Nimesoma mahali andiko la Jasusi Chahali kuhusu Mbowe kuwa mahabusu kwa siku tisini.
Katika andiko lake hilo amesikitishwa na kitendo hicho lakini kama nimemsoma vizuri mwishowe amewaangushia jumba bovu Chadema.Amewalaumu Chadema kumkumbatia Kigogo wakati wakijua fika Kigogo alikuwa mwizi anayetafutwa.Pili ameonyesha kuwa Chadema kuwashabikia wanaharakati wanaondesha mijadala mingine kuhusu Katiba mpya,na kwa uelewa wangu ni kama anawasikitikia Chadema kuingizwa chaka tena!!
Yote aliyoyaandika yanaweza kuwa kweli lakini hebu tuchukue nafasi ya Chadema katika hayo yaliyozungumzwa na tuyatizame kwa jicho la tatu.Kama ilivyo kwa binadamu wote ni vigumu kujua anachowaza mtu na mara nyingi tunaaminiana au kutuhumiana bila hata ushahidi wa kina.Kwa Chama cha siasa kuweza kuwajua wabaya na wazuri ni kudra ya Mungu tu.Jambo hili linawafanya mara nyingi wawe suscipious ambayo inawasaidia kutokupanga jambo lolote ovu (Hamuaminiani).Hii ni safety mechanism ambayo kwa mtizamo wangu imewasaidia sana Chadema mpaka kufika hapa walipo leo.Wangepanga kitu chochote fishy si ajabu wangeshapotea wengi!!Lakini jambo hili athari ingine kubwa hasa ikiwa Chadema wataendelea kuonewa ni kusababisha watu kupanga mambo kama individual na madhara yake ni kutokea watu kama kina Hamza.
Tukija kwa wanaharakati hata mie binafsi siwaamini sana,kuna mmoja maarufu hajapata msukosuko hata mmoja pamoja na harakati zake,kuna mwenyekiti wa Chadema wa wilaya moja ambaye kwa maandishi yake ungetegemea apate msukosuko lakini wapi.
Utamwamini nani kwani hata Bwana Chahali,mkosoaji mkubwa wa serikali aliwahi kukiri kudhulumiwa pesa na Kinana (Je alimfanyia Kinana,(Katibu Mkuu wa CCM) kazi gani,ajuaye ni Mwenyezi Mungu.
Chadema imeondokewa na makatibu wakuu wawili (watendaji wakuu wa Chama na waendeshaji wa shughuli za kila siku za chama),hawa si watu wadogo.Ni kipi walikisema walipokwenda huko ni kipi walikitoa kwa hiari na ni kipi walilazimishwa au kulaghaiwa, hakuna ajuaye ila Mwenyezi Mungu na katika hatua hiyo HAKUNA WA KUMUAMINI ni kumuachia MUNGU TU!!
Katika andiko lake hilo amesikitishwa na kitendo hicho lakini kama nimemsoma vizuri mwishowe amewaangushia jumba bovu Chadema.Amewalaumu Chadema kumkumbatia Kigogo wakati wakijua fika Kigogo alikuwa mwizi anayetafutwa.Pili ameonyesha kuwa Chadema kuwashabikia wanaharakati wanaondesha mijadala mingine kuhusu Katiba mpya,na kwa uelewa wangu ni kama anawasikitikia Chadema kuingizwa chaka tena!!
Yote aliyoyaandika yanaweza kuwa kweli lakini hebu tuchukue nafasi ya Chadema katika hayo yaliyozungumzwa na tuyatizame kwa jicho la tatu.Kama ilivyo kwa binadamu wote ni vigumu kujua anachowaza mtu na mara nyingi tunaaminiana au kutuhumiana bila hata ushahidi wa kina.Kwa Chama cha siasa kuweza kuwajua wabaya na wazuri ni kudra ya Mungu tu.Jambo hili linawafanya mara nyingi wawe suscipious ambayo inawasaidia kutokupanga jambo lolote ovu (Hamuaminiani).Hii ni safety mechanism ambayo kwa mtizamo wangu imewasaidia sana Chadema mpaka kufika hapa walipo leo.Wangepanga kitu chochote fishy si ajabu wangeshapotea wengi!!Lakini jambo hili athari ingine kubwa hasa ikiwa Chadema wataendelea kuonewa ni kusababisha watu kupanga mambo kama individual na madhara yake ni kutokea watu kama kina Hamza.
Tukija kwa wanaharakati hata mie binafsi siwaamini sana,kuna mmoja maarufu hajapata msukosuko hata mmoja pamoja na harakati zake,kuna mwenyekiti wa Chadema wa wilaya moja ambaye kwa maandishi yake ungetegemea apate msukosuko lakini wapi.
Utamwamini nani kwani hata Bwana Chahali,mkosoaji mkubwa wa serikali aliwahi kukiri kudhulumiwa pesa na Kinana (Je alimfanyia Kinana,(Katibu Mkuu wa CCM) kazi gani,ajuaye ni Mwenyezi Mungu.
Chadema imeondokewa na makatibu wakuu wawili (watendaji wakuu wa Chama na waendeshaji wa shughuli za kila siku za chama),hawa si watu wadogo.Ni kipi walikisema walipokwenda huko ni kipi walikitoa kwa hiari na ni kipi walilazimishwa au kulaghaiwa, hakuna ajuaye ila Mwenyezi Mungu na katika hatua hiyo HAKUNA WA KUMUAMINI ni kumuachia MUNGU TU!!