Ana sifa karibia zote ninazohitaji, ila tatizo elimu yake

Ana sifa karibia zote ninazohitaji, ila tatizo elimu yake

tindikalikali

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2011
Posts
4,854
Reaction score
1,143
WanaJF,

Nipo katika mahusiano na mwanamke ambaye elimu yake ni std 7, mimi nina elimu ya pia nipo certified na moja professional board hapa Tanzania! Kiukweli ni mtu anayejali na anaonesha kunipenda pia anatamani niwe mme wake, tatizo linakuja baada ya muda huu niliokuwa naye, uwezo wake wa kupambanua mambo uko chini sana.

Yani anachojua yeye ni whatsapp, FB, Instagram na habari za wasanii na movie! Mambo ya uchumi, siasa, technolojia na jinsi dunia inavyoenda kwake ni hakuna! Kiukweli nakosa uhuru kabisa kwani inanibidi nijilimiti vitu vya kuongea naye na pia siwezi kabisa changanya kimombo kwenye maongezi ya ana kwa ana au text na mimi nilishazoea hivyo.

Naomba nieleweke kwamba sijaandika haya kwa ajili ya kubeza watu wenye elimu ndogo hapana, ila napata wakati mgumu kujiadjust ili niende sambamba naye! Je watu mliooa watu wa aina hii mnakutana na changamoto zipi?

Natanguliza shukrani
 
Huyo ndo mwenyewe sasa, mpnandishe juu kidogo n wewe shuka chini kidogo, utazoea tuu!! kama unataka stress, tafuta "msomi"!
Ila kama hana elimu alafu anajua mambo ya whatsapp, instagram etc, nalo janga! Hawachelewi kutongozwa kwenye whatsapp na vipicha picha!!
 
Braza oa huyo huyo... cz atakuheshimu na kukujali.. wasomi ni headache atakupanda kichwani.. thn mpeleke QT.. moyo hauna elimu best
 
mapenzi ni upendo. hivyo vingine ni nyongeza tu. hata hivyo ukipata aliyesoma halafu akawa na upendo wa kweli nayo poa. Ila usimpate mwenye elimu kubwa halafu akawa hana mapenzi ya dhati, utajuta maisha yako yote.
kaz kwako

Mkuu na hiyo ndiyo hofu yangu, naweza nikamkimbia huyu na nikaingia sehemu ya ajabu!!
 
Braza oa huyo huyo... cz atakuheshimu na kukujali.. wasomi ni headache atakupanda kichwani.. thn mpeleke QT.. moyo hauna elimu best

Ni kweli mkuu, maana hata kukosa elimu kuna sababu nyingi nyuma yake!!
 
mkuu wakishasoma huwa wanageuka hawa, hilo kwa kweli bado sijalifikiria!!!

ushawahi kuwaza siku ukifa darasa la7 ataimudu vipi family?
naweza kukusapoti about shule mana hadi aje amalize chuo.sio leo na.kazi zinasumbua hata kama una masters,
nashauri mfungulie duka hivi,la nguo au biashara ya chakula inalipa kulingana na eneo,
kimsingi awe na shughul ya kumuingizia kipato shule is veree late now
 
mkuu wakishasoma huwa wanageuka hawa, hilo kwa kweli bado sijalifikiria!!!
Sasa kama hutaki afanane na wewe mkubali kama alivyo na kama umeridhika na akili yake hiyo ya facebook na kigodoro
endeleanae kizungu utakujaongea na wanao au na watoto wa shule..........
 
tindikalikali

Kwanza Hongera sanaa kwa kuandika uzi wako kiustadi, inaonesha hii ni reality, Mi nataka kujua tu kuhusu Umri wake ili tuone makadilio ya kwenda shule kama atayamudu kabla hujaM-mimba
 
Last edited by a moderator:
yani anachojua yeye ni whatsapp, FB, instagram na habari za wasanii na movie!! Mambo ya uchumi, siasa, technolojia na jinsi dunia inavyoenda kwake ni hakuna!! Kiukweli nakosa uhuru kabisa kwani inanibidi nijilimit vitu vya kuongea naye na pia siwezi kabisa changanya kimombo kwenye maongezi ya ana kwa ana au text na mimi nilishazoea hivyo!!


Natanguliza shukrani!!
Muda mwingine ni interests za mtu pia, japo elimu ina-matter ila sio kigezo. Kuna watu na Ph.D zao na bado hawana habari na yanayoendelea duniani.

M-train ili muweze kwenda sambamba, halafu na wewe una-compromise kidogo mnakutana kati kati.
 
Kwanza Hongera sanaa kwa kuandika uzi wako kiustadi, inaonesha hii ni reality, Mi nataka kujua tu kuhusu Umri wake ili tuone makadilio ya kwenda shule kama atayamudu kabla hujaM-mimba

ana 25!!
 
As long as mnapendana, anajitambua na Unaona Kabisa Ni Mtu anayekufaa kujenga naye familia, just marry her. Kuna watu wana elimu zao, ila ndo elimu zetu tu za makaratasi, Hana analolijua. Na kuhusu kushinda fb, insta, wasap etc Ni hulka tu ya Mtu, jitahidi kuongea naye ili apunguze hayo matumizi ya simu. Unaweza kumpeleka hata English course au akaenda akasomea ujuzi Fulani.., eventually mambo yatakuwa poa.
 
Back
Top Bottom