Andrew Nyerere on Mwalimu humble children!

Andrew Nyerere on Mwalimu humble children!

Wako wapi na wanafanya kazi gani?

Huyu kwanini kafaia muhimbili.na sio INDIA au paris?

Nnajuwa mmoja ni mbunge wa bunge la Afrika Mashariki.

Hilo la kifo naomba tumwachie Mwenyeezi Mungu.
 
Hawa ni wale nilipokuwa Nakua niliwaona, angalia kwenye picha kuna namba japo hazijakaa swadakta.
1.Makongoro.
2.Leticia
3.Rose.



huyo kwenye wekundu ni mke wa Madaraka sio mtoto wa kuzaa.
 
Kama wenyewe "hawajajiuza" mpaka sasa maana yake hawapendi. , .

Waheshimiwe kwa hilo.
 
Kupitia Picha hii Manyerere Jackton na Endrew Nyerere mnaweza kututajia nani ni nani katika umoja wenu huu..
View attachment 250690

Waliosimama kutoka kushoto:
Anna Watiku, Andrew, Merciana (ndugu ya Maria ) na John (kati kati ya Nyerere & Maria ).

Waliokaa chini kutoka kulia:
Charles Makongoro, Rosemary, Emil Magige na Kwame (mtoto wa Joseph Nyerere ).
 
DSN na wadau wote, nashukuru kubaini kuwa mna kiu ya kuifahamu familia ya mwalimu. Mimi si msemaji wa ukoo lakini kwa heshima ya John Guido Nyerere nitaandika wasifu wa namna nilivyomfamu. Vuteni subira.
 
  • Thanks
Reactions: DSN
DSN na wadau wote, nashukuru kubaini kuwa mna kiu ya kuifahamu familia ya mwalimu. Mimi si msemaji wa ukoo lakini kwa heshima ya John Guido Nyerere nitaandika wasifu wa namna nilivyomfamu. Vuteni subira.
Sawa MJ !!
Ndio tunatambua yupo msemaji wa familia kama kiongozi wenu...lakini na nyie kama familia mfike sehemu jamani muwe flexible..msiwe wapole kupitia kipimo bhana, upole ukizidi ni dhambi..yani Comrade mzima anafariki ishie kusemwa Mtoto wa Mwalimu Kafa na kijipicha kwenye magazeti yetu kwishiney.

Hatujui alifanya nini kama Mtanzania wa Kawaida hata kama hakuwa mbele ya maruninga yetu ...manake pia sio wakaa backbench wote ni mbumbu, wengine ni HESHIMA wapewe tuwaite waje kukaa mbele.Ungwana ni vitendo familia ile HAIKUISHI kwa kutangaza UKUU wa Baba.Lakini pale ambapo tuna jamii sasa imepevuka na kuna mambo tunasema tunamuenzi Mwalimu Nyerere tufike sehemu pia Wananchi wajifunze kitu kupitia Mwalimu kuwa NAE alikuwa na watoto lakini watoto wake hao waliishi maisha ya kawaida kama Watanzania wengine, walisoma shue za kawaid za serikali [Goverment schools], walikula dona na maarage kama watoto wengine wa Taifa hili.

Kupitia picha kama hizo jamii inajiona na kupima malezi ya familia za sasa za viongozi wetu d=zidi ya zile za zamani. Ndio kweli kuna mabadiliko hayaepukiki ni lazima kuishi kulingana na ulimwengu wa sasa kama nyakati.Lakini kwa kuishi uko kulingana na ulimwengu huo mpya si fursapia ya kuwafanya Watoto wa Viongozi wetu wawe na tofauti kubwa sana ya kimalezi katika misingi ya Elimu, Afya, Utamaduni na hata kimaendeleo kulinganisha na watoto wa malika yao ya Watanzania wengine.Ni nani asie jua kuwa ukiingia kwenye takwimu ukatafuta majina ya watoto wa viongozi wanaosoma Shule za Saint Kayumba kama utakutana nayo ..mmmh thubutu, kwanini?...

Je kiongozi huyo kama hana Mwana anaesoma Saint Kayumba do you think akili yake itakumbuka kuboresha maendeleo ya Shule zile katika uhalisia.Hakika No Thank!!!aiwezi kwa sababu anapo pewa taarifa au record za masomo na matokeo ya Mwanae ni ya mtaala wa kiingereza ambao ni opposite na Kayumba...Wakati mwingine we live with it na kwa kuwa HATUONI we loose Conciousness kuona UHALISIA kwa kuwa kwa hulka iliyomzunguka kiongozi anae ISHI na Watoto wake wakisoma International hawezi narudia tena hawezi kuona REALITY ya maisha ya mtoto anae soma SAINT KAYUMBA kwa kuwa challenge zinazomzunguka mtoto yule hazimgusi kiongozi husika kwa kuwa its not part of his life no more zaidi ya kuzikuta katika documents za Serikali anapodeal na matatizo hayo.

Mwalimu alisomesha watoto wake Shule za kawaida malalamiko yakirudi nyumbani iwe rikizo time, au siku za kawaida yakiingia ndanii ya KUTA za IKULU kuhusu watoto wa Rais ilikuwa ni sawa na matatiizo yoyote yale ya mtoto wa Shule yoyote Tanzania kapeleka matatizo yake nyumbani kwao Ibinzamata Shinyanga, Kanyigo Bukoba, Kigera-Musoma, Mfaranyaki-Songea, Kwa Mromboo-Arusha, Kibororoni-Moshi, Mwandiga-Kigoma, Cheyo-Tabora na sehemu mablimbali Tanzania nzima.

Ni funzo lisilo ingia akilini kwa haraka katika maisha yetu, lakini ni funzo ambalo kwa mtu kwenye hofu ya Mungu, Hofu ya Nyakati na Mabadiliko ni somo jepesi na la maana sana kwa kuwa Mungu alivyotuumba HATUIJUI KESHO ITAKUWAJE.Leo hii kwa mtoto wa Mobutu kwenda kuomba kugombea siasa za Kongo ni kazi sana...kwa sababu legacy ya Baba yao kwenye Taifa hilo haikushabiana na maisha ya Wanakongo.Sadam kaenda na wanae, Watoto wa Gadafi ni kama Wakaimbizi pamoja na madola yote yale.Mubarak anapumulia mashine maisha ya wanae hayatambuliki yako vipi.

Sasa kwa kuwa watoto wa Mwalimu ni jamii [Na ni familia Namba Moja ] ni vyema ukafanya utaratibu wa kutumegea kidogo ili kuonysha unyofu wa maisha ya Mtoto wa Mtu ambae angeweza kuwa Mkwasi Namba moja East Afrika lakini kwa uishi kawaida kawalea Watoto pia kuishi kawaida na kutafuta kwa jasho lao.Kwa watoto wenye busara kutoka kwa baadhi ya viongozi aka vigogo wetu ata kama Baba yake ni kiongozi mwenye UKWASI USIO NA HESABU mtoto wa Mkwasi anaweza kuamua KUFUATA njia YAKE na kuamua HATIMA ya Maisha yake katika FAIR WAY na sio njia ya Kikwasi.Kwa kuwa mwisho wa siku Mungu pia alitupatia UTASHI wa kuamua our DESTINY katika kuamua WHAT IS WRONG AND WHAT IS RIGHT.
Aksante kwa kuliona ilo.
 
Hawa ni wale nilipokuwa Nakua niliwaona, angalia kwenye picha kuna namba japo hazijakaa swadakta.
1.Makongoro.
2.Leticia
3.Rose.
Sidhani kama Leticia ni mtoto wa Nyerere bali ni mkwe ,aliolewa na mtoto wa Nyerere,si ndio huyu wa Chadema anaishi Marekani?
 
Soma comment ya hapo juu kabla ya hiyo yakwako.
Sidhani kama Leticia ni mtoto wa Nyerere bali ni mkwe ,aliolewa na mtoto wa Nyerere,si ndio huyu wa Chadema anaishi Marekani?
 
Mmoja ndo katutoka jana. John Guido Nyerere alikuww mtoto wa nne kwa mwalimu nyererr na mwalimu maria. Alikuwa fighter pilot. Tutamzika butiama jumatano mei 13. Tayari tumeshawasili butiama kumsindikiza kamanda john.

John alikuwa mcheza karate na mpiga gitaa. Alikuwa na wimbo wake maarufu wa 'amina dole tupu'

Pole sana mkuu kwa kuondokewa na brother john! Mungu ailaze roho yake mahala pema pepon! Amin
 
ebaeban
wewe ebaeban mbona huna adabu hata ya kuvalia nguo yako.unasubutu kweli kumtukana mwanamke hivyo.kweli. huna mzazi wa kike wewe au ndugu au jamaa wa kike au mke katika ukoo wenu.huoni hata vibaya kuja katika mtandao na kutukana hivi.kweli asiye leleka utamjua tu.na mkuu wa hii blog una wacha posti hii ya kutukanwa ipite tuu.kwa nini?hasara yako we ebaeban.ningemjibia tusi hili ulilo mtukana faizafoxy nadhani ninge pigwa ban leo hii.na wala sijali but najisheshimu sana kwa vile nimeleleka nikaleleka kwetu.sijibishani na watu mitandaoni wasio na malezi mema.
 
Last edited by a moderator:
Marehemu john alikuwa rubani wa jwtz na hata vitani uganda alikwenda,kwahiyo yeye binafsi anamchango mkubwa sana Tanzania
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom