Anataka muda wote awe na msaidizi wa kazi za ndani, yani housegirl, lakini hawezi kukaa naye hata kwa miezi miwili!!!

Samahani

JF-Expert Member
Oct 29, 2018
222
335
Wadau wa jukwaa, naomba kuliweka hili mbele yenu, huenda roho yangu ikapoa.

Uwezo wa maisha bado haujanipa kibali cha kujenga nyumba yangu, na hivyo naishi katika nyumba ya kupanga yenye vyumba viwili vya kulala. Kwa bahati mbaya, Mke wangu wa ndoa ambaye tumejaliwa naye mtoto mmoja tu sio mwajiriwa, hivyo yupo nyumbani akipambana na majukumu ya nyumbani pamoja na bishara ndogo ndogo ambazo kwakweli ni muhimu sana kwa ustawi wa familia yetu.

Lakini ajabu ni kuwa, mama huyu "Anataka muda wote awe na msaidizi wa kazi za ndani, yani housegirl, lakini hawezi kukaa naye hata kwa miezi miwili!!!". Pamoja na mimi mwenyewe kupendelea walau kuishi na ndugu ili kuwasaidia pia kimaisha, iwe ni wa kwangu au wa kwake, mara zote hataki, na anasisitiza kuwa anahitaji "House Girl"

Mara kadhaa nimeshamruhusu kwa shingo upande, lakini ajabu ni kuwa, hakai na wadada wa kazi kwa zaidi ya miezi miwili. Nashindwa kuelewa hasa tatizo ni nini, lakini kila baada ya mwezi mmoja na nusu au miwili, wadada hawa huamua kuondoka, na wapo ambao huniaga kuwa wanakwenda kusalimia kisha hawarudi, huku wengine wakaiamua kutoroka usiku wa manane au alfajiri sana!!

Mosi, Nashindwa kuelewa ni kwanini hasa mama watoto anahitaji kuwa na dada wa kazi ilhali nyumba yetu ni ndogo, yenye majukumu yanayoweza kusimamiwa na yeye peke yake na mimi kumsaidia pia kwa kuwa kila nitokapo kazini nina jukumu la kuungana naye kumalizia baadhi ya kazi za nyumbani.

Pili, ni hii adha ya wasichana wa kazi kuondoka mapema wakati ndio kwanza tunaanza kuwazoea. Mbaya zaidi, ni mara zote nalazimika kuwapigia ndugu wa mikoani wanisaidie kupata wafanyakazi. Hili la kupata adha ya kuwapigia ndugu, jamaa na marafiki zangu kila mwezi linanikwaza mno, na kwakweli nimeshakata shauri kuwa, SITAHANGAIKA TENA!!

Nisaidieni niwe na amani tena!!
 
Haezi kuishi na wadad vzr..mchunguze kauli zake na matendo yake hueza kuta anawanyanyasa wakat wale wanatakiwa wapate upendo kama mwanao ndo utadumu nao

Me nakushauri mwache apambane na kazi za hapo mdada wa nn wakt yupo nyumbani au anataka akazurure
 
Kama ni swala kutafta housegal wewe jitoe atafte mwenyewe awalipe yeye vinginevyo yeye ni mkeo na kumbe mtoto n mmoja tu anaweza kujipangilia mwenyewe kazi zake wewe ukirudi waweza malizia zilizobakia akizidi kusisitiza mfanya kazi atafte yeye agharamike yeye

Kuhusu kutokukaa nao vizur na kuamua kuondoka inawezekana anawanyanyasa au kuna vitu anafanya haviwapendezi maybe kama una uwezo ujaribu mara ya mwisho na uweke cctv camera ujue ni kitu gani hua kinaendelea ukiwa haupo
 
Huyo ana gubu

Fanya uchunguzi ujue tatizo linalofanya asikae na dada wa kazi ni nini

Inawezekana akawa kakosa imani nao kwakuhisi unawatongoza.labda ana wanyayasa au labda ana kasumba nyingine ambayo haishabihiani na hao wadada wa kazi
 
Wanawake wengi wa kitanzania hawawezi kuishi na wadada wa kazi kwa kuwa
1. Wana maneno sana
2. Wanaishi na mtu na kumnyanyasa na kumsimanga
3. Huwa wanajiona matajiri kwa kuwalipa hawa wadada elfu arobaini
4. Wavivu mno mtu anataka afuliwe mpaka chupi,sidiria na kumiminiwa chai

Pia wengi visirani sana
 
Pole sana ndugu ila uenda Mke wako
1) anafujo sana kwa hao mabinti
) mabinti wanamchanganya sana(japo si rahis wote wamchanganye)
3) labda ana wivu anajua wakianza kunawili utawatamani
4) hana haja na binti wa kumsaidia ndiyo maana hataki mlete ndugu bali anataka kujionesha kwa mashoga zake kuwa na yeye anamfanyakazi
5)ana roho ya ubinafsi.
6) ana roho mbaya
#lolote laweza au lisiweze kuwa jibu kati ya hayo#
 
Haezi kuishi na wadad vzr..mchunguze kauli zake na matendo yake hueza kuta anawanyanyasa wakat wale wanatakiwa wapate upendo kama mwanao ndo utadumu nao

Me nakushauri mwache apambane na kazi za hapo mdada wa nn wakt yupo nyumbani au anataka akazurure
Hakika hata ,mimi
Kama ni swala kutafta housegal wewe jitoe atafte mwenyewe awalipe yeye vinginevyo yeye ni mkeo na kumbe mtoto n mmoja tu anaweza kujipangilia mwenyewe kazi zake wewe ukirudi waweza malizia zilizobakia akizidi kusisitiza mfanya kazi atafte yeye agharamike yeye

Kuhusu kutokukaa nao vizur na kuamua kuondoka inawezekana anawanyanyasa au kuna vitu anafanya haviwapendezi maybe kama una uwezo ujaribu mara ya mwisho na uweke cctv camera ujue ni kitu gani hua kinaendelea ukiwa haupo
Wonderful!! Hakika nauchukua huu kama ulivyo.. Nilikwishamwambia kabisa kuwa habari za mimi tena kujihusisha kumtafutia hawa wadada wa kazi kwakweli hapana, apambane ili awapate ambao anaweza kukaa nao.. Ukweli kuwa sioni umuhimu wa kuwa na msichana wa kazi nimeshajadili naye, na kuna wakati huwa anakubali, kisha baada ya wiki tu anaanza tena maswali kuhusu kuwa na msichana wa kazi, tena na kununa juu!!!
 
Nakushauri usikate tamaa, hebu tafuta tena msichana mwingine, then hakikisha una mdadisi kero anazopata au furaha anazopata kutoka kwa mkeo.
Ukikata tamaa kuwa hutatafuta msichana utakuwa bado hujatibu tatizo. Cha muhimu hakikisha unajua chanzo cha hao wasichana kuondoka.
Kwakweli huwa nanatamani wakati fulani kuwa karibu na hawa wasichana ili walau nijue nini kinachowasibu maana kwangu hawa ni ndugu kama tu walivyo ndugu wengine. Lakini mara zote napata hofu kuwa, huenda ataanza kunihisi vibaya kuwa nina ukaribu usiostahili na wadada wa kazi.. Na hili limenifanya mara zote kuwa mbali nao KABISA!!

Mathalani, wife amejiwekea utaratibu. Nikifika tu nyumbani, hata kama dada wa kazi alikuwa ameketi sebuleni akiangalia TV, itamlazimu anipishe ili nisikae naye karibu, na kwa kuwa sipendi tabia hii, ninapofika tu nyumbani huwa ama ninaketi chumbani au nakuwa busy nikiwa nasaidia kazi hasa zile za nje. Najua akina dada wengi wanapenda kutazama TV, na nikilazimisha mimi kukaa sebuleni, ina maana ni kuhalalisha wadada hawa kukosa starehe hii muhimu, hivyo ninaangalia TV ya chumbani ama niache kabisa maswala ya TV
 
Back
Top Bottom