Watu wa JF wamejaa roho mbaya na husda. Ukisoma maandiko yote hapa, utafahamu kuwa wote wana nafsi zilizojaa takataka na mawazo hasi.
Kwanza, mimi nikupongeze. Una msimamo wa kiume na hupaswi kuyumbishwa. Simamia kile unachokiamini kuwa ni sahihi.
Pili, kama nia yako ni njema, humtetei shemeji yako kwa sababu una tamaa naye au malengo ya kuwa na mahusiano naye, basi nakuombea Mungu na akubariki. Lazima ujiweke katika nafasi ya unayemtendea hivyo.
Je, ungelikuwa wewe ndiye binti hakuna kinachoendelea baina yenu alafu kesho ufukuzwe na kukatishwa mafunzo yako kwa husda tu za nduguyo ungejisikiaje? Ni ndugu wangapi ambao hawapendi maendeleo ya wenzake?
Kama mkeo ana wasiwasi, kwa nini asiseme hadharani na badala yake anamkaba nduguye?
Tatu, acha kununa. Zungumza kwa misimamo. Mpe simu yake aendelee na mawasiliano.
Nne, wapigie wazazi wao. Waeleze moja mbili tatu. Wao wataona namna njema ya kuondoa hiyo sintofahamu.
Tano, kama uwezo upo basi fanya mipango umpangie huyo shemeji yako. Acha kusindikizana naye.
Kila la kheri Mkuu.