Naamin hamjambo na
mnaendelea vzr na kutusaidia ushaur sisi wenye matatz ya hapa na pale.
ni miezi minne imepita toka nimchukuwe mdogo wangu (mtoto wa baba mdogo)
kijijini baada ya yeye kufeli form four na kuzalisha mtoto nikaona
nimchukue nije nae mjini kwenye biashara yetu angalau apate pesa za
maziwa ya mtoto
basi tumeishi vizuri siku zote na juz ndiyo akaniaga anataka arudi
nyumbani akamuone mwanae,nikamwambia hakuna tatizo jiandae nkamwandalia
pesa za safari vzr bas akaondoka jana.
baada ya kuondoka mume wangu akaniweka kwa mazungumzo nanukuu( mdogo
wako kanieleza mambo ya kusikitisha umekuwa na mazoea mabaya na wanaume
pale kwenye biashara wengne wanakuja kila siku,wengne wanaenda china
wanakuletea zawadi unanidhalilidha,umekuwa malaya kwa kuzoeana na
wanaume lukuki pale kazini na maneno meng sana)
Ukweli n kuwa hayo aliyoeleza mengne ni kweli nimezoeana na hao watu ni
wateja wetu wazuri lakn hakuna cha zaidi hata huyu mdogo wangu anaelewa
ukweli kwani muda wote nipo nae kazini.
nimemweleza mama yangu hajaamini kashangaa sana yani.
nafikiria najiuliza au huyu mdogo wangu alitumwa na mama yake kuja
kuniharibia ndoa au ni kipi nilichomkosea au kosa langu kumsaidia had
sasa amekuwa nae mtu anaonekana?au. ni kipi bado sielewi
mpaka sasa mume wangu ana kinyongo,
Huyo mdogo wangu cjamuuliza kitu chochote
nafikiria nimwambie neno gani ajue jinsi amenikosea au ninyamaze?
nishaurini wapendwa nifanye nini?
Wakisha ingia mjini ndio shida!wanajifanya wanajuaa sana!huna sababu ya kunyamaza mweleze ajue kosa lake ila asirudi tena hapo nyumbani!jitahidi kutengeneza kwa hubby mara nyingi kwenye ukweli uongo hujitenga!pole mwaya