Alhaji Mussa Salum: Mwezi haujaonekana

Alhaji Mussa Salum: Mwezi haujaonekana

"Tamko lisilo na mipaka maalum."



Ama jambo la kusema kila watu na mtenguko wao wa jua kwa hivyo wana wakati wao wa kuswali na kufunga (Swaum) ndio hivyo hivyo; ni vyema ieleweke hivyo ni vitu viwili tofauti. Swala imeambatana na mitenguko ya jua na Swaum imeambatana na kuandama kwa mwezi. Mas-ala ya nyakati za Swala yameshaelezwa na kufafanuliwa na Mwenyewe Mwenyezi Mungu katika Qur-aan na pia Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amelibainisha kwa uwazi kabisa katika Hadiyth. Wala hakuna ikhtilafu yoyote mbele ya Wanazuoni juu ya jambo hilo. Ijmai ya Wanazuoni wamekubaliana kuwa kila sehemu, wala si kila nchi nzima inaweza kusali kwa wakati mmoja. Kwani mtenguko wa jua unaweza kutofautiana hata katika nchi moja. Angalia Dar es Salaam na Kigoma wanaswali na kufuturu tofauti, lakini wanafunga kwa mwandamo mmoja.



Kila sehemu itaswali kwa wakati wake kwa kutegemea mtenguko wake wa jua. Mwenyezi Mungu Amebainisha hayo katika Surat Bani Israil (17: 78) kama ifuatavyo:



{{أَقِمِ الصَّلَاةَ لِدُلُوكِ الشَّمْسِ إِلَىٰ غَسَقِ اللَّيْلِ}}



{{Simamisha Swala jua linapopinduka (likaenda magharibi) mpaka giza la usiku.}}
 
Kama vile nimesikia watu wanaswali asubuhi, sijui nlikua naota.... sijaenda job najua leo Eid
 
ndugu,kabla hujaandika tafakari kwanza,na hivyo hivyo kabla hujapost,hatupo hapa kwa ajili ya kutukanana....ANAEFUNGUA LEO AFUNGUE,NA ANAEFUNGA AFUNGE...Mbona kina Shafii na Maliki (awawie radhi M/mungu)hawajaishi hivyo???KAENI CHINI MSOME..
Baad ya kusoma ndio nimeibuka na msimamo huu! kabla hapo nilikuwa nasubiri mpaka niambiwe cha kufanya. kusoma kumenisaidia kujua ukweli. Islamic calenda ndio ntarehe tulioletewa na Quran, so haiwezekani tarehee hii isituunganishe au tushindwe kutekeleza ahadi kwa tarehe ya kiislam, Wanakuuliza kuhusu mwezi mwandamo! sema hizo ni nyakati kwa watu na hija (Quran) nilichokifahamu hapa mamboyetu yoote tunatakiwa tutumie tarehe ya kiislamu, lakini hilo halitawezekana iwapo kila nchi watahesabu mwzi kivyake, misimamo ya kila mtu na mwezi wake ndio iliyoufanya ulimwengu wa kiislam kushindwa kuitumia kalenda ya kiislam huku tukijitapa Quran imekamilika wakati tunaishi kwa tarehe ya kikiristo. Mnaizalilisha kalenda ya kiislam.

https://www.jamiiforums.com/habari-...alendar-a-question-of-messed-up-calendar.html
 
Mimi huwa siwaelewi hawa jamaa zetu katika Mungu mmoja. Wao sikukuu yao kutegemea mwandamo wa mwezi si hoja kwangu ila hoja ya msingi ni shida na mahangaiko ya kuuona huo mwezi km umeandama.

Ebu mtuondoleeni uvivu wa kufikiri ktk zama hizi za sayansi na technolojia mnashindwa kuwa na technolojia ya kuona km mwezi umeandama au bado.

Maana huwa mnatusumbua ata wengine tusiokuwemo mtu unaamka hujui ni Eid au la! Unawaza uende kazini au vipi jamani ebu badirikeni kila kitu kinawezekana acheni uvivu.

sasa mkuu kama wewe ni katika "wasiokuwemo" kinachokuwasha ujue ni nini na wewe haikuhusu?
 
Tatizo sikukuu zenu zinategemea majaaliwa ya mwezi halafu hiyo ya January mosi ipo kwenye calendar mnayotumia hata nyinyi

Hapo kwenye RED, I see ...kumbe hili kwako ni TATIZO?? Wewe ulitaka iwe inategemea nini labda?iwe inategemea moshi mweupe ? Hebu waache waislamu na dini yao, usiwachagulie unachotaka wewe. Wewe una dini yako na wao wana yao, wewe una abudu mungu wako na wao wanaabudu MUNGU wao. Vumilia ndio njia pekee iliyobaki.
 
Wanaudhi sana! Ata siku ya kihama watakosea siku wanakuja leo kumbe hukumu imetolewa jana au wanasubiri kesho kumbe hukumu leo hatari yake ni wote kukubwa na kihama..! Wenye hatia na wema.

Ungerudi kwanza KG 1 ukajifunze kuandika ,halafu ndio uje hapa kujenga hoja.
 
Umeona! hawajamaa shule ndogo eti hawaoni km kila sikukuu wanatumislead...!

Hongera sana wewe mwenye shule kubwa ambayo imeshindwa kukusaidia kukufunza kuandika vizuri,kujenga hoja, kuwa mstaarabu nk.
bora mimi muislamu mwenye"shule ndogo" ambaye mchango wangu usio na ubaguzi kwa jamii unaonekana tena jamii yenye waislamu na wasio waislamu!
Shule yangu ndogo imenifunza kujenga hoja na kukubaliana kutokubalina kwa yule ambae ana mtizamo tofauti na mimi.
Shule yangu ndogo imenisaidia kujifunza kuheshimu imani ya mwengine!
 
Dada FF hii kila siku kuhitilafiana na wenzetu itaisha lini?
Inakera sana. Saudia ina tofaut gani na Tanzanua?Kila kitu tupo sawa nao! Mwez ungeonekana Japan au Kule Australia sawa, lakini kwa Saudia

Mwenendo wa mwezi si kama jua.

Huku kukhitilafiana kuna kheri kubwa sana ndani yake, laiti tusingkhitilafiana kusingekuwa na maswali wala tafiti za ziyada.

Mi nnaichukulia hii kama blessing kubwa sana.
 
Back
Top Bottom