JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,309
- 5,464
Rushyna amesema kama unaona haupati amani sehemu using’ang’anie, mtangulize Mungu mbele kisha endelea kupambana.
SWALI: Uliwahi kukosa amani katika ndoa yako?
JIBU: Somehow
Umewahi kupitia vipigo katika ndoa yako?
JIBU: Kawaida
Unajutia kuoana na Manara
JIBU: 50-50
Umepewa talaka ngapi na Manara?
JIBU: Moja
Hiyo ina maanisha anaweza kurejea kwako?
JIBU: No, kwa sababu hata kuachana kwetu hatukuachana kisheria, ningefuata sheria inamaanisha ningekuwa kwenye eda.
Kwa nini haujadai talaka zote ili uwe huru?
JIBU: Sihitaji hata hiyo ndoa kwa sasa
Una uhusiano na mtu kwa sasa?
JIBU: 50-50
Ni kweli kuwa ulifuata hela kwa Haji Manara?
JIBU: Kwani Haji ana hela? Hana pesa, ana pesa ya kawaida
Haji alikupa kazi kama msaidizi wake, unaendelea na hiyo kazi?
JIBU: HAPANA
Siku ya birthday yake alikupost kisha akafuta, ilikukwaza?
JIBU: Huwa sikwazikagi na mambo ya kijinga
Kuna mtu au watu wamejaribu kuwapatanisha?
JIBU: Nikiamua kitu change siwezi kushauriwa, nikisema nimechoka basi ujue nimechoka
Ukaribu wako na Harmonie upoje?
JIBU: Ni rafiki tu, nina marafiki wengi maarufu, ninawapost pale ninapojisikia
Watu wanasema wewe haujatulia na wewe ndio una matatizo na haukuwa unamsikiliza mume?
JIBU: Siyo kweli, yanayozungumzwa kuhusu mimi ni stori za kutungwa, sitetereki kujibu kwa kuwa habari zote ni za uwongo. Suala la kutulia kila mtu ana muono wake, huwezi kumridhisha kila mtu.
Ni kweli ulimnyima Haji perfume?
JIBU: Kwanza hilo jambo hata ukilisikia unaona halina maana
Ni kweli utarudi Shinyanga?
JIBU: Nitarudi (anacheka)