Alhaji Mussa Salum: Mwezi haujaonekana

Alhaji Mussa Salum: Mwezi haujaonekana

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,143
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhaji Musa Salum,kwa niaba ya Kaimu Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir,amesema kuwa mwezi haujaonekana na hivyo Waislam wataendelea na mfungo kesho.

Alhaji Salum amesema swala ya Eid itafanyika Jumamosi tarehe 18 na kimkoa itakuwa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja na kitaifa ni mkoani Geita.

Chanzo: East Africa Radio
 
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhaji Musa Salum,kwa niaba ya Kaimu Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir,amesema kuwa mwezi haujaonekana na hivyo Waislam wataendelea na mfungo kesho.

Alhaji Salum amesema swala ya Eid itafanyika Jumamosi tarehe 18 na kitaifa itakuwa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja.

Chanzo: East Africa Radio

Kitaifa Geita. Mnazi Mmoja labda kimkoa
 
Maajabu ya dunia haya hadi petro unatoa taarifa za mwez... By the way huyo mtu anaitwa alhaji kweli?? Jiridhishe kabla ya kupost

Mkuu yaser,si dhambi kutoa taarifa. Anaitwa Alhaji. Amekwenda na kurudi salama kuhiji
 
Last edited by a moderator:
Mkuu yaser,si dhambi kutoa taarifa. Anaitwa Alhaji. Amekwenda na kurudi salama kuhiji

Alhad!
Ndivyo wanavyomuadress daily...huwa najiuliza tofauti ya Alhaj na Alhad ni nini?
Pia sijawahi kusikia mwingine awaye yote akiitwa Alhad...ila yeye tu.

Naomba wajuvi wa haya mambo wanitoe tongotongo katika hili.. FaizaFoxy, Gang Chomba na wengine tafadhali.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom