Kusali ni muhimu, lakini baadhi ya tabia na sheria za baadhi ya makanisa yanachangia sana kuvunja moyo watu kuabudu.
Naomba mwenye kujua kanisa lolote lenye sifa zifuatazo ili nijiunge;
Naomba mwenye kujua kanisa lolote lenye sifa zifuatazo ili nijiunge;
- Liwe ni kanisa la kikristu
- Liwe na mfumo wa kitaasisi (yaani management iwe kimfumo wa kitaasisi)
- Liwe linapatikana angalau kila wilaya/mkoa
- Misingi ya waumini wake iwe ni ile ya teamwork (umoja bila kubagua masikini au tajiri hususani wakati wa matatizo ya mmoja mmoja)
- Liwe ni kanisa lisilotegemea uwepo wa mchungaji/kiongozi mmoja
- Liwe ni kanisa lenye ratiba maalum ya kuzingatiwa (standards)
- Liwe ni kanisa linalojali malezi ya watoto kiroho
- Liwe ni kanisa la watu wenye akili timamu.
- Liwe ni kanisa lenye kupenda haki, usawa na uwazi
- Liwe ni kanisa linaloponya, kukuza na kujenga imani kwa waumini wachanga n.k