Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela amesema alipigiwa simu na mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Dniale Chongolo na akamjulisha kuhusu mtu aliyetoroka karantini
Mtu huyo baada ya kutoroka Dar alionekana yuko Iringa, uongozi wa wilaya walishirikiana na jeshi la polishi kujua anapokaa mtu huyo na wamempeleka kantini
Mtu huyo inasemekana alitoka Norway, na ana siku nne tangu aingie hapa Tanzania. Alikaa karantini siku tatu na kuamua kutoroka
Nyumba aliyokaa pia iko chini ya karantini na mganga mkuu wa wilaya atawapima wote wanaoishi katika nyumba hiyo
Kasesela amesema kuna mwingine wiki iliyopita alitoroka karantini ya Tunduma na hadi sasa hawajui yuko wapi, lakini mtu huyo alikuwa mmalawi
Sent using
Jamii Forums mobile app