Alichokisema Lissu juu ya kesi ya Wema

Alichokisema Lissu juu ya kesi ya Wema

Makonda are serious??? Hii vita kweli ni ya DAWA za kulevya??
Tafadhari anaejua kidonge cha panadol ni gram ngapi atuambie.1.08g za bangi??? Makonda kweli kaka yangu upo serious?? Kweli MBAWA akitaka kufa uharubika pua kwanza.Jamani msokoto wa bangi unatengenezwa na 1.08g kweli ???????
Makonda na kaka yako mtukufu Mungu anawaona.
 
Naona wanachadema busy na yasiyosaidia wananchi au kuwaletea maendeleo.
So far umewasaidiaje hao Wananchi wewe na CCM yako? CHADEMA inawapa wananchi Elimu ya SHERIA bure, nyie kaeni na ukilaza wenu na ubabe maandazi!
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Naanza kukosa imani na utendaji wa cdm Mh lissu nenda mkaunganishe nguvu arusha kwenye kesi ya lema
 
Lijualikali in prison, big brain at work. Seleman Mathew in prison, big brain at work. Godbless Lema in prison, big brain at work!
Utakuwa unapumuliwa kisogoni. Hao uliowataja wote wana Mawakili wao, na Lema hayuko Prison, yuko Mahabusu! CCM Ni mjumuiko WA VI.laza!
 
Huwezi kujivunia kushinda kesi kwa kutumia 'teknikalitizi' za kimahakama. Jivunie kesi kwa kumtetea mdai ama mdaiwa kulingana na hali halisi ya tukio zima. Usitumie mbinu ovu kuvuruga haki ya mdai. Stivu, kadhibitisha anavuta...wameenda usiku wamekuta 'msuba' wewe unasema ameonewa....!!! ndiyo maana mukulu kulu anataka nanyi mfungwe nao hao wahalifu!
Hayo yanawezekana tuu kwenye Mahakama za Chato na Monkey Republic! Sio kwenye hii Tz ya Watz! Hii sii Mali ya mtu binafsi!
 
Naona wanachadema busy na yasiyosaidia wananchi au kuwaletea maendeleo.
kiukweli hii semozi inapooza, ina maana kumsaidia wema iwe haki kwake sio mambo ya kuwasaidia wananchi ama unafikiri singida kuna watz na wakimbizi !!!... kwa taarifa yako Arusha alikamtwa Askari mbambikiziaji ili tangazwa ulisikia na Tundu kuonesha hali kama hii mimi kwangu namwona ni shujaa na mtetezi wa kweli ktk haki.. Simpendi wema lkn haina haja baya lisilo la haki limpate.
 
mtahangaika sana. kwa miaka mingi mmeaminishwa kwamba lissu ndio mwanasheria bora kuliko wote, kwamba hashindwi kesi, kwamba anajua sanaaaaaa kuliko wanasheria wengine. You are very wrong.
Ngoja tukusifie wewe! You are the Best than all! Congratulations!
 
Naona wanachadema busy na yasiyosaidia wananchi au kuwaletea maendeleo.
Ccm ndo wameacha ahadi zao wanahangaika na wapinzan tu na bado miaka miwili tu amalize miaka 5 afu hajafanya chochote alichoahidi maana wameahidi viwanda wanaleta viwonder
 
Usilitaje jina la Mungu kwa mambo yasiyo ya maana na wala usimshirikishe ktk mambo ya kijinga. Mnatafuta laana na mambo yenu ya mihemko ya kisiasa. Mungu akusamehe.
huyu nae kavurugwa, hapo kamdhihaki vp Mungu wetu? Hivi mbona usemi huyo anaewezasema anaposimama ni Mungu kasimama, utukufu huo Mungu kuwa miguu yake kapewa saa ngapi?
 
Ameandika wakili msomi Tundu lissu

Sio msokoto wa bangi. Hati ya mashtaka dhidi yake inasema Wema amekutwa na gramu 1.08 za bangi. Gramu, sio kilogramu. Polisi waliokamata 'madawa hayo ya kulevya' walifanya sachi saa tatu usiku. Sheria inayohusu sachi inasema sachi inatakiwa kufanyika kati ya saa moja asubuhi na saa 12 jioni ili, obviously, kupunguza uwezekano wa polisi kupandikiza ushahidi. Tunamsubiri Paul Makonda mahakamani aje atoe ushahidi wa namna alivyojua Wema anatumia madawa ya kulevya mpaka akamtaja hadharani. Asipokuja basi kesi hakuna.
 
Mtoaa mada ulimsikiliza Steven nyerere kwenye audio zake zote na mama wema na akatoaa ushahidi
 
Ameandika wakili msomi Tundu lissu

Sio msokoto wa bangi. Hati ya mashtaka dhidi yake inasema Wema amekutwa na gramu 1.08 za bangi. Gramu, sio kilogramu. Polisi waliokamata 'madawa hayo ya kulevya' walifanya sachi saa tatu usiku.

Sheria inayohusu sachi inasema sachi inatakiwa kufanyika kati ya saa moja asubuhi na saa 12 jioni ili, obviously, kupunguza uwezekano wa polisi kupandikiza ushahidi.

Tunamsubiri Paul Makonda mahakamani aje atoe ushahidi wa namna alivyojua Wema anatumia madawa ya kulevya mpaka akamtaja hadharani. Asipokuja basi kesi hakuna.
NILIONGEA JUU YA LISU KUKAMATA HUU MPINI, Lazima amweke mtu wake kati. Harafu nimekumbuka wale watemi wa WWE wanavyotwangana mangumi ya kulipizana, twanga! anasikilizia na yeye anajibu, mtwango! piga nikupige inaitwa hivyo
 
Sasa huyu wakili "msomi" mbona anaanza utetezi mitandaoni wakati kesi ipo mahakamani?
anarusha ngumi kwa swaiba yake ajibu, si alianzisha ngumi za mtandaoni, wacha kila mtu atunishe misuli muvi inogile %^&*%#@$^*
 
Back
Top Bottom