Hivi mtoto wa shangazi yako akikulia ndani ya nyumba ya mjomba wake ambae ni baba yako mkiwa ndani wote uwa mnaitwa kwa jina gani vile...''watoto'' basi kama ndio jina hilo si ajabu mwalimu kuwa na watoto pia wa ndugu na jamaa waliokulia mikononi mwake...manake hata mashemeji na wadogo zetu upitia mikononi mwetu mpaka kufika utu uzima.Ukizingatia mfumo wa utamaduni ambao Mwalimu aliusimamia na nina hakika pia aliushi kwa vitendo kwa jina la ujamaa wa Kiafrika.Yani mpango mzima nyumbani kuona mtoto wa Shangazi, Mjomba, Mdogo wake Baba, Dada yake Baba, mtoto wa rafiki yake Babu na wengineo wengi tu kama sehemu moja ya kifamilia.
Tukisema watoto wa Mwalimu tunamaanisha watoto wake Mwalimu Nyerere na Maria Nyerere...