wiseboy.
JF-Expert Member
- Aug 11, 2014
- 2,931
- 4,549
Wakuu, mimi kijana wa Kanda ya Ziwa nipo hapa Dar kwa takriban wiki ya pili sasa. Leo katika kuzungukazunguka yangu usiku huu wakati narejea kulala majira ya saa mbili hivi nimeokota pochi yenye kiasi kikubwa hivi cha pesa pamoja na driving license maeneo ya ilala katika flat za wanajeshi kwenye njia inayochepukia kuelekea Kigogo.
Kwanza nimewaza sana iwapo hii ni bahati au lah! Nikajiuliza mara mbili mbili, baadae moyo ukaniambia kuwa mwenye huo mzigo yawezekana nae ana matatizo yake na hiyo pesa ndo alikuwa anaitegemea sana, kwa kuwa mimi kidogo nipo vizuri kiuchumi nimeona ni bora nitangaze, kwa yeyote aliyepoteza aniPM na aeleze jina lake kama lilivyo kwenye license na aseme kiasi halisi cha pesa, kisha tuonane nimpatie mzigo wake.
Warning: Kama huhusiki tafadhali pita sitaki usumbufu wala kejeli, heshima ni kitu cha bure.
Kwanza nimewaza sana iwapo hii ni bahati au lah! Nikajiuliza mara mbili mbili, baadae moyo ukaniambia kuwa mwenye huo mzigo yawezekana nae ana matatizo yake na hiyo pesa ndo alikuwa anaitegemea sana, kwa kuwa mimi kidogo nipo vizuri kiuchumi nimeona ni bora nitangaze, kwa yeyote aliyepoteza aniPM na aeleze jina lake kama lilivyo kwenye license na aseme kiasi halisi cha pesa, kisha tuonane nimpatie mzigo wake.
Warning: Kama huhusiki tafadhali pita sitaki usumbufu wala kejeli, heshima ni kitu cha bure.