hizo hazitatumika ISIPOKUWA ikitokea hitilafu ikakiuka sheria KAMPUNI YA UMEME INALIPA FAINI.&lt;/li&gt;&lt;/ul&gt;Hawa ni waafrika wenzetu, MAGAMBA mnasemaje juu ya hili?
<br />
watu kwa kusifia bwana. Hivi ukisoma hiyo sheria mbona loopholes kibao? Nini hitilafu? Yaani unaweza kucheza na masaa na fidia hailipwi. Afrika ni moja ndugu zangu msijidanganye.
 
<br />
watu kwa kusifia bwana. Hivi ukisoma hiyo sheria mbona loopholes kibao? Nini hitilafu? Yaani unaweza kucheza na masaa na fidia hailipwi. Afrika ni moja ndugu zangu msijidanganye.

Wale wale! Inawezekana wewe mwenzetu "sweeping statement" zimekuingia kweli kweli kiasi kwamba unadhani hakuwezi kuwa na mabadiliko. Tafakari yafuatayo:

  • Alikwambia nani ulichokisoma ndio sheria yenyewe - kwa maana ya kuwa nilichokiandika hapa kiko "detailed" -and I am not a lawyer?
  • Umedanganywa na kuamini kuwa usanii unaofanywa hapa kwetu ndio unaofanywa nchi nyingine Afrika (rejea kauli yako:..Afrika ni moja..."). Kama Afrika ni moja (which means we are and behave the same) iweje kukawa na nchi zilizopiga hatua na sisi tunarudi nyuma? Au kwako kila nchi ya Afrika leo hii ina mgao wa umeme? Kwa taarifa yako kuna nchi Afrika hii hii watu hawajui kukatika umeme maana yake nini!
Jiamini ndugu yangu, kuwa Afrika haina maana hakuwezi kuwa na maendeleo au kuwa na sheria bora NA ZINAZOFUATWA kumlinda mwananchi wa kawaida. Fanya homework hii ndogo: Tafuta katiba mpya ya Kenya uone inasemaje kuhusu haki ya mwananchi kupata huduma za kijamii na kinga ya mtu mlevi (kwa maana ya alcoholic).

IT CAN BE DONE, PLAY YOUR PART.
 
bongo pazuri sana, asubuhi watu tunakunywa bia, mchana watu tunakula lunch na jioni watu tupo nyumba za kupumzikia wageni....hii ndo bongo! kila mtu analalamika hadi mkuu wa kaya!
 
Umeme kupatikana bila matatizo ni anasa au ni kosa lisilosameheka.
Eti nchi imepiga hatua kiuchumi! wakati umeme wenyewe longolongo tupu.
 
Wale wale! Inawezekana wewe mwenzetu "sweeping statement" zimekuingia kweli kweli kiasi kwamba unadhani hakuwezi kuwa na mabadiliko. Tafakari yafuatayo:

  • Alikwambia nani ulichokisoma ndio sheria yenyewe - kwa maana ya kuwa nilichokiandika hapa kiko "detailed" -and I am not a lawyer?
  • Umedanganywa na kuamini kuwa usanii unaofanywa hapa kwetu ndio unaofanywa nchi nyingine Afrika (rejea kauli yako:..Afrika ni moja..."). Kama Afrika ni moja (which means we are and behave the same) iweje kukawa na nchi zilizopiga hatua na sisi tunarudi nyuma? Au kwako kila nchi ya Afrika leo hii ina mgao wa umeme? Kwa taarifa yako kuna nchi Afrika hii hii watu hawajui kukatika umeme maana yake nini!
Jiamini ndugu yangu, kuwa Afrika haina maana hakuwezi kuwa na maendeleo au kuwa na sheria bora NA ZINAZOFUATWA kumlinda mwananchi wa kawaida. Fanya homework hii ndogo: Tafuta katiba mpya ya Kenya uone inasemaje kuhusu haki ya mwananchi kupata huduma za kijamii na kinga ya mtu mlevi (kwa maana ya alcoholic).

IT CAN BE DONE, PLAY YOUR PART.
Sasa ukitaja proffessional yako ndio unataka uachwe tu! Ulete vitu vina hang hapa halafu vipite salama kwa sababu wewe umesema? Unajua proffessional ya kila mtu? Hebu tafuta Index zote unazozifaham kuanzia ile ya Transparency, MO, Human Rights etc halafu njoo useme hayo maneno yako. Huko Ghana asilimia ngapi wanapata umeme? Institution quality in terms of governance zikoje? South Africa yenyewe inayosemekana better kuna madudu kibao. Narudia tena na tena kila sehem ina sweeping statements na kwa Africa tunayo na ndio hiyo, Afrika yote ni sawa.
 
Back
Top Bottom