Alichofanyiwa Zitto ndani ya CHADEMA: Akili ndogo inatawala akili kubwa

Mwigulu huna jipya wewe hiyo akili ndogo kutawala akili kubwa umeicopy kwa peter msigwa halafu unashindwa kumnukuu
 
kama mtu una akili zinazokutosha kichwani huwezi kuandika namna hii. haya ni maandishi ya hovyo kuliko ,kuwahi kuyasoma.
 
Chadema ni chama kinachoendeshwa katika misingi ya kilaghai...

Lazima kiwaume! Hakuna watu wamepata hasara kwa ZITTO na Mamluki wengine kuvuliwa Gamba km nyie na chama chenu CCM!
Kama CDM kinaendeshwa kwa misingi ya kilaghai, si aende CCM chama kilichokuwa kikimtumia kuivuruga CDM?
CHADEMA ni taasisi na haitegemei Umashuhuri wa mtu mmoja mmoja isipokuwa watu ndio wanaotegemea umashuhuri wa CDM!
ZITTO hakuwahi kujua kwamba CDM ni chama chenye kuweza kuweza kuchukua kile kinachoitwa Maamuzi magumu.

Masikini CCM walimtegemea Zitto km Karata yao ya mwisho ktk uchaguzi mkuu 2015. Bahati mbaya Jogoo kawika kabla hakujakucha!!
 
najua umeshindwa kulisema hili kwa kuwa wewe ni public figure naomba nikusaidie @zitto amefukuzwa kwakuwa ni dini tofauti na malengo ya chama,,,,,,anatoka kanda tofauti hivyo pengine angeweza kutwaa uenyekiti na kupoka nguvu ya ile kanda sasa chama kinaendeshwa na akili ndogo.


​ccm tushangilie ushindi unakuja...
 
washauri wahamie huko uliko toka lini ukaombea chadema mambo mazuri,halafu hili jambo limewauma magamba zaidi
 
Mbona puvu linaanza kukutoka, gamba mkubwa? Hizo ni hasira baada ya kuona kwamba mpango wenu wa kuwapandikiza virusi wa kuivuruga CHADEMA umegonga mwamba. Kajipange upya. Mlidhani hila zenu hazitagundulika? Nenda zako gaidi mkubwa!
 
Msimamo wa mtu mmoja mwingine anaweza kuuelewa. Ukifuatilia mtiririko wa masuala ndani ya Chadema, ungeelewa in kwanini CCM imeumia sana an hatua hii ya Chadema kumsimamisha uongozi Zitto Kabwe. Waliwekeza fedha nyingi sana kwake ili aisambaratishe Chadema. $1,000,000 kwa mtu mmoja tu kama Zitto siyo mchezo. Chadema wameshtukia mchezo na kuvunja daraja hilo. Ndiyo maana CCM wanahangaika. Kwa Hilo sasa wanasikitishwa kushtukiwa mipango yao. Kwamba CCM wanaumizwa sana an hatua hiyo ya Chadema siyo jambo linaloweza kumshangaza yule anayejua mchezo wa CCM nyuma ya pazia inavyoshirikiana na TISS na Polisi kuiangamiza Chadema. Ukilijua hilo utaona mantiki ya masikitiko ya CCM.

Naomba nikusahihishe,

Zitto hajasimamishwa uongozi Chadema bali amevuliwa uongozi.

Anayesimamishwa huwa anaweza kurudishwa.

Hawa mamluki baada ya siku 14 wanafutwa rasmi uanachama ili kilio kikolee Lumumba.

Msishangae mkiona hadi Jakaya Kikwete naye akianza kulialia kana hii misukule yake iliyoleta hii thread mavi.
 
Mheshimiwa, wewe unacheo kikubwa ndani ya chama. Hutakiwi kuyazungumzia haya kwa hali hii hata kama ni propaganda. Sijui unazungumza kama kiongozi wa chama au kama wewe tu? Hata hivyo CDM ni taasisi kama CCM. Kuheshimu maamuzi ya taasisi yoyote kwa kiongozi kama wewe ni vizuri sana. Achana na siasa za Le Mutuz!

Usimshangae hana akili huyu jamaa.viongozi wenzake wametulia yeye anapayuka kabla hata ya viongozi wa cDm wenyewe kusema.kwanza ameiga quotation ya Peter Msigwa.SHAMEeee on you mwigulu....
 
maamuzi magumu waachie CHADEMA pekee.
hivi inawezekana kweli kocha msaidizi wa Team A akatetea maslahi ya wachezaji wa team B??
 
Kwi kwi kwi kwi lol!!!! Nyie MACCM mbona mnatokwa na mapovu hivyo!? Maamuzi yafanywe ndani ya CHADEMA mapovu mtokwe nyie!? Ni aje MACCM!? Kama mnamuona wa maana kiasi hicho si mumpe ukatibu Mkuu B ndani ya chama chenu kabla hajamfuata rafiki yake Kafulila kule NCCR!?

Kwa jinsi mnavyotokwa na mapovu inaonyesha ni kiasi gani mlikuwa mnafaidika na yeye kuwepo ndani ya CHADEMA na katika nafasi za juu za uongozi. Sasa siri za ndani ya CHADEMA hamtazipata kamwe.

Chama chochote cha siasa kilichokomaa huweza kuchukua maamuzi magumu ambayo hayakutegemewa na wengi bila kujali athari zake. Mlidhani Viongozi wa juu ndani ya CHADEMA hawawezi kufanya uamuzi walioufanya sasa imekula kwenu na inaelekea mliwekeza sana ili kupata ya ndani kabisa toka CHADEMA, maana haingii akilini hizi kelele mnazozipiga kupinga maamuzi ya chama ambacho hakiwahusu kwa lolote lile. Sijawahi kuona MACCM yakitokwa mapovu kiasi hiki!!! Dah!!!!

Nyie kwenu kule kamwe hamuwezi kuthubutu kumvua yeyote uongozi wa juu maana kila mtu ni mchafu wa kupindukia hana moral authority ya kumnyooshea kidole mwenzake na kumwambia hapa umevurunda kupita kiasi kwa hiyo uongozi wa juu ndani ya chama umeamua kukuvua wadhifa wako na pia kukufukuza kama mwanachama. Ndiyo sababu kubwa ndani ya chama chenu kuna wauza unga, mafisadi akina Mkapa, Lowassa walionunua Urais kwa mabilioni 2005, mafisadi wa rada, EPA, majangili na kila mazagazaga mabaya yote ndani ya nchi yetu yamekumbatiwa ndani ya chama chenu kilichokosa muelekeo.

Wanachadema popote pale mlipo tembeeni vifua mbele kufurahia ukomavu mkubwa ulionyeshwa na Viongozi wa CHADEMA kuchukua maamuzi magumu kama haya. Wameyavumilia mengi na kwa miaka mingi lakini uvumilivu una mwisho wake ndio maana wamesema sasa basi imetosha ni lazima turudishe mshikamano na heshima katika chame chetu kwa faida ya wanachadema wote, viongozi wao na pia kwa faida ya Tanzania na Watanzania. Ndani ya CHADEMA siku zote akili kubwa hutawala akili ndogo tofauti na MACCM, "Sasa tunalivua gamba" Ooh!! hatulivui tena...hatukusema hivyo...kauli ile mliitafsiri vibaya kwi kwi kwi kwi CCM MULUGO na Serikali MULUGO.

CHADEMA Oyeeee!!! Oyeeee!!! Peopleeeeez!!!! Pawaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa


Alutta continua!!! continua!!!!


:peace::peace::peace:
 
Back
Top Bottom