Jamani Xspin wangu mie sijui nisemeje.....innalillahi wa inna illahi rajiun.
Mwenyezi mungu awafariji wote wafiwa, Loh! kweli majaaliwa huwezi jua kesho itakuwaje. Poleni sana.
Yaa! Mama alikuwa kwenye gari ndogo iliyokuwa nyuma ya coaster iliyopata ajali. So alishuhudia ajali ile kwa macho. Sasa mambo ya mshtuko hakuwa na jinsi zaidi ya ku-colapse.
Pole sana kaka. Tell ur friend, to count his blessings and he will be surprised to see what God has already done for him. E.g. hadi age hii bado alikuwa na wazazi wote wawili etc.
May God give him the courage to go on.
Bwana ametoa na bwana ametwaa, jina la bwana lihimidiwe
Pole sana Chrispin....kusema kweli wote tupo kwenye huu msiba mzito ambao umetugusa kwa namna ya pekee
Lakini kwa Mungu kuna msamaha...ili yeye aogopwe na aitwe Mungu
Tuwaombee wafiwa wote jamani!
Hebu fikiria:
Una rafiki yako mpendwa, mliyeshibana sana. Mmesoma darasa moja toka A-Level mpaka chuo kimoja. Bahati ikawanyookea mkapata kazi kampuni moja, kabla ya rafiki yako mwezi mmoja uliopita kupata kazi sehemu nyingine.
Na urafiki wenu huu ukapelekea na familia zenu kufahamiana na kuheshimiana sana.Mkawa mnashirikiana katika shida na raha.
Halafu ghafla asubuhi unapata simu ya rafiki yako. Kama kawaida unaipokea kwa utani lakini sauti ya rafiki yako kwenye simu si ya kawaida. Ana majonzi na sauti imekuwa nzito. Anakuuliza: umesikia ile ajali ya Same? unamwambia umeisikia. Then anamalizia kwa kusema: Ajali ile imemaliza familia yangu yote!
Ndicho kilichonifanya kuwa speechless kwa leo nisijue la kufanya. Nimechanganyikiwa nimsaidieje huyu rafiki yangu!
Please pray for his Dady, Sister, Brother and other 16 close relatives to Rest in Peace.
Dah mm mwenyewe hapa nimeishiwa nguvu kabisa sijui nipihe Valuu akili ije? maana sielewi la kufanya.
any way mpwa pole sana kwa tukio hili tupo pamoja kwa sala