Ngalikihinja
JF-Expert Member
- Sep 1, 2009
- 34,637
- 37,960
Umenishangaza sana ndugu. Nimejiuliza yafuatayo;Wakuu hamjambo....
Sasa Kuna jambo limetokea nyumbani kwangu ninaishi na mwanamke ambaye sijafunga naye ndoa lakini pia yupo Mdogo wake wa kike ambaye amekuja kujiendeleza mambo ya ushonaji.
Sasa ninapotoka asubuhi kwenda kazini Huwa ninatoka na Mdogo mtu ambaye Huwa anaelekea huko kwenye ushonaji maana tunaelekea uelekeo mmoja.
Kumbe jambo Hilo linamkwaza sana dada mtu ingawa hasemi yaani ninamaanisha dada mtu hataki niongozane na Mdogo wake.
Matokeo yake dada mtu amekuwa akipiga simu kwao kisirisiri akiongea mambo ya uwongo kuhusu Mdogo wake pamoja na Mimi lengo likiwa Mdogo wake apigiwe simu kwao kwamba aondoke hapa arudi nyumbani huko kwao kwenyewe mambo ni magumu maana ni kijijini hata dada mtu mwenyewe tu hataki kupasikia.
Niwe mkweli ninaishi nyumba ya kupanga na ndo mwaka wa 3 Toka nimeanza maisha Nina chumba na sebule Sasa Mdogo mtu alipofika sikutaka mambo mengi niliruhusu vitu vyake vyote kuwekwa chumbani na akitaka kujiandaa aingie chumbani ajiandae kasoro kulala tu. Imekuwa hivyo Toka amekuja hapa hata mwezi haujaisha.
Cha ajabu juzi dada mtu ananitumia sms anasema hataki kumuona Mdogo wake anaingia chumbani aisee nilikataa kbs nikamwambia Hilo zoezi halitafanyika maana Toka amefika hapa chumbani amekuwa akiingia mara Kwa mara na hakuna tatzo halafu Leo ghafla tu tumwambie usiingie chumbani unadhan atahisi nn pili sebuleni kumejaa hata godoro lenyewe kumtandikia tunamtandikia Kwa kujibana je vitu vyake tuvihamishie sebuleni vikae wapi nikasema hapana.
Akalalamika sana mi nikabaki na msimamo wangu. Sasa ameanzsha tabia ya kumpeleleza Mdogo wake Kila akirudi huko kwenye ushonaji kujua kama Kuna nn tumeongea na Mdogo wake au huko kwenye ushonaji mambo Yako sawa ila lengo lake anataka asikie mambo hayako sawa ili apige simu kwao kusema kwamba huyu dogo huku hakuna anachokifanya arudi home tu.
Nilipoligundua Hilo nilimpa angalizo mdogo mtu maana nimeshangaa sana huyu mwanamke mpaka simu yake ameweka password mpya ghafla wakati alikuwa hawekagi nikagundua Kuna jambo linaendelea hapa.
Jana wakati naondoka na mdogo mtu nikamwambia anipe simu yake aliponipa nilikuta sms nyingi sn za dada ake akimuhoji kama SI kumpeleleza akinizungumzia Mimi niliumia sn mbaya zaidi sms zngn zimeandikwa usku na Mimi nikiwemo ndani yaani amemchatisha Mdogo mtu sms usiku wakinizungumzia Mimi.
Nilipogundua haya yote mi nimechukua hatua za kunyamaza kimya tu siongei na mtu sjibu mtu Wala siulizi chochote Kwa mtu humu ndani na Wala sili humu ndani Wala siitikii salamu ya mtu nipo busy na mambo yangu tu.
Usiku dada mtu analia eti ye ikibidi atakunywa hata sumu au vidonge mimi skujibu.
Line za simu alizokuwa anatumia nilimsajilia Mimi nazo nimechukua maana SI ndio hizo anatumia kunizungumzia Mimi.
Na nimetoa msimamo akiondoka Mdogo mtu kisa visa vya dada ake basi nitaamini pia huyu mwanamke hawezi kuishi na ndugu yangu Wala kuishi na Mimi kama ameshindwa kuishi na Mdogo wake wa damu kwaiyo na yeye ataondoka so achague Moja.
Sasa wakuu nimekosea wapi hapo kosa langu ni lipi?
1. Inaonyesha unamlinda sana huyo mdogo mtu. Una maslahi gani naye hadi utoe ulinzi mkubwa kiasi hicho?
2. Hapo ni ndugu na ndugu wanatiliana shaka. Inawezakana kabisa wewe usiwe unataka chochote toka kwake, lakini je, unatumia jia gani kumwaminisha mwenzio kuwa humnyandui mdogo wake?
3. Inakuwaje wewe unaingilia ugomvi wa mtu na mdogo wake? Huna ndugu zako wa kuwatetea kwa kiwango hicho?
4. Umesema anapiga simu kwao. Hii inaonyesha hata ndugu zake wanakijua unachokifanya, ingawa kwa stori za upande mmoja. Sasa kwanini ufarakanishe familia kisa kutoa lift? Utapungukiwa chochote ukiacha?
5. Yaani kabisa mdogo wake anafanya anayoyataka chumbani kwenu, kasoro kulala pekee..!! Huu ni ujinga wa kiwango cha SGR..!! Huwezi ruhusu chumba chako mtu mwingine awe huru nacho kama vile chake. Wewe humgongi kweli? Tena inawezekana unamgongea humohumo chumbani kwenu na ndiyo maana unamtetea sana.
