Kikifanywa kwa Kiba eti ni sahihi kabisaaaaa, ila kikifanywa kwa ndomo basi ni kinyume chake huku wakiwatusi watanzania, sasa sijui wenzetu wakenya!!! Hivi kumbe kuunyanyua muziki wa tz ni kumnyanyua ndomo tu na kuwakandamiza wanamuziki na wasanii wengine??? Hell Noooo kama wanataka mabadiliko basi yaanze na wao,wanachomfanyia Kiba sio kabisaaaa ila hilo walaa hawalioni
Au mnasahau maneno kama "wakati wake umekwisha" "hajui lolote" na matusi kede wa kede!!, why hamkusapoti juhudi zake hizi za sasa maana ni kati ya wanamuziki wa kujivunia Tanzania, ila mkakazana kweli kumdidimiza alafu mje mseme mnakuza muziki wa bongo flavour!!(upi kwanza)
Hizo mnazoziita chuki mmezipandikiza wenyewe, ukipanda mchicha huvuni mahindi, kama nyie wasafi sana, wazalendo sana,mna akili sana, wajuvi sana,mna upendo sana anzeni kwa kutokuwabagua wanamuziki wetu(wanaofanya vizuri) ili muziki wetu uendelee,
Msimtafute mchawi wenu wakati mmejiroga wenyeweeeeee, hebu anzeni nyie kwa kuziondoa hizo chuki zenu kwa Kiba alafu ndio muendelee kuhubiri huo uzalendo wenu, au uzalendo unahitajika kwa mmoja tu nchi hii!!!
Mwaona maboriti ya kwenye macho ya wenzenu tu atii!!! Haya wenye good look zenu onyesheni kwa vitendo mnayoyahubiri humu na hukooo!!