Smart AJ
JF-Expert Member
- Mar 21, 2022
- 5,540
- 5,752
PART 1
MICHEPUKO YA MUME WANGU NI NDUGU ZAKE WA DAMU
Zamani nilikuwa nikisikia mtu anasema Ndoa sio ya kukimbilia au mwingine akisema ndoa sio kitu cha mchezo nilikuwa naona kama wananionea wivu. Kabla sijaolewa Shangazi yangu aliniambia hakikisha kabla hujaingia kwenye ndoa umemjua huyo Mwanaume anaekuoa vizuri yeye pamoja na familia yake. Hakikisha unawajua ni watu wa aina gani na wanaishije. Kiukweli nilimsikiliza Shangazi na kumuitikia kana kwamba nilifanyia kazi kile alichonishauri lakini haikuwa hivyo. Akili yangu yote ilikuwa kwenye Ndoa, nifunge ndoa nipendeze siku ya harusi tufurahi na kushangilia.
Nilifunga Ndoa na Mume wangu Fabian mwaka 2021, kweli tulikuwa tunapendana sana na wote tulikuwa na hamu ya kuoana na kuishi pamoja. Mume wangu hakuwa Mtu wa starehe wala wanawake. Kipindi chote cha uchumba kama hayuko na Mimi au hayuko kazini basi atakuwa pamoja na ndugu zake kwani aliniambia kuwa familia yake ni familia yenye umoja ambayo Ndugu huwa wanapanga siku za kutoka na kukaa pamoja. Hivyo hata tulivyoowana kuna muda huwa anatoka na kurudi usiku sana na maranyingine asubuhi kwani anakuwa yupo na Ndugu zake na sikuwa na tatizo na hilo.
Nakumbuka siku yangu ya Mahari familia ya Fabian ilikuja kwetu, walikuja Ndugu zake wengi wakiwemo wadogo zake watoto Shangazi, Mama wakubwa na wadogo. Ila kitu cha kushangaza ni kwamba ulipofika muda wa pete, mmoja wa mabinti ambaye ni Mtoto wa Mama yake Mdogo alianza kulia akatoka nje. Ndugu zangu waliniuliza yule ni nani na mbona alikuwa analia wakati unavalishwa Pete nikawaambia ni Dada yake Fabian Mtoto wa Mama Mdogo, wakasema sasa kwanini alie vile. Nikanyamaza sikuwa na majibu nikajua labda anadeka tu.
Chakushangaza hata Siku ya Harusi, wale mabinti ambao ni ndugu zake hawakuwa na furaha kabisaaa, walikuwa wamenuna tofauti na nilivyotarajia. Nikajiuliza sana maswali, ila nikahisi hawanipendi labda walitaka kaka yao aoe Mwanamke mwingine na sio Mimi. Baada ya harusi nilimuhadithia rafiki yangu akasema wakwe ndivyo walivyo, unatakiwa uwazoee tu, mradi ushaolewa wavumilie tu. Kwasasa wapotezee mbeleni watakuelewa na mtaishi vizuri tu. Basi nikatulia hofu ikapungua.
ITAENDELEA PART 2
MICHEPUKO YA MUME WANGU NI NDUGU ZAKE WA DAMU
Zamani nilikuwa nikisikia mtu anasema Ndoa sio ya kukimbilia au mwingine akisema ndoa sio kitu cha mchezo nilikuwa naona kama wananionea wivu. Kabla sijaolewa Shangazi yangu aliniambia hakikisha kabla hujaingia kwenye ndoa umemjua huyo Mwanaume anaekuoa vizuri yeye pamoja na familia yake. Hakikisha unawajua ni watu wa aina gani na wanaishije. Kiukweli nilimsikiliza Shangazi na kumuitikia kana kwamba nilifanyia kazi kile alichonishauri lakini haikuwa hivyo. Akili yangu yote ilikuwa kwenye Ndoa, nifunge ndoa nipendeze siku ya harusi tufurahi na kushangilia.
Nilifunga Ndoa na Mume wangu Fabian mwaka 2021, kweli tulikuwa tunapendana sana na wote tulikuwa na hamu ya kuoana na kuishi pamoja. Mume wangu hakuwa Mtu wa starehe wala wanawake. Kipindi chote cha uchumba kama hayuko na Mimi au hayuko kazini basi atakuwa pamoja na ndugu zake kwani aliniambia kuwa familia yake ni familia yenye umoja ambayo Ndugu huwa wanapanga siku za kutoka na kukaa pamoja. Hivyo hata tulivyoowana kuna muda huwa anatoka na kurudi usiku sana na maranyingine asubuhi kwani anakuwa yupo na Ndugu zake na sikuwa na tatizo na hilo.
Nakumbuka siku yangu ya Mahari familia ya Fabian ilikuja kwetu, walikuja Ndugu zake wengi wakiwemo wadogo zake watoto Shangazi, Mama wakubwa na wadogo. Ila kitu cha kushangaza ni kwamba ulipofika muda wa pete, mmoja wa mabinti ambaye ni Mtoto wa Mama yake Mdogo alianza kulia akatoka nje. Ndugu zangu waliniuliza yule ni nani na mbona alikuwa analia wakati unavalishwa Pete nikawaambia ni Dada yake Fabian Mtoto wa Mama Mdogo, wakasema sasa kwanini alie vile. Nikanyamaza sikuwa na majibu nikajua labda anadeka tu.
Chakushangaza hata Siku ya Harusi, wale mabinti ambao ni ndugu zake hawakuwa na furaha kabisaaa, walikuwa wamenuna tofauti na nilivyotarajia. Nikajiuliza sana maswali, ila nikahisi hawanipendi labda walitaka kaka yao aoe Mwanamke mwingine na sio Mimi. Baada ya harusi nilimuhadithia rafiki yangu akasema wakwe ndivyo walivyo, unatakiwa uwazoee tu, mradi ushaolewa wavumilie tu. Kwasasa wapotezee mbeleni watakuelewa na mtaishi vizuri tu. Basi nikatulia hofu ikapungua.
ITAENDELEA PART 2