Andrew Nyerere awatemea cheche TISS

Andrew Nyerere awatemea cheche TISS

Huyu Mzee Julius Kwanini aliiacha familia Ikiwa na hali mbaya kiasi hiki? Hivi kweli alishindwa kuwawekea vitega uchumi vya kudumu licha ya kutawala nchi kwa zaidi ya miaka 20?

Alishindwa hata kuwaandaa Walau waweze kujitegemea?

Mpaka Sasa Nafikiri wanaishi kwa kutegemea posho Toka serikalini!

This is shame kwakweli!
Waasisi huwa wanakuwa katika wakati mgumu sana kuhusu mali za taifa, nahisi Mwalimu alifkiria akiwawekea wanae vitega uchumi ataweka nadharia mbaya kwa wanaomfuata. Kiuhalisia hilo ndilo kosa alofanya, waliofatia wote hawakuwa waaminifu kama yeye.
 
Hiyo tofauti yao ya maisha mazuri au mabaya inatokana na wazazi wao au watoto wenyewe na uzalendo au uzembe wa hao wazazi wao inategemea na mtazamo wako au wao, lakini sio sababu ya serikali.

Serikali kama serikali hakuna fungu maalumu la kuhudumia watoto wa raisi wastaafu.
Kuna fungu la raisi mstaafu labda na mkewe tu.
Sasa Mkuu unadhani hata Mkewe anapewa mahitaji yake ipasavyo?
 
Hawa watoto wa Nyerere waingizwe kwenye pay roll ya ikulu,wawe wanavuta mpunga kila mwezi hadi watakapo aga dunia.
Haipendezi wakae kwenye "extremly poverty" wakati baba yao alitumia mda mwingi kuikomboa Tanganyika,na kusahau familia yake.
Laiti Nyerere angekuwa na mentality ya ubinafsi,hao watoto leo ndio wangekuwa matajiri wa kutupwa,na watanganyika tungekuwa extremly poor
Mkuu kuna mambo yanaumiza sana, hivi akiwa kama Baba wa Taifa alishindwa kuwapa hawa wazungu madini na yeye akachukua asilimia zake ukitazama kipindi kile Watanzania ndo tuliwa wajinga zaidi, sio madini tu, hata wanyama na biasha zingine mbovu angeweza kufanya ili kujilimbikizia mali.Leo hii ona mke na watoto wanavyoishi. Huwezi fananisha familia ya Mwalimu na mtu kama Mkapa au Kikwete.
 
Nimeisoma tena na tena hii thread huku nikijiuliza huyu jamaa Andrew ni kweli hajui anachoandika? Ni kweli usalama wanamlinda yeye? Kama wamepewa kazi ya kumlinda yeye ni kwa umuhimu gani alionao(maana kazungumzia hao usalama ni kama kundi flani hivi). Na kwanini sasa baada ya kundi hilo kupewa kazi ya kumlinda Andrew huku wakilipwa mishahara minono sana wamemgeuka na sasa wanaanza kumtukana, tena yeye akiishi katika umasikini uliotopea?! Anataka kusema kitu gani hasa?

Baada kufikiria scenario nyingi za social economic zinazojiri katika jamii fulani ya nchi fulani nimegundua Andrew Nyerere kuna ujumbe ameutoa. Ujumbe wenye maana hasa, na kauficha katika fasihi yenye kuhitaji tafakuri.
Kwenye jamii hiyo anayoizungumzia kuna wanaolalamika ambao kwa sura ya nje wanaonekana kama wanathaminiwa na kulindwa vyema na watu wanaolipwa unono sana lakini kiuhalisia watu hao wamegeuka na wanawanyanyasa hao wanaombiwa wanapewa ulinzi, mpaka wanatamani wawatoe kwenye nafasi hizo ili wakafanye kazi zingene na badala yao waje wengine

Anyways labda ni fikra zangu tu lakini ndio kazi ya fasihi kila mtu aweza kufikiria kivyake
 
wengne mnalopol humu mtadhan mmewekewa cherehan midomon pasipo kutafakar.!ths family iko kwenye maisha ya shda sana,wakat baba yao ameplay part kubwa sana ktk hii nchi,utashangaa kina ridh na watoto wengne wa wakulu wanaish kama wafalme wakat watoto wa mwl kama watumwa!wat a shame
hao watoto wengine baba zao waliwandalia masha mazuri, kafanya hivyo Mwinyi, Mkapa na hata Kikwete, vijana wao maisha mazuri, sasa Mwalimu kama aliacha heshima tu akidhani ndio watoto watakula hiyo sawa aliamua yeye...
Btw, yeye nadhani anajifunikia mwamvuli wa mama pale maana TISS pale kazi ni kuhakikisha usalama wa mama Maria Nyerere sasa hao kina Andrew wapambane kimpango mwisho wa siku watadai na wajukuu zao serikali iwatambue
 
wengne mnalopol humu mtadhan mmewekewa cherehan midomon pasipo kutafakar.!ths family iko kwenye maisha ya shda sana,wakat baba yao ameplay part kubwa sana ktk hii nchi,utashangaa kina ridh na watoto wengne wa wakulu wanaish kama wafalme wakat watoto wa mwl kama watumwa!wat a shame
Hakuna kati hao uliowataja wanapata single cent toka serikalini wamezipata kwa baba zao kama baba yao hakuwaandaaa sio kosa la serikali ni kosa lakifamilia
 
Huyu Mzee Julius Kwanini aliiacha familia Ikiwa na hali mbaya kiasi hiki? Hivi kweli alishindwa kuwawekea vitega uchumi vya kudumu licha ya kutawala nchi kwa zaidi ya miaka 20?

Alishindwa hata kuwaandaa Walau waweze kujitegemea?

Mpaka Sasa Nafikiri wanaishi kwa kutegemea posho Toka serikalini!

This is shame kwakweli!
Ulitaka awamegee kaeneo ndani ya Jamhuri mkuu
 
Anapotosha hakuna Usalama wa Taifa wanaomlinda yeye, wao wanamlinda mke wa Mwalimu(mama yake) Mama Maria pamoja na makazi yake ya Mikocheni na Butiama, yeye kajikuta yupo cordoned kwa virtual yakuishi ktk hayo makazi embu ahame aone kama kuna atakaemlinda...dogo anatafuta kiki tu
 
Hawa watoto wa Nyerere waingizwe kwenye pay roll ya ikulu,wawe wanavuta mpunga kila mwezi hadi watakapo aga dunia.
Haipendezi wakae kwenye "extremly poverty" wakati baba yao alitumia mda mwingi kuikomboa Tanganyika,na kusahau familia yake.
Laiti Nyerere angekuwa na mentality ya ubinafsi,hao watoto leo ndio wangekuwa matajiri wa kutupwa,na watanganyika tungekuwa extremly poor
Ukisema hao wa nyerere usisahau hakua mwenyewe utaibua watoto wa kina Kawawa na wazee wengine wao wapambane na hali zao
 
wengne mnalopol humu mtadhan mmewekewa cherehan midomon pasipo kutafakar.!ths family iko kwenye maisha ya shda sana,wakat baba yao ameplay part kubwa sana ktk hii nchi,utashangaa kina ridh na watoto wengne wa wakulu wanaish kama wafalme wakat watoto wa mwl kama watumwa!wat a shame
Shame kwa baba yao aliyewaandalia maisha ya kitumwa,unataka shame uende kwa nani labda
 
Back
Top Bottom