Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,466
- 113,550
Wanabodi,
Hii ni Makala yangu ya Nipashe Jumapili
Tanzania tulipopata Uhuru ile Desemba 9, 1961, sisi Tanzania tukiwa na rasilimali lukuki, lakini sasa hapa tulipo, tukijilinganisha na baadhi ya wenzetu nchi tulizopata nazo uhuru, wengi with nothing compared, kiukweli kabisa, sisi tumeachwa mbali!,
Nikijiuliza tatizo ni nini, ndipo nimekuja na conclusion yangu, sisi Tanzania tuna tatizo katika upangaji wa vipaumbele vyetu!.
Tangu enzi za Nyerere, tumepata uhuru, tukiwa na maadui wakubwa watatu ambao ni adui Ujinga, Umasikini na Maradhi, leo baada ya miaka 60 sio tuu maadui watatu hao bado wapo, bali tumeongeza na maadui wengine wawili wa Rushwa na Ufisadi!.
Falsafa ya Maendeleo ya Mwalimu Nyerere "Ili tuendelee, tunahitaji vitu 4, Watu, Aridhi, Siasa Safi na Uongozi Bora", hivi vyote vinne tulikuwa navyo, sasa tulikwama wapi?.
Falsama hiyo hiyo ilikuwa na makosa, kwa kukinzana na Adam Smith kwenye Land, Labor, Capita na Interprenaship. ilikuwa na omission ya Capital.
Ile Siasa Safi na Uongozi Bora ni kitu kimoja, tulihitaji Capital, uwekezaji mkubwa.
Kwenye upangaji wa vipaumbele vyetu, Mwalimu alikosea, Mwinyi akakosea, Mkapa akakosea, JK akakosea, JPM akakosea, na sasa Samia, asiposaidiwa kwenye hili la upangaji vipaumbele vyetu, pia Samia atakosea, hivyo natoa wito, tumsaidie ili asikosee kwa kuangazia maeneo ya vipaumbele ambavyo huko nyuma yalipuuzwa.
Moja ya maeneo haya ni eneo la sekta ndogo ya umeme.
Ungana nami katika mfulilizo wa makala hizi za "Kwa Maslahi ya Taifa", ambazo hutoka kila Jumapili kwenye gazeti la Nipashe, sasa zitakuwa zinaandamana na kipindi cha TV, ambacho kwa kuanzia, kitakuwa kinarishwa na TBC na ITV kuanzia wiki hii.
A 5 min short version
. A full 30 min Prog.
Makala yenyewe ni Hii
MAENDELEO NI NISHATI, NI KOSA KUBWA NISHATI KUTOKUWA KIPAUMBELE
Moja ya kero kubwa kwa Watanzania ni kero ya kukatika katika kwa umeme, Waziri January Makamba amesema, kunachangiwa na ukuaji wa ghafla wa uchumi wa mtu mmoja mmopja, watu wengi zaidi sasa wanatumia vifaa vya umeme ukilinganisha na kule nyuma, hivyo peak demand ya matumizi ya umeme kwa wakati mmoja, kuongezeka maradufu, na kusababisha instability.
Waziri Makamba, amemalizia kwa kuwahakikishia Watanzania, serikali ya awamu ya 6, chini ya Rais Samia, imedhamiria kwa dhati, kukabiliana na changamoto zote zinazoikabili sekta ya nishati, miradi ya kupeleka umeme vijijini, iko pale pale, Tanesco iko kwenye mageuzi makubwa ya kiutendaji kuboresha huduma zake.”
Shida zilizopo tunazijua, changamoto tunazijua, majawa tunayajua, kinachohitaji ni subra na uvumilivu, na baada ya muda sii mrefu, kukatika katika umeme, kutakuwa ni historia”
Hili tatizo la Upangaji wa Vipaumbele Vyetu, litajirudia very soon, baada ya nishati ya kupikia na umeme majumbani nishati muhimu sana ni mafuta ya petrol na dizeli. Kufuatia vita vya Ukraine, mafuta yatapanda tena bei kwenye soko la dunia kama enzi za vita vya ghuba, watu wanaojua kupanga Vipaumbele kupitia kufanya SWOT and PEST Analysis by now tungeishajua mafuta yatapanda sana bei na kuanza kujipanga kwa mitigation steps kabla hayajapanda ili kuzuia kupanda bei, na sio kusubiri yapande, yazue taharuki ndipo msikie vikao vya kukutana ku mitigate, ndipo itolewe ruzuku bei ya mafute ishuke.
Paskali
Hii ni Makala yangu ya Nipashe Jumapili
Tanzania tulipopata Uhuru ile Desemba 9, 1961, sisi Tanzania tukiwa na rasilimali lukuki, lakini sasa hapa tulipo, tukijilinganisha na baadhi ya wenzetu nchi tulizopata nazo uhuru, wengi with nothing compared, kiukweli kabisa, sisi tumeachwa mbali!,
Nikijiuliza tatizo ni nini, ndipo nimekuja na conclusion yangu, sisi Tanzania tuna tatizo katika upangaji wa vipaumbele vyetu!.
Tangu enzi za Nyerere, tumepata uhuru, tukiwa na maadui wakubwa watatu ambao ni adui Ujinga, Umasikini na Maradhi, leo baada ya miaka 60 sio tuu maadui watatu hao bado wapo, bali tumeongeza na maadui wengine wawili wa Rushwa na Ufisadi!.
Falsafa ya Maendeleo ya Mwalimu Nyerere "Ili tuendelee, tunahitaji vitu 4, Watu, Aridhi, Siasa Safi na Uongozi Bora", hivi vyote vinne tulikuwa navyo, sasa tulikwama wapi?.
Falsama hiyo hiyo ilikuwa na makosa, kwa kukinzana na Adam Smith kwenye Land, Labor, Capita na Interprenaship. ilikuwa na omission ya Capital.
Ile Siasa Safi na Uongozi Bora ni kitu kimoja, tulihitaji Capital, uwekezaji mkubwa.
Kwenye upangaji wa vipaumbele vyetu, Mwalimu alikosea, Mwinyi akakosea, Mkapa akakosea, JK akakosea, JPM akakosea, na sasa Samia, asiposaidiwa kwenye hili la upangaji vipaumbele vyetu, pia Samia atakosea, hivyo natoa wito, tumsaidie ili asikosee kwa kuangazia maeneo ya vipaumbele ambavyo huko nyuma yalipuuzwa.
Moja ya maeneo haya ni eneo la sekta ndogo ya umeme.
Ungana nami katika mfulilizo wa makala hizi za "Kwa Maslahi ya Taifa", ambazo hutoka kila Jumapili kwenye gazeti la Nipashe, sasa zitakuwa zinaandamana na kipindi cha TV, ambacho kwa kuanzia, kitakuwa kinarishwa na TBC na ITV kuanzia wiki hii.
A 5 min short version
. A full 30 min Prog.
Makala yenyewe ni Hii
MAENDELEO NI NISHATI, NI KOSA KUBWA NISHATI KUTOKUWA KIPAUMBELE
Kama kawaida, safu ya Kwa Maslahi ya Taifa, inaangazia mada anuwai kuhusu Taifa Letu Tanzania, ikijikita kwenye mada za kisiasa, kiuchumi na kijamii, na kwa mudamuda mrefu “Kwa Maslahi ya Taifa, imekuwa ikitokea kwenye makala Magazetini na mitandao ya kijamii pekee, kuanzia wiki hii, makala hizi za kwa Maslahi ya Taifa, pia zitaanza kuonekana kwenye luninga zetu, kwa kipindi cha TV kiitwacho “Kwa Maslahi ya Taifa” na kwa kuanzia, kitaanza kuonekana TBC na ITV, mambo yakienda vizuri, pia kitarushwa Star TV, Channel Ten na Azam TV, kwa lengo lile lile la kulisaidia taifa letu.
Si wengi wanafahamu kuwa ukiondoa uhai, tuliopatiwa na Mwenyeenzi Mungu, hewa tuyayovuta, na maji, kitu muhimu kuliko kitu kingine chochote ni Nishati. Bila hewa, maji na nishati ya jua, hakuna mmea wowote unaoweza kuota, hivyo dunia kuangamizwa kwa baa la njaa.
Mimi ni miongoni mwa wale waumini wa falsafa ya maendeleo ya Mwalimu Nyerere, aliyoiandika kwenye kitabu chake cha “Binadamu na Maendeleo”, kuwa ili tuendelee, tunahitaji vitu vine, Watu, Ardhi, Siasa Safi na Uongozi Bora, “fedha si msingi, fedha ni matokeo tuu”. Sisi Tanzania, toka ile tunapata uhuru, miaka ya 60, vitu hivyo vyote vine tunavyo, jee tunakwama wapi?.
Japo mimi sio mchumi, ila kwa maoni yangu, Tanzania tunakwama kwenye kupanga vipaumbele vyetu.
Kwa muda mrefu nchi wafadhili, mashirika fadhili, nay a misaada ya kimataifa, ndio yanatupangia vipaumbele vyetu watakavyo fadhili, hivyo kupata misaada ya kimaendeleo na mikopo yenye masharti.
Kwa vile sisi watu wa media, sio wachumi, kazi yetu ni kusikiliza tuu wachumi na wakubwa wakipanga, na sisi kazi yetu ni kuripoti, kuandika kilichosemwa na wakubwa hawa, hivyo kujikuta, hatulisaidii taifa.
Mimi naamini kabisa kwa dhani ya moyo wangu kuwa Rais Samia, ana nia ya dhati, ya kulisaidia Taifa, lakini ili afanikiwe, ni lazima asaidiwe kuelezwa ukweli maeneo yenye udhaifu, yaliyotukwamisha, ni eneo la upangaji vipaumbele vyetu, moja ya maeneo hayo ni eneo nishati, kiukweli kabisa, licha ya Tanzania kugundua gesi asili, kuwa na maporomoko ya Mto Rufiji, tuna jua la kutosha kuzalisha solar energy, tunaupepo wa kutosha kufunga windmills, na chini ya ardhi tuna geothermal ya kutosha kuzalisha umeme, mpaka sasa ni nchi kubwa yenye watu milioni 60, lakini umeme wetu ni Megawatt 1,600, ni aibu!.
Japo tuna wataalamu na wataamuna, wachumi waliobobea, wanaopanga vipaumbele vyetu, kiukweli kwenye baadhi ya vipaumbele, wanazidi tuu kumuingiza chaka Mama Samia, namshauri mama Samia, aendelee kuwasikiliza Wataalamu wake wa uchumi, lakini pia asipuuze sauti zetu sisi akina hohehahe, kuna vitu tunaona tunakwenda ndivyo sivyo, tunashauri tunapuuzwa, nashauri pia tusikilizwe, huwezi jua, tunaweza kusaidia. Vipaumbele vikuu vyetu view, 1. Elimu, 2. Kilimo, 3. Afya 4. Nishati, 5. Miundombinu.
Wiki iliyopita katika siku ya Tanzania Day, kwenye Maonyesho ya Expo Dubai 2020, Wizara ya Nishati, pia ilifanya Kongamano la Kimataifa la Uwekezaji kwenye Sekta ya Nishati ambalo lilihutubiwa na Waziri wetu wa Nishati, Mhe. January Makamba.
Hivyo mara tuu baada ya kurejea, nchini, nilimtafuta Mhe. Januari
Makamba amesema “Moja ya Changamoto kubwa sana ya sub sector ya umeme ni uwekezaji usiotosheleza , Nchi yenye ukubwa kama yetu, inayokuwa kwa kasi kama yetu, na ongezeko la idadi ya watu, kuwa na Megawati 1600 ni aibu kubwa, au kuwa na mtandao mdogo wa usafirishaji umeme kama tulionao ni aibu” Amesema “ tumezungumza na wawekezaji wengi, wakubwa wenye uwezo, na nia njema ambao wako tayari kuja nchini kwetu na kuwekeza katika maeneo hayo”
Makamba amesema, kufuatia hali ya nishati nchini kwetu, na fursa zilizopo Tanzania katika umeme, mafuta na gesi, Tanzania imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa ni kitovu cha biashara ya Nishati ukanda huu wa Afrika Mashariki, kati na Kusini”
Makamba amesema, “Tanzania imedhamiria kufanya mapinduzi makubwa ya nishati, kwa kuifanya nishati ya kupikia, kupatikana kwa wingi na kwa urahisi zaidi, kufuatia asilimia 70 ya nishati yote Tanzania, kutumika kwa kupikia, ikifuatiwa na mafuta na umeme. Nishati kubwa inayoongoza kutumika n kupikia, ni nishati ya Tungomotaka (biomass).
Makamba ameusema ukweli mchungu kuwa “Hali ya nishati ya nchini Tanzania, sio nzuri, watu 22,000 wanapoteza maisha, kila mwaka kutokana na magojwa ya upumuaji yanayosababishwa na moshi wa kupikia kwa kuni na mkaa, hivyo kufuatia hali hiyo, kipaumbele cha kwanza kwenye sekta ya nishati, ni kuhakikisha gesi inapatikana kwa urahisi na kwa bei nafuu na inafika kwenye kila nyumba, hivyo kupunguza matumizi ya kuni na mkaa.
Pia Makamba, amezungumzia hali ya nishati ya Umeme nchini sio nzuri, kutokana na ukuaji mkubwa wa uchumi, na ongezeko la idadi ya watu, usiokwenda sambamba na uwekezaji kwenye sekta ya umeme, hivyo kinachofanyika sasa ni kutafuta fedha, za kufanya uwekezaji mkubwa kwenye umeme, kuweza kukidhi mahitaji.
Kwa upande wa Tanesco, Waziri wa Nishati, January Makamba, amesema Tanesco inahitaji transformes mpya zaidi ya 20,000 nchi nchi nzima ili ku stabilize umeme, kuacha kukatika katika mara kwa mara kutokana na transformers zilizopo kuelemewa.
Moja ya kero kubwa kwa Watanzania ni kero ya kukatika katika kwa umeme, Waziri January Makamba amesema, kunachangiwa na ukuaji wa ghafla wa uchumi wa mtu mmoja mmopja, watu wengi zaidi sasa wanatumia vifaa vya umeme ukilinganisha na kule nyuma, hivyo peak demand ya matumizi ya umeme kwa wakati mmoja, kuongezeka maradufu, na kusababisha instability.
Waziri Makamba, amemalizia kwa kuwahakikishia Watanzania, serikali ya awamu ya 6, chini ya Rais Samia, imedhamiria kwa dhati, kukabiliana na changamoto zote zinazoikabili sekta ya nishati, miradi ya kupeleka umeme vijijini, iko pale pale, Tanesco iko kwenye mageuzi makubwa ya kiutendaji kuboresha huduma zake.”
Shida zilizopo tunazijua, changamoto tunazijua, majawa tunayajua, kinachohitaji ni subra na uvumilivu, na baada ya muda sii mrefu, kukatika katika umeme, kutakuwa ni historia”
Hili tatizo la Upangaji wa Vipaumbele Vyetu, litajirudia very soon, baada ya nishati ya kupikia na umeme majumbani nishati muhimu sana ni mafuta ya petrol na dizeli. Kufuatia vita vya Ukraine, mafuta yatapanda tena bei kwenye soko la dunia kama enzi za vita vya ghuba, watu wanaojua kupanga Vipaumbele kupitia kufanya SWOT and PEST Analysis by now tungeishajua mafuta yatapanda sana bei na kuanza kujipanga kwa mitigation steps kabla hayajapanda ili kuzuia kupanda bei, na sio kusubiri yapande, yazue taharuki ndipo msikie vikao vya kukutana ku mitigate, ndipo itolewe ruzuku bei ya mafute ishuke.
Paskali