Amani aliyoipigania Nyerere imevurugwa, ila Nina Imani hizi zama zitapita na Tanzania yetu Itarudi Salama na Kusimama tena

Amani aliyoipigania Nyerere imevurugwa, ila Nina Imani hizi zama zitapita na Tanzania yetu Itarudi Salama na Kusimama tena

Mtu Alie Nyikani

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2022
Posts
1,355
Reaction score
3,090
Wakuu kwema?

Leo hii, moyo wa taifa letu unapitia majaribu. Kumekuwa na ongezeko la matukio ya utekaji, mateso na mauaji ya raia hasa wale wanaotoa maoni tofauti au kusimamia haki. Hali hii inaleta hofu, giza, na ukimya wa kulazimishwa.

Matukio haya yameipaka doa nchi yetu ambayo kwa muda mrefu imejulikana kwa amani na utulivu

Lakini pamoja na hayo yote, bado nina imani.

Nina imani kuwa hii si Tanzania ya milele. Nina imani kuwa ukimya huu si ushindi wa uovu. Ninaamini kuwa damu ya wasio na hatia haitapotea bure. Kila tone ni kilio cha haki, na haki huwa haipotei – huchelewa tu. Nina imani kuwa dhuluma haiwezi kushinda milele.

Serikali, kwa upande wake, inapaswa kufanya kazi yake kwa uwazi na kwa haki. Uhalifu hauna rangi ya chama wala dini – wote wanaohusika na utekaji na mauaji lazima wawajibishwe kwa mujibu wa sheria, bila kinga wala kufichwa nyuma ya taasisi. Vyombo vya usalama visitumike kuumiza, bali kulinda.

Ni wajibu wa kila mmoja wetu viongozi wa kisiasa, wanaharakati, waandishi, watu wa dini, vijana, na wazee – kusimama kwa wima na kutetea utu, uhuru, na haki za kila Mtanzania.

Tunaweza kutofautiana kimawazo, lakini tusikubali kutofautiana katika utu. Amani ya kweli haipo kama watu wanateswa kwa maoni yao.

Hizi zama za giza zitapita.
Na Tanzania yetu – ile ya upendo, haki, na sauti za watu – itarudi salama.
Stay Safe
Soka
Mdude
Ally Kibao
 
Hatukuwahi kusikia watu kutekwa, kuuawa au kupotezwa na serikali wakati wa Nyerere, Mwinyi wala Mkpa.

Huu ushetani ulinza kidogo wakati wa Kikwete, ukaota mizizi wakati wa Magufuli, na umekomazwa zaidi na Samia. Walaaniwe mashetani yote yanayohusika na huu ushetani, kuanzia waliowaajiri, wanaowapa maelekezo, wanaoshabikia na kuunga mkono huu ushenzi, na hasa C hama C ha M ashetani kinachowatumia. Ilaaniwe CCM, viongozi wake na machawa yao yanayoshangilia uovu.
 
Hatukuwahi kusikia watu kutekwa, kuuawa au kupotezwa na serikali wakati wa Nyerere, Mwinyi wala Mkpa.
Ulikuwa bado hujazaliwa...
Kwenye kutekwa, muulize Pascal Mayalla, baba yake alifanyiwa nini....
Kwenye kuuwawa, tumia hio tecno kutafuta walikufa kipindi chake ikiwemo wanaharakati wa Msumbiji, alipogundua na wanashirikiana wa wazungu
1750462628332.png
 
Ulikuwa bado hujazaliwa...
Kwenye kutekwa, muulize Pascal Mayalla, baba yake alifanyiwa nini....
Kwenye kuuwawa, tumia hio tecno kutafuta walikufa kipindi chake ikiwemo wanaharakati wa Msumbiji, alipogundua na wanashirikiana wa wazungu
View attachment 3377262

..baba yake Pascal Mayalla aliachishwa kazi toka ktk Idara ya usalama wa taifa na baadaye kushtakiwa kutokana na kashfa ya maafisa usalama kutesa wananchi waliokuwa wakiwahoji ktk mahabusu za serikali. Kashfa hiyo ilitokea wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere.
 
Wakuu kwema?

Leo hii, moyo wa taifa letu unapitia majaribu. Kumekuwa na ongezeko la matukio ya utekaji, mateso na mauaji ya raia hasa wale wanaotoa maoni tofauti au kusimamia haki. Hali hii inaleta hofu, giza, na ukimya wa kulazimishwa.

Matukio haya yameipaka doa nchi yetu ambayo kwa muda mrefu imejulikana kwa amani na utulivu

Lakini pamoja na hayo yote, bado nina imani.

Nina imani kuwa hii si Tanzania ya milele. Nina imani kuwa ukimya huu si ushindi wa uovu. Ninaamini kuwa damu ya wasio na hatia haitapotea bure. Kila tone ni kilio cha haki, na haki huwa haipotei – huchelewa tu. Nina imani kuwa dhuluma haiwezi kushinda milele.

Serikali, kwa upande wake, inapaswa kufanya kazi yake kwa uwazi na kwa haki. Uhalifu hauna rangi ya chama wala dini – wote wanaohusika na utekaji na mauaji lazima wawajibishwe kwa mujibu wa sheria, bila kinga wala kufichwa nyuma ya taasisi. Vyombo vya usalama visitumike kuumiza, bali kulinda.

Ni wajibu wa kila mmoja wetu viongozi wa kisiasa, wanaharakati, waandishi, watu wa dini, vijana, na wazee – kusimama kwa wima na kutetea utu, uhuru, na haki za kila Mtanzania.

Tunaweza kutofautiana kimawazo, lakini tusikubali kutofautiana katika utu. Amani ya kweli haipo kama watu wanateswa kwa maoni yao.

Hizi zama za giza zitapita.
Na Tanzania yetu – ile ya upendo, haki, na sauti za watu – itarudi salama.
Stay Safe
Soka
Mdude
Ally Kibao
Bado unaendelea kunywa gongo? Nilikushauri uache tangu uanze kulala mitaroni
 
Hatukuwahi kusikia watu kutekwa, kuuawa au kupotezwa na serikali wakati wa Nyerere, Mwinyi wala Mkpa.

Huu ushetani ulinza kidogo wakati wa Kikwete, ukaota mizizi wakati wa Magufuli, na umekomazwa zaidi na Samia. Walaaniwe mashetani yote yanayohusika na huu ushetani, kuanzia waliowaajiri, wanaowapa maelekezo, wanaoshabikia na kuunga mkono huu ushenzi, na hasa C hama C ha M ashetani kinachowatumia. Ilaaniwe CCM, viongozi wake na machawa yao yanayoshangilia uovu.
Duuuh

Enzi za mwalimu we couldn’t even question the government wala watu wa serikali

Vijana hamkuwepo

Hii freedom ya kutukana ya leo would never even be thought of enzi zile
 
Tunaweza kutofautiana kimawazo, lakini tusikubali kutofautiana katika utu. Amani ya kweli haipo kama watu wanateswa kwa maoni yao.
Ni mtu mwenye upungufu mkubwa sana anayweza kuikatia tamaa nchi kama Tanzania. Upuuzi huu wa sasa utakomeshwa na Tanzania yenye heshima itasimama miongoni mwa mataifa.

Mkuu, 'Mtu aliye Nyikani', wewe umezungumzia sehemu moja tu ya maovu wanayofanyiwa waTanzania kuhusu utekaji, kuuliwa, n.k..
Uovu hauishii hapo. WaTanzania kunyanyaswa ndani ya nchi yao, na kuporwa raslimali zao; kutwezwa utu wao na heshima yao ni uhalifu mkubwa zaidi, kama unaotumika kuvuruga akili zao wajine wao kuwa binaadam duni miongoni mwa binaadam wengine.
Mambo haya huwezi kuyaona kwa muda mfupi; matokeo yake ni ya muda mrefu

Lililopo ni kukomesha utawala huu wa kishetani ambao haujawahi kuonekana ndani ya nchi hii. Naamini Samia Suluhu Hassan na Genge lake watakomeshwa tu na waTanzania wenyewe.
 
Duuuh

Enzi za mwalimu we couldn’t even question the government wala watu wa serikali

Vijana hamkuwepo

Hii freedom ya kutukana ya leo would never even be thought of enzi zile
Wewe bila shaka utakuwa ni mmoja wa wahitimu wa Chuo Kikuu cha Kariakoo; kwa mzee Mohamed Said.
Huu utekaji na uuaji uliuona wakati huo kama ulivyo sasa? Si ulimwona waziri mzima, Mwinyi akiachia ngazi, au hukuona, na hata kusimuliwa tu?
'Hii freedom...."? 'Freedom gani ya kuua watu, au kuwateka na kuwapoteza?

Chama cha CCM kilichoundwa kwa uangalifu mkubwa sana, sasa ndicho mmekivamia na kukifanya kuwa kichaka chenu cha kuwafanyiaa maovu waTanzania; halafu leo unakuja hapa na kubwabwaja kuhusu Enzi za mwalimu...," na kujifanya mjuaji kumbe hujui lolote.
Lililo wazi ni kwamba, aliyoyazuia Mwalimu wakati wake, sasa ndiyo mnayatekeleza, kwa kukigeuza chama kuwa msitu wa kufanyia uhalifu!
 
..baba yake Pascal Mayalla aliachishwa kazi toka ktk Idara ya usalama wa taifa na baadaye kushtakiwa kutokana na kashfa ya maafisa usalama kutesa wananchi waliokuwa wakiwahoji ktk mahabusu za serikali. Kashfa hiyo ilitokea wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere.
Na Mwinyi, Waziri wa Mambo ya ndani kuachia ngazi sawia (kuwajibika). Leo hii ni nani anawajibika wala hata kuwajibishwa?
 
Wewe bila shaka utakuwa ni mmoja wa wahitimu wa Chuo Kikuu cha Kariakoo; kwa mzee Mohamed Said.
Huu utekaji na uuaji uliuona wakati huo kama ulivyo sasa? Si ulimwona waziri mzima, Mwinyi akiachia ngazi, au hukuona, na hata kusimuliwa tu?
'Hii freedom...."? 'Freedom gani ya kuua watu, au kuwateka na kuwapoteza?

Chama cha CCM kilichoundwa kwa uangalifu mkubwa sana, sasa ndicho mmekivamia na kukifanya kuwa kichaka chenu cha kuwafanyiaa maovu waTanzania; halafu leo unakuja hapa na kubwabwaja kuhusu Enzi za mwalimu...," na kujifanya mjuaji kumbe hujui lolote.
Lililo wazi ni kwamba, aliyoyazuia Mwalimu wakati wake, sasa ndiyo mnayatekeleza, kwa kukigeuza chama kuwa msitu wa kufanyia uhalifu!
We didn’t have social media dogo

Na kuhusu uhitimu usitie shaka, sisi ni udsm products zilizokua serious… sio Hutu tutoto twa cuhas na makumira
 
Wakuu kwema?.

Serikali, kwa upande wake, inapaswa kufanya kazi yake kwa uwazi na kwa haki. Uhalifu hauna rangi ya chama wala dini – wote wanaohusika na utekaji na mauaji lazima wawajibishwe kwa mujibu wa sheria, bila kinga wala kufichwa nyuma ya taasisi. Vyombo vya usalama visitumike kuumiza, bali kulinda.
Naunga mkono hoja
P
 
Back
Top Bottom