Anataka mchukua mwanangu kinyemela

Anataka mchukua mwanangu kinyemela

Latoya

JF-Expert Member
Joined
Apr 18, 2013
Posts
660
Reaction score
457
Habari za mida wanabodi
Nikiri tu mimi ni member mzuri sana wa JF.Ok tuache soga ndefu,ni hivi kuna mwanaume nilizaa nae kitambo kiasi na baada ya mtoto kuzaliwa tu akanipotezea mimi na mwanangu.Bt hey tembo hashindwi na mkonga wake nikamlea mwanangu peke yangu since mimba hadi saivi akiwa kijana flan amazing,ana afya bora,ana akili sana,etc

Niliamua kufanya hivyo baada ya yeye kujitenga na kutonisupport kwa lolote si mimi wala mwanangu.Nikaacha kumuomba matumizi na kadhalika in short nilikata mawasiliano naye kabisa.mwanzo nilikuwa namsihi aniboost hata matumizi ya mtoto akagoma,so nikafanya maamuzi magumu,nikamwacha aendelee na maisha yake na nikawa single mom rasmi and am proud of that.

At the moment mimi na my prince we are ok,ana afya bora thanks to my GOD,and mimi pia nina mahusiano na mtu mwingine tayari and we are happy.

Ishu niliyoileta mhusika,baba wa mwanangu ameanza kufanya mawasiliano,its ok ukizingatia niko na mwanae.tatizo ananisihi nimpe mwanangu anisaidie kulea,ila naona kama trick ya kutaka kumchukua kijana wangu jumla.

Mara zote nimemwambia subiri atimize miaka saba then afate taratibu za kisheria amchukue.Anadai amemmiss mwanae anataka kuishi naye na hatonizuia kumuona.funny !!!mtu ambaye hajawahi toa hata mia ya chakula cha mwanae leo anaona ana haki ya kuchukua furaha yangu.ukizingatia ana kipato kizuri tu.

Amenambia kama ni mtoto mwingine atanipa,ila mie nimemjibu siko tayari kuzaa naye tena.Kwani alinitelekeza mimi na mwanangu.huko aliko azae mtoto mwingine ama wengine huyu nataka nimlee mwenyewe .He is my joy,life and prestige(my son,my little man).

Naombeni ushauri kwakuwa najua jamaa anataka kumchukua mwanangu mazima.jambo ambalo siko tayari.nashukuru Mungu nina ka uwezo ka kumlea.ikifika muda nikashindwa nitampa kwa ridhaa yangu,kwani naangalia maslahi mapana ya mwanangu .Ila kwa sasa sijashindwa,nayaweza yote katika yeye anitiaye nguvu.

Na sina mpango wa kuzaa tena,maumivu aliyonipitisha yamenifunza .Wanasema mjinga wakati wa kwenda .karibuni wadau,nahitaji mawazo yenu kwa hakika .
 
Tafuta mwanasheria
ninavyojua mtoto chini ya miaka kumi anatakiwa kukaa na mama
unless kuwe na sababu zingine

anzia pia ustawi wa jamii
Ok The boss thanks,nilikaa kimya nikawa nafanya yangu,lakini naona kila leo kauli yake ni hiyo ya kumchukua mtoto.Je alivyonitelekeza nikaaibika asijulikane baba wa mtoto hata kwa majirani kipindi chote hiko,anaona si hoja.Nadhani ni wakati sasa nifanye maamuzi magumu.sijawahi mnyima kumwona mwanae ila kumchukua aache nikishindwa kumlea nitamkabidhi mwenyewe bila shuruti
 
Kwani umeshindwa kumlea mwanao?!...kama unaweza kumlea bila yeye haina haja ya kumpa kwanza mtt kwenda kuishi na watu ambao hawafahamu itamsumbua sana halafu ataona kama umemtelekeza
 
Huu ndio tunauita ubinafsi, mtoto mlitafuta wote alafu unatumia neno my prince inamaana ye hamhusu? Kukataa kulea haitoi uhalisia wa ubaba wake na umiliki wa huyo mtoto.

Ushauri wangu tafuteni sehemu tuliivu mkiwa wawili mjadili hatma ya huyo mtoto na jinsi ya kumlea nina imani hakita haribika kitu
 
Kwani umeshindwa kumlea mwanao?!...kama unaweza kumlea bila yeye haina haja ya kumpa kwanza mtt kwenda kuishi na watu ambao hawafahamu itamsumbua sana halafu ataona kama umemtelekeza
Na hilo ndilo nalohofia,saivi kaona mwanangu kanona anamtamani,anadhani ni miujiza,ni kujinyima na kuhakikisha mwanangu anapata lishe bora na mazingira bora ya ukuaji,si kila mtu yuko tayari kujinyima akulele mtoto miaka hii
 
Huu ndio tunauita ubinafsi, mtoto mlitafuta wote alafu unatumia neno my prince inamaana ye hamhusu? Kukataa kulea haitoi uhalisia wa ubaba wake na umiliki wa huyo mtoto.

Ushauri wangu tafuteni sehemu tuliivu mkiwa wawili mjadili hatma ya huyo mtoto na jinsi ya kumlea nina imani hakita haribika kitu
Cc wanaume huwa hatusapot ujinga
 
Huu ndio tunauita ubinafsi, mtoto mlitafuta wote alafu unatumia neno my prince inamaana ye hamhusu? Kukataa kulea haitoi uhalisia wa ubaba wake na umiliki wa huyo mtoto.

Ushauri wangu tafuteni sehemu tuliivu mkiwa wawili mjadili hatma ya huyo mtoto na jinsi ya kumlea nina imani hakita haribika kitu
No si ubinafsi,naangalia maslahi mapana ya mwanangu.at least atimize umri wa kujitambua,ndio kwanza ana miaka 3.isitoshe sijawahi mnyima kumwona, pamoja na hayo mwanzoni alinambia yeye hakuwa na mpango wa kuzaa,so hilo ni langu nilibebe,nikalibeba.nikakubali majukumu kama mwanamke na mama.leo imekuwaje?imagine mtu anakuja mwona mwanae hata machungwa tu hamletei?atajali malezi na makuzi ya huyu mtoto kweli?yeye anamwona kanona anadhani ni muujiza,malezi ni kujitoa na kujikana.
 
Malezi mazuri ya mtoto ni kutoka kwa wazazi wote wawili...

Even after all what the dude has made you go through, you sound still loving the dude...

Kukupa ushauri ni ngumu kwa sababu bado unampenda huyo jamaa..

Cc: mahondaw
Am done with him,sijawahi mchukia lakini hilo halifanyi niwe mjinga anigeuze incubator,nilijifunza na sijawahi rudi huko.mahusiano kati yangu naye yalivunjika nilimpomzaa mwanangu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom