WanaJf,
NI vizuri tukawafahamu watoto wote wa Mwalimu Nyerere, wako wapi, wanafanya nini na wanaishije. Ninatuma ombi hili maalumu ili tuweze kuwajua hawa watu kwa sababu ndiyo familia ya pekee ndani ya nchi yetu inayoheshimika zaidi kutokana na kazi za baba yao.
Mimi kwa kweli siwajui ila kidogo sana namfahamu Makongoro wakati akiwa Mbunge wetu hapa Arusha na kipindi hicho nilikuwa bado mdogo.
Nina hamu sana sana ya kuwajua hawa watu wanafanya nini na ni kwa nini hawajihusishi na siasa na kutafuta vyeo, na nataka kujua shule walizosoma. Je, walisoma International school? Halafu napenda kujua kama walipelekwa ng'ambo kusoma na elimu zao zikoje.
Tupende tusipende familia ya Mwalimu Nyerere mdiyo familia Humble na ya kuheshimika kuliko familia yoyote hapa Tanzania.