Hatimaye aliyemmiminia risasi 21 Erasto akamatwa ni mtu wake wa karibu sana na alishawahi fungwa miaka sita kwa ujambazi.
Watu waliomuua mfanyabiashara wa madini Erasto wamekamatwa. Watu hao ni mfanyabiashara mwenzake ambaye anaitwa Sharifu na watu wengine watatu. Inasemekana huyu sharifu ndiye aliyeratibu mauaji hayo kwa kusajili laini mbili za simu ambazo zilitumika kumuweka marehemu kwenye mtego wa kumuua. Alimrubuni mmasai mmoja ambaye ndie aliyesajili laini hizo kwa kitambulisho chake. Baada ya wana usalama kufuatlia mawasiliano ndipo yule masai alipokamatwa na baada ya mahojiano alijieleza kuwa sharifu alimwomba amsajilie lain kwa kitambulisho chake kwani yeye hakuwa na kitambulisho. Sharifu alinunua pikipiki mbili ambazo zilitumika kutekeleza mauaji. Sababu kubwa ya mauji haya ni ugomvi wa kugombania wachimbaji wadogo ambao mara nyingi huzama kwenye mgodi wa Tanzanite one na kuiba madini na hatimae kumuuzia Erasto na Sharif. Source- mtaani Mererani.