Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Siku hizi sina raha, na mke wangu nyumbani
Nirudipo kazini humkuta, kajiinamia
Nauliza vipi mke wangu, mbona umekasirika, hushindwa kunijibu hubakli anaalia
Nazidi kumbembeleza sana sana mke wangu ee, mwisho naye kaamua kunielezeaaa
Eti anafahamu mambo yangu yotee, nifanyayo nikiwa kaziniii
Eti nina wanawake wengi sana mie, hivyo basi anataka tutenganeee
Namfikiria ampaye maneno mke wanguu, nami sitokubalii namsaka mbea huyooo
Jamani……………
Rudia mwanzo……………………………
Ama zake eee ama zangu, ole wake akae akijua labda nismtambueee……
Naelewa nia yake ni kutaka kunigombanisha,imekuwa sikai na kufurahi mimi na mke wanguuu
Mtu huyoo adui yangu, kanitafuta kwa siku nyingi naona amenipataaa
Naelewa nia yake ni kutaka kunigombanisha,imekuwa sikai na kufurahi mimi na mke wanguuu
Ama zake eee ama zangu, ole wake akae akijua labda nismtambueee……
Mtu huyoo adui yangu, kanitafuta kwa siku nyingi naona amenipataaa
Hao wanaitwa DDC Mlimani Park Sikinde……………..