Tulioacha wake zetu kwa sababu ya usaliti waliotufanyia tukutane hapa

Johnson12345

JF-Expert Member
May 29, 2023
206
422
Habari wana JF. Leo na leta kisa changu hiki kilichonitokea, nina miaka 38 sasa. Ni Baba wa watoto 2 nilizaa na wanawake wawili. Wa kwanza mke wangu wa pili niseme kama mchumba tuu.

Miaka kama 12 hivi iliyopita nilikutana na mdada mmoja kanisani, nilimpenda kwa muonekano wake hasa mavazi yake ya heshima. Na maneno yake na sauti yake ilikuwa nyembamba kiasi.

Nilijitahidi na nikafanikiwa kuingia nae kwenye mahusiano tulikaa kwa miaka miwili hatimaye nikafanikiwa kuingia kwenye ndoa Takamine.

Tulikaa kwa muda kwenye ndoa mpaka kuweza kupata mtoto mmoja wa kike. Mimi na mke wangu ni black niseme na hata kwao mke wangu ni black na kwetu mimi pia ni hivyo. So dogo alikuwa ni black kama sisi.

Tuliendelea kwenye ndoa nakumbuka siku moja mke wangu aliniambia kuwa yeye hapendi mwanaume msaliti kwenye mapenzi na kama akisaliti basi asijue kabisa.

Mimi ni mfanyabiashara nina biashara zangu tuu. Mke wangu yeye ni mfanyakazi wa benk moja hivi DSM hapa.

Nakumbuka mke wangu baada ya kujifungua nilimnunulia gari pale Mwenge, Toyota harrier alikuwa ni kujimwaga tuu town.

Sasa baada ya miaka 2 na nusu hivi siku moja mke wangu alichelewa kurudi home alirudi kama saa 3 jioni hivi. Aaa mimi nikajiuliza hii sio kawaida yake sikumuuliza kitu chochote, maana hata alivyorudi alirudi kama anahangika na kama ana hofu flani. Sikumuuliza chochote ila nikawa na wasiswasi kuwa kashaanza kuliwa na kidume kingine. Sikutaka kuomba game usiku nikakausha.

Sasa mimi huaga ninasafiri sana, ila huo mchezo uliendelea kama 3 weeks japo alikuwa anajitahidi kuwahi kurudi anarudi kama saa 12 jioni hasa. Wakati yeye mara nyingi ni saa 10 mpaka 11 anakuwa tayari kasharudi. Nilimuuliza akajibu tuu shughuli. Tukaendela na ndoa baada ya miezi kama 2 hivi nakumbuka mke wangu sikukutananae kama siku tano hivi. Nikakutanae siku moja kabla ya kusafiri.

Kesho yake nilisafiri kwenda nje kwenye shughuli zangu. Baada ya kukaa kule kama 2 weeks wife akaniambia kuwa ana ujauzito wa 2 weeks mimi aaa kwa vile siku ile kabla ya kusafiri nilikutatane na nilicum kwenye pu*sy magoli 3, nikaona poa tuu. Japo kwa kubadilika kule nikaona hii inaweza ikawa sio ila nilikausha tuu.

Mimba hiyo nilirudi nikanyamaza tuu, mimba ilikuwa mpaka mtoto kuzaliwa. Baada ya kujifungua mimi nikasema fresh japo baada ya kumuona mtoto alikuwa ni white, mimi mmmh hata kwa wife yeye mwenyewe alishtuka. Mimi nikaona labda mtoto alitoka tumboni, nikamwambia nenda kwenu ukapate uzazi akagoma, nikamwambia kama unataka kwenda kwetu kwa my mama basi nikupeleke akagoma pia. Mimi mmh nikamuacha. Baada kama 3 weeks still dogo ni mweupe balaa. Mimi bwana uvumilivu ulinishinda nikaamua kumwambia ukweli tuu kuhusu mtoto.

Nilimwambia kuwa mtoto ni mweupe mbona nina wasiwasi sana, siunajua wanawake akaanza inaamna uniamini au vipi, mbona mimi nakuamini. Katika kujibizana maneno mwishoni akasema kama umtaki mtoto wangu sema tuu.

Mimi nikaamua kupiga simu kwao nikawaambia mke wangu amejifungua mnajua? Wakasema hawajui ila walikuwa wanajua tuu ni mjamzito. Mimi nikasema ana mtoto wa kiume now. Dada yake na mama yake wakasema tutakuja nikasema sawa, si wakaja bwana kwanza wao walishangaa dogo ni white. Niliona reaction yao walikuwa ni watu sura za huzuni flani na kunitazama mimi. Niliamua kuondoka home. Nilikaa kwenye mgahawa mmoja kule Kariakoo mpaka saa 6 night kwa mawazo yale.

Niliamua kurudi home na kuaanza kumuuliza maswali kesho yake mke wangu nilimuuliza maswali mengi sana mwishowe alikataa, nikamwambia mimi nipo tayari kwenda kupima DNA. Yeye akasema kama utaki mwanangu basi. Nikaamua kumfukuza home nikamwambia nenda kwenu sikutaki hapa.

Nakumbuka nilimnyang'anya funguo za gari. Ilikuwa Jumapili alitaka kuondoka na mtoto wangu wa kike nilimkatalia akaamua kuondoka yeye mwenyewe na kwenda kwa rafiki yake. Hakwenda kwao.

Nilimpigia dada yake na kumueleza, Dada yake akaamua kumtafuta na kumchukua na kwenda kwao. Mimi nilifikisha ujumbe home walishtuka sana.

Baada ya kama wiki 3 hivi wakasema basi tukutane pande mbili tujue shida ni nini, mimi niliwaambia shida mtoto nina wasiwasi sio wangu.

Wakasema basi twende tukathibitishe kwa DNA, ila mke wangu anagoma kabisa akasema kama haniamini basi.

Walijaribu kutumia mpaka viongozi wa dini lakini still aligoma kabisa kuhusiswa kwenye majalidiano, yeye anadai mimi simuamini kama simtaki mtoto basi.

Ila alipokaa na wazazi wake na kumuuliza vizuri alikiri kuwa alikuwa na mahusiano na mtu mmoja ambaye ni ofisi ya jirani na benk anayofanyia hapa DSM, jamaa ni kweli ni white so dogo ni wake.

Ila baadae wazazi wake walikuwa hawataki ndoa kuvunjika waliniomba niende kwa tuyamalize, walitumia viongozi mpaka wa dini kunishawishi.

Ila mimi niliona ni usaliti mkubwa sana tena wa kuacha alama.
Mke nae anasingizia Bahati mbaya sijui shetani alimpitia. Nikaona ni uwongo tuu hakuna kitu hapa. Niliamua kuvunja ndoa ile na nilifanikiwa, niliumia sana tena sana nilijiuliza maswali mengi ina maana yote haya niliyomfanyia alikuwa haridhiki au ni nini. Daaa nilimfanyia vitu vingi sana huyu dada.
Alijitahidi kuniomba msamaha, pamoja na mama yake na dada yake kwa pamoja ila mimi wala.

Mama yake alienda mbali na kusema kama mtoto hutamkubali basi yeye atakaa na mtoto ila mwanae nisimwache, Baba yake akasema kufanya hivyo ni kutetea ujinga na uzizi wa mtu,
Baba yake akasema yeye hakai na mtoto wa mtu mbaye wazazi wake wapo na wana maisha yao. Kuna kipindi mke wangu alijaribu kumtumia my brother ili kumsamehe ila ilishindikana.

Na alileta kisingizio cha ndoa yetu ni ya kanisani. Mimi nikamwambia kwa hilo ulilofanya sina hamu na wewe tena, nikamwambia kuwa nipo tayari kuzini na malaya ila sio wewe.

Mwishowe nilijikuta naingia kwenye mahusiano na mnyarwanda mmoja mdada nilikutanane Zanzibar, katika safari zangu za kupunguza stress.

Mdada ni mrembo si unajua wanyarwanda, nilikaa nae kwenye mahusiano kama mwaka hivi, kwa uzuri ule alinifanya nimsahau mke wangu. Ila kusema ukweli jamani watusti wazuri balaa . Akitabasamu tukiwa kitandani asalala, na pua zao, kwa kipindi kile nilikuwa na furaha sana. Ila niliachana nae baadae.

Mwaka 2020 nilikutana na mdada mmoja hivi nilianzisha mahusiano nae ila nilimueleza yote yaliyonitokea, mwaka jana mwezi January alibeba mimba yangu ila baada ya kujifungua alifariki na kuacha mtoto wa kike ambaye mimi ndio Baba.

Dogo yupo kwa mama yake. Naendaga kumsalia na kupeleka mahitaji.

Sasa tangu ex wife wangu kujua hilo kuwa nina mtoto na mama yake katangulia, SMS, simu sana anaomba turudiane ili anisaidie kunilelea mtoto. Simu ni nyingi mpaka naona kero, kuna siku alienda mpaka kwa wazazi wangu anawaomba wajaribu kunishawishi yeye yupo tayari kulea mtoto kama wake. Ila mimi kwa usaliti ule daaa. Sina hisia nae kabisa.

Ila najua kwa nini anataka kurudiana na mimi.
Mimi kwa sasa maisha yangu yapo fresh sana tena fresh. Yule mdada mnyarwanda alinisaidia sana kimawazo hasa ya biashara na connection, niseme ukweli tuu alinisaidia sana maana yeye ni mtu wa kuagiza vitu China na Japan, alinisaidia sana, yeye anafanya kazi kwenye kampuni ya crystal venture ipo Rwanda, ndo anafanya nao biashara nao sana na yeye ni mmoja wapo nafikiri.

Mke wangu misamaha yote kesho anaendelea kuomba, naamini kujutia ila simuhitaji tena.

Home wananishauri turudiane coz wote tuna watoto nje,
Ila mimi kwangu nimesema NO.

NB; AKINA DADA SISI WANAUME MNAVYOTUCHEAT HUWA TUNAWAZA VITU VINGI SANA, JUST IMAGE UMEMTOLEA MAHARI MKE KAMA MIMI NILITOA 3.5 MILLION, NDOA UNAGHARAMIA, UNAMLETA NYUMBANI KWAKO, UNAMUHUDUMIA, MPAKA UNAMPA NA GARI MWISHOWE UNAAMBULIA USALITI, SISI WANAUME TUNAUMIA SANA NA KUWAZA MENGI, WHY KAFANYA HIVI????
 
Pole sana. Ndo shida ya kucheat kwa mke, akipata ujauzito nje ni ngumu kujua wewe ulijua baada ya ndogo kuwa mweupe kiasi hicho.

Ila angecheat na mtu mweusi usingejua bro. Wapo wanaume wengi hawajui na wanalea hivyo bila kujua.
Mme akizaa nje itajulikana mtoto si wa ndoa, ila mke akizaa nje ni ngumu sana kujua kaka, japo wewe ulijua.

Wanawake, unamtongoza wewe, unapeleka posa wewe na pesa ndani, unatoa mahari wewe, unaandaa harusi wewe, unamleta nyumbani kwako, unamuhudumia wewe, unamnunulia gari wewe, unamlisha unamvesha wewe lakini still unaambulia usaliti.

Ni Kweli ulivyosema huwa tunaumia sana.

Ebu Kapeace njoo ujibu hoja huku.
 
Pole sana .
Ndo shida ya kucheat kwa mke , akipata ujauzito nje ni ngumu kujua wewe ulijua baada ya ndogo kuwa mweupe kiasi hicho.
Ila angecheat na mtu mweusi usingejua bro.
Wapo wanaume wengi hawajui na wanalea hivyo bila kujua.
Mme akizaa nje itajulikana mtoto si wa ndoa , ila mke akizaa nje ni ngumu sana kujua kaka , japo wewe ulijua.

Wanawake , unamtongoza wewe, unapeleka posa wewe na pesa ndani, unatoa mahari wewe, unaandaa harusi wewe, unamleta nyumbani kwako, unamuudumia wewe, unamnunulia gari wewe, unamlisha unamvesha wewe lkn still unaambulia usaliti.
Ni kweli ulivyosema uwa tunaumia sana.
Ebu Kapeace njoo ujibu hoja huku.
Wakati wife anacheat ye alikuwa wapi?
 
Back
Top Bottom