McCollum
JF-Expert Member
- Jan 10, 2023
- 384
- 679
Habari za Jumapili?
Naomba niende moja kwa mona kwenye mada, hiko hivi, kuna kijana ambaye ametokea mkoa mmoja huko Kanda ya Kaskazini, huyu hakuwa na wazazi wote wawili kwani walifariki kipindi alipokuwa mdogo sana. Kwa kipindi kirefu cha Elimu yake alikuwa akiishi na bibi upande wa mama (kuanzia alipoanza darasa la kwanza mpaka alipohitimu kidato cha nne).
Ndugu upande wa baba na mama yake walikuwa wakiishi mbali na mkoa aliokuwa akiishi kijana huyu (Tumuite Dan, hili ni jina la kubuni). Baada ya kumaliza kidato cha nne matokeo yalitoka na Dan alikuwa amefaulu kwa daraja la tatu la mwanzoni. Shida ilikuja kwenye gharama za kumsomeshea A-level, bibi angepata wapi pesa? Hakukuwa na mahala pakupata pesa hizo, baadhi ya wasamaria wema wa mawazo walimahauri kijana Dan amfuate mkuu wa wilaya na kumuomba msaada.
Dan alilichukua lile wazo na kulifanyia kazi, mkuu wa wilaya aliguswa na namna ambavyo Dan alikuwa akiipambania Elimu licha ya kuwa katika mazingira magumu na akaahidi kumsaidia. Ulipofika muda muafaka wa kuanza shuld Dan alikabidhiwa mahitaji ya shule ambayo yalihusisha uniform, madaftari, pesa ya kujikimu lakini upande wa ada yule mkuu wa wilaya alifanya malipo kabla na kumkabidhi Dan pay slip. Sikwamba mkuu wa wilaya alikuwa akitoa pesa zote peke yake, la hasha, mkuu wa wilaya ali"organize" wadau ambao walikuwa wakisaidia kuwasomesha vijana ambao hawakuwa na msaada wowote kutoka kwa ndugu zao (ingawa hawakuwa wengi).
Dan aliingia Advance na alichagua mchepuo wa HGL, na huko baada ya kufanya mtihani wa taifa-NECTA ya kidato cha sita (ACSEE) alipata division two, baada ya kurejea kijijini lwa bibi yake alianza kujiandaa kufanya application za chuo, muda huu Dan alikuwa akijihusisha na kazi ndogo ndogo za kusukuma siku na kumsaidia bibi yake ambaye alikuwa akipata msaada mdogo kutoka kwa ndugu na mara nyingi alikuwa akisaidiwa na majirani ambao waliguswa na maisha yake duni.
Hata yalipotoka majina ya vijana waliochaguliwa kujiunga jeshi jina la Dan halikuwepo, hii ilimpa muda kukaa na bibi yake ambaye ndiye aliyekuwa mama, baba, shangazi, mjomba na ndugu zake wa karibu. Dan alikuwa akisikia tu kutoka kwa bibi zake kwamba kuna baadhi ya ndugu zake ambao walikuwa maeneo ya Ukerewe na walikuwa wakijiweza kiuchumi lakini hakuwahi mwambia kwanini ndugu hao waliamua kuwatupa kiasi hicho na kuwaacha wakijipaka matope ya ufukara wa hali ya juu.
SEHEMU YA PILI
SEHEMU YA TATU
Naomba niende moja kwa mona kwenye mada, hiko hivi, kuna kijana ambaye ametokea mkoa mmoja huko Kanda ya Kaskazini, huyu hakuwa na wazazi wote wawili kwani walifariki kipindi alipokuwa mdogo sana. Kwa kipindi kirefu cha Elimu yake alikuwa akiishi na bibi upande wa mama (kuanzia alipoanza darasa la kwanza mpaka alipohitimu kidato cha nne).
Ndugu upande wa baba na mama yake walikuwa wakiishi mbali na mkoa aliokuwa akiishi kijana huyu (Tumuite Dan, hili ni jina la kubuni). Baada ya kumaliza kidato cha nne matokeo yalitoka na Dan alikuwa amefaulu kwa daraja la tatu la mwanzoni. Shida ilikuja kwenye gharama za kumsomeshea A-level, bibi angepata wapi pesa? Hakukuwa na mahala pakupata pesa hizo, baadhi ya wasamaria wema wa mawazo walimahauri kijana Dan amfuate mkuu wa wilaya na kumuomba msaada.
Dan alilichukua lile wazo na kulifanyia kazi, mkuu wa wilaya aliguswa na namna ambavyo Dan alikuwa akiipambania Elimu licha ya kuwa katika mazingira magumu na akaahidi kumsaidia. Ulipofika muda muafaka wa kuanza shuld Dan alikabidhiwa mahitaji ya shule ambayo yalihusisha uniform, madaftari, pesa ya kujikimu lakini upande wa ada yule mkuu wa wilaya alifanya malipo kabla na kumkabidhi Dan pay slip. Sikwamba mkuu wa wilaya alikuwa akitoa pesa zote peke yake, la hasha, mkuu wa wilaya ali"organize" wadau ambao walikuwa wakisaidia kuwasomesha vijana ambao hawakuwa na msaada wowote kutoka kwa ndugu zao (ingawa hawakuwa wengi).
Dan aliingia Advance na alichagua mchepuo wa HGL, na huko baada ya kufanya mtihani wa taifa-NECTA ya kidato cha sita (ACSEE) alipata division two, baada ya kurejea kijijini lwa bibi yake alianza kujiandaa kufanya application za chuo, muda huu Dan alikuwa akijihusisha na kazi ndogo ndogo za kusukuma siku na kumsaidia bibi yake ambaye alikuwa akipata msaada mdogo kutoka kwa ndugu na mara nyingi alikuwa akisaidiwa na majirani ambao waliguswa na maisha yake duni.
Hata yalipotoka majina ya vijana waliochaguliwa kujiunga jeshi jina la Dan halikuwepo, hii ilimpa muda kukaa na bibi yake ambaye ndiye aliyekuwa mama, baba, shangazi, mjomba na ndugu zake wa karibu. Dan alikuwa akisikia tu kutoka kwa bibi zake kwamba kuna baadhi ya ndugu zake ambao walikuwa maeneo ya Ukerewe na walikuwa wakijiweza kiuchumi lakini hakuwahi mwambia kwanini ndugu hao waliamua kuwatupa kiasi hicho na kuwaacha wakijipaka matope ya ufukara wa hali ya juu.
SEHEMU YA PILI
SEHEMU YA TATU