Aliyemtapeli Imamu simu, kusomewa Dua Maalum

Hivi yule alikatiwa mikarafuu yake kule pemba na kutoa muda wahusika kujisalimisha kabla kusomewa albadili amefikia wapi au anasubiri mwezi mtukufu uishe. Au ndy mikwara maana mrema alisomewa albadili za kutosha lkn hatukuona kitu.
Hahahahaha


Noumaaaaaa sana.
 
Tapeli maarufu ambaye ameutumia mwezi Mtukufu wa Ramadhani kutapeli kwenye misikiti mbalimbali kwa minajili ya kufuturisha sasa anaandaliwa dua maalum kwa mujibu wa Imam wa Msikiti mmoja huko Temeke DSM aliyekua akihojiwa na Clouds nami kumsikia LIVE

Tapeli huyo alifika kwa imamu akiwa na toyo na kumwambia amekuja hapo kwa nia ya kufuturisha na akamwomba wanawake wawili wa kupika, alipoondoka nao kama anakwenda sokoni akawapiga simu kisha kurudi kwa imamu naye akampiga simu kwa kumwambia anataka aongee na mtu wa kumtumia fedha na kutokomea nayo kumbe alimfuata wa toyo na kumtapeli pia simu yake.

Yasemekana ameshafanya hivi huko Mbagala na kwingineko
dini yake inamruhusu kumsomea dua mbaya mtu mwngne?
 
Kuna ustaadh mmoja tanga jina limenitoka aliibiwa nazi shambani kwake akawaomba walioiba wazirudishe hawakuskia!
Akapiga AL BADIRI wale waloiba walikufa walionunua na kuzitumia majumbani pia waliathirika unaambiwa hadi punda alievuta mkokoteni uliobeba nazi alikufa kifo kibaya sana!
Danganya toto
 
Kwani simu yenyewe ya IMAM ni aina gani???

usikute ni nokia tu ya tochi mnataka kumpoteza mtu!!
 
Tapeli maarufu ambaye ameutumia mwezi Mtukufu wa Ramadhani kutapeli kwenye misikiti mbalimbali kwa minajili ya kufuturisha sasa anaandaliwa dua maalum kwa mujibu wa Imam wa Msikiti mmoja huko Temeke DSM aliyekua akihojiwa na Clouds nami kumsikia LIVE

Tapeli huyo alifika kwa imamu akiwa na toyo na kumwambia amekuja hapo kwa nia ya kufuturisha na akamwomba wanawake wawili wa kupika, alipoondoka nao kama anakwenda sokoni akawapiga simu kisha kurudi kwa imamu naye akampiga simu kwa kumwambia anataka aongee na mtu wa kumtumia fedha na kutokomea nayo kumbe alimfuata wa toyo na kumtapeli pia simu yake.

Yasemekana ameshafanya hivi huko Mbagala na kwingineko
Yes Mbagala nilimshitukia nikakataa kumpa mchele na vitu vingine alivyokuwa anavitaka kuwa eti hela inatumwa kwa Mpesa! Nikamwambia subiri mpaka hela ije!
 
Jamaa waliofyeka mikarafuu ya waziri bado wanadunfa mtaani au wamekufa?
 
Back
Top Bottom