Drifter
JF-Expert Member
- Jan 4, 2010
- 4,436
- 4,151
Mkuu, hilo ndio tatizo la vijana wa BAVICHA. Unakimbilia kutukana tu kabla hata hujasoma kinachojadiliwa.
Amnesty International wanataka Rais wa Tanzania afute sheria zilizotungwa na Bunge halali la kidemokrasia la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Je, unakubaliana na shinikizo hilo la Shirika hilo binafsi?
Tatizo, sisi Watanzania tunajua na AI wanajua kuwa Bunge la JMT halina uwezo wa kujadili na kukataa kupitisha muswada unaoletwa na serikali hata kama unapingana na Katiba na mikataba ya kimataifa tuliyoridhia. Hivyo, si kila sheria inayopitishwa na Bunge hilo ni halali.
Bunge linashindwa kuonyesha uhuru na uhalali wake kivitendo. Ukweli ni kuwa Rais wa JMT yuko juu ya Bunge: ana uwezo wa kutunga, kutengua na hata kupuuza (ignore) sheria yoyote ya nchi. Bunge linatumika kama muhuri tu kuweka uhalali.