Albert Msando: Hatushindani na chama au wanachama wa CHADEMA

Albert Msando: Hatushindani na chama au wanachama wa CHADEMA

Wakili msomi AlbertMsando ametoa yaliyo moyoni. Kupitia ukarasa wake wa Fb haya ndio aliyoandika.

Albert Msando

Kwa marafiki zangu

Hatujashinda kesi dhidi ya chama. Hatushindani na chama au wanachama wa CHADEMAQUOTE]

Acha kubwabwaja wewe haya tuambie Robert Makaranga alikuandikia namna ya kufaili kesi kama ilivyozagaa kwenye mitandao

Natambua kwamba kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA mojawapo ya madhumuni ya chama ni kuendeleza na kudumisha Demokrasia katika mfumo wa vyama vingi vya siasa, kujenga utamaduni wa demokrasia katika jamii kwa kutambua haki za wengi katika maamuzi na pia kutambua haki za wachache kusikilizwa, kuheshimiwa na kulindwa, sambamba na kukubali ushindani huru, wa haki na wa wazi

Pale ulipokwenda Sarena kutangazia wananchi kuhusu matakwa ya mteja wako na wewe mwenyewe yndio demokrasia inayohitajika wewe unataka kulazimisha taratibu na kanuni ziende nje ya utaratibu wa chama kwa nini hukumshauri mteja wako aende mbele ya kamati halafu ndio uende mahakamani kama umevimbiwa fedha unazolipwa na MACCM ili ubomoe chama peleka zingine huko mabogini kwa yatima na wajane wakajihifadhi Msando hutabomoa chama kitalinwa na wananchi wameteseka sana ndani ya mumiani wa kisiasa CCM kwa miaka 52 nchi iko mikono mwa koo kumi na moja hakuna atakaye kubali kufunga spidi governer mageuzi

Pia natambua kwamba kwa mujibu wa Katiba ya chama Wajibu wa mwanachama wa Chadema ni kuwa tayari kupambana na namna yeyote ya uonevu, ukandamizaji, udhalilishaji na ubaguzi

Unataka kusema umekuwa mbunge mabogini kwa sababu ya kabila lako la kichaga wewe umelewa fedha lakini aibu ya kusaliti chama itakwandama milele utazomewa popote uendapo kwa sababu MACCM yenyewe yameshindwa kubomoa chama wewe utaweza usivimbe kichwa kujinadi eti unabaguliwa mteja wako ni muha alipewa unaibu katibu mkuu na vyeo vyote kwa sababu ni MUha wewe msando kula hizo fedha ukiwa na akili si kuropoka ropoka wakati umepewa fursa zote sio kwa kabila lako ila kwa sababu ulikuwa unaweza

Wajibu huu ni ndani na nje ya chama. Hatuwezi kutekeleza wajibu upande mmoja. Binafsi ninalo jukumu kutekeleza wajibu wangu kwa manufaa ya chama
Hicho ndio wanachama wanasema kama wewe na mteja wako ni Malaya wa kisiasa nendeni mukajiuze kisiasa kwa MACCM huko huko ,unavunja taratibu za chama kwa sababu muna wakwe IKULU halafu unakuja kuongea ujinga eti taratibu ziwe ndani na nje wakati wewe unafanya hayo hayo unayolaumu watu

Kumekuwa na lawama, shutuma na malalamiko kwamba nilichokifanya kinadhoofisha chama. Napinga kwa nguvu zangu zote. Inawezekana kabisa nilichofanya kinadhoofisha watu wachache ndani ya chama ila sio CHAMA.

Ndio mpango wako na mteja wako baada ya kuona umma uko nyuma ya chama sasa unataka kutenga viongozi na chama kama nyie mulivyojitenga tukuulize hivi wewe hujui kwamba Katiba ya chama imesema kwamba kupeleka chama mahakamani si utaratibu kama ulikuwa unapambana na watu sasa baraza la wadhamini kwa nini ulilishitaki si ungeshitaki mwenyekiti na katibu mkuu wale wanaoongoza vikao rushwa itakutokea puani wewe chama hiki beba na hata yule mkulu pale magogogoni hamkiui

CHADEMA sio mtu binafsi. Ni taasisi. Wanachama wake ndio nguzo muhimu. Sio Zitto wala Mbowe wala Slaa. Hawa ni viongozi tu ambao wajibu wao ni kuendelea kujenga chama Uwezo wao upimwe kwa matokeo ya sasa. Sio kwa mvuto na haiba zao. Fundisho la haya yote ni moja: KUVUMILIANA SIO KUFICHIANA SIRI AU UDHAIFU. Kosa limetendeka na kukubali kosa sio dhambi
.


Kama ulijua Chadema ni taasisi basi ungefuata misingi ya kutatua tatizo la mteja wako kitaasisi lakini kwa sababu umetumwa ndio maana ulivizia usiku wa manane kupeleka pingamizi wewe ni mvurugaji umevaa uchadema huku ukila kwa mkono wa nyuma uzuri unaanza kupata hisia kwamba siri zako na mteja wako kuwa mamuluki ,wasaliti nchi nzima wanazijua endeleeni kukodishiwa wapiga mawe

wazi kabisa kumekuwa na kutokuelewana kwa muda mrefu. Ni dhahiri viongozi wetu wamekuwa wanajua udhaifu wa kila mmoja wao. Lakini kwa sababu ambazo hazijawa wazi waliamua kukaa kimya. Au labda ilikuwa ni kwa kuamini kwamba yatamalizika bila athari. Sasa matokeo yake ndio haya

toka lini mahakama ikawa suluhisho la watu wasioelewana kama ulikuwa unalijua hilo jitahhada zipi ulizifanya ili wasioelewana wakaelewana mumiani wa kisiasa wewe kupitia joho la uwakili

]Kinachohitajika sasa sio kutafuta mchawi. Ni jukumu la kila mmoja wetu kuwajibika ipasavyo na kuhakikisha suluhu inapatikana. Na niseme wazi kabisa, kama suluhu ni mtu kufukuzwa basi tuhakikishe hilo linafanyika kwa mujibu wa Katiba na Kanuni kwa kuzingatia haki za msingi kama ambavyo tumekuwa tukipigania.

Hakuna cha damage control hapa suluhu ipatikane kwa mtinagi wewe mteja wako kila wakati amekiumiza chama kwa njia mbalimbali unabariki dhambi ya usaliti halafu unasema suluhu ishieni mahakamani na mutakuwa marafiki wa mahakama lakini wananchi watalinda chama chao kajenge tuu maghorofa fedha mulizopewa simulikubaliana 2015 chama kiwe kimekwisha munaona mbele giza unataka suluhu na nani maliza hata miezi sita ukifungua kesi za kila sampuli lakini ujenzi wa chama unaendelea wewe ukinuua kipara chako mahakamani kuna watu wako vijijini wanaeneza injili ya chadema na ukombozi

Haki itendeke, na zaidi lazima ionekane imetendeka. Pamoja tunaweza
.

Taja haki moja ambayo muteja wako alidhulumiwa kama alinyimwa kitu sasa wewe na mteja wako mukishauriwa jambo mukakubali munaligeuzia mtaji wa kisiasa embu twambia Msando unaamini Mbowe alimuua Chacha wangwe kama mteja wako anavyosema wakati mahakama ilimtia hatiani muuaji na KIkwete akamtoa baada ya wiki mbili hiyo ndiyo haki usemayo

Mwisho, tusiruhusu muendelezo wa 'ufuasi' wa watu ndani ya chama. Tuwe wafuasi wa misingi ya chama. Bado nafasi ipo ya kurekebisha pale tulipoangukia kama busara na hekima vitatumika



baada ya kugundua wanachadema na wafuasi wao ni wafuasi wa chadema na mteja wako anapambana na wanachadema wote ndio maana kwa msaada wa CCM mulipotaka kuzuia Safari ya Katibu mkuu Kigoma mukajua hakuna mfuasi wa mtu wewe ndio mfuasi wa mtu hufai kuwa wakili wa mteja munayepanga naye njama za kuua chama
Nawatakia kila kheri ndugu zangu.
Jitakie heri mwenyewe Mungu akuangazie mwanga ujitambue kwamba hata upate fedha sawa na mlima Kilimanjaro hutaiuwa chadema ,mageuzi na mabadiriko kwa sasa ni inevitable
In a battle for the minority rights we have to promote the rights of the majority and we will remain united" AGM 2014.

truly you have united with CCM and TISS to use every unjustified means to slow the pace of changes but you will never win
 
hongera sana msando,

salam na ziwafikie huko TENGERU,,KILAM KITU HUYO MZEE ASIANGALIE KWA KUTUMIA MAKENGEZA KAMA YALE YA MKWE WAKE,MKAZA BINTI YAKE,,,ZAMA ZIMEBADILIKA HIZI,,

CHAMA KIWE NI CHA KITAIFA,,CHAMA KISIWE CHA KIKANDA,KIDINI NA KIKABILA,HILO HALIKUBALIKI

Jadili mada sio vilema vya watu makengeza ya Mtei kwani yalimfanya ashindwe fanya kazi zake wewe hapa juzi umetangaza upambe wa gesi haitoki umeshindwa sasa unalipwa book 7 mwalimu mzima huku ukijua kabla hujafa hujaumbika kipofu na mfinyu wa ufikiri wewe
 
Najaribu kuelewa tu Kashaga. Kwani Kamati Kuu ilikwishamchukulia hatua za kinidhamu Zitto? Si ndio process ilikuwa inaendelea. Walimapatia makosa 11, akatakiwa awasilishe utetezi, ndio Kamati Kuu ingetoa maamuzi. Labda kwa utetezi wake KK ingeridhika na kuamua vinginevyo. Kisha baada ya hapo ingefuata rufaa Baraza Kuu. Kwa mfano, Dr Kitila na Mwigamba, baada ya kuvuliwa uwanachama na KK sasa wana haki ya kikatiba kukata rufaa BK dhidi ya mamuzi yao. Sasa Zitto anataka kukatia rufaa maamuzi yepi?

Mkuu,zzk anakatia rufaa maamuzi ya kumvua vyeo vyake vyote chamani!
 
Kwani Msando kashinda kesi gani kwa haya matambo..mwambie asubiri kesi iendelee kama hajaikimbia kizimba chake cha utetezi..alikuwa anataka ukaribu na LEMA jamaa akamshtukia kuwa ni msaka umaarufu na noti.
Hebu kajiandikishe kwenye mashindano haya hapa kwenye pic.hurry

article-2535172-1A77596300000578-560_634x417.jpg
 
Msando umewavua nguo wazandiki

Ndugu yangu aminangalo huyo kajivua nguo mwenyewe. Ukiliangali hilo bandiko lake ni out of context tena limeandikwa kwa woga na kujishuku kwani niujinga kusema hujakishtaki chama wakati wanaofika Mahakamani ni Wadhamini wa chama na gharama zinazotumika ni gharama na muda ambao ungetumika kukijenga chama kwa hali nyingine hasa kipindi hiki tunachojipanga kwa chaguzi ndogo za madiwani pamoja na suala la Katiba Mpya ...hiki alichokifanya ni unafiki na asijishuku kwa kujidai "neutral" kimaadili kwasababu yeye ni mwanachama wa CHADEMA angekuwa ni mtu wa kutaka Umoja angemshauri mteja wake aende kwa wakili mwingine wa kumuwakilisha na siyo yeye iwapo kweli angekuwa mtu mwenye kupenda usuluhishi.

Atambue tu kwamba YOU CAN NOT EAT THE CAKE THE STILL HAVE IT.... aendelee na hilo alilolifanya na kuhusu CHAMA akae kimya hawezi kuwa wakili wapande mbili wala kushauri Chama kwa lolote.kwasasa watakao shauri upande wa CHAMA ni Tundu Lisu na Pita Kibatala ambao ndiyo watetezi wa chama na wadhamini walioshtakiwa.Yeye aendelee na upande alio uchagua vinginevyo ni uchokozi wa wazi na kebehi kwa chama na wanachama.
 
mshika chuma nadhan atakuwa kashikishwa chuma cha moto..!!

BIGSHOW ATAMUWEZEA WAPI??WAMESHINDWA WATU,LABDA WAYATUME MASHETANI,,

KAMA ANATAFUTA BWANA WA BURE HAPA HAWEZ KUMPATA,SISI TUPO HAPA KWA KAZI MOJA TUH,,KUKEMEA UKANDA,UDINI NA UKABILA WA HIYO SACCOSS YAO YA AYATOLLAH MTEI

Inaelekea huko Mtwara waheshimiwa sana waliokuwa wanawasulubu akina Gesi haitoki walikufanya mke akili yako inaretireate kwa kuwaita wenzio hivyo udini wako kama akina abdallah wa Tabata utashindwa kabisa ,waalimu wa udini akina KIkwete wamenyoosha mikono sasa
 
mimi nasema, kama haya wanayosema kina Msando hayana 'hidden' agenda then mimi sina shida, lakini hofu yangu ni kwamba haya wanayosema hayatoki moyoni
 
Kwani Msando kashinda kesi gani kwa haya matambo..mwambie asubiri kesi iendelee kama hajaikimbia kizimba chake cha utetezi..alikuwa anataka ukaribu na LEMA jamaa akamshtukia kuwa ni msaka umaarufu na noti.

Kwan amejitambia au kaongea ukwl wake?
 
Wakili msomi Albert Msando ametoa yaliyo moyoni. Kupitia ukarasa wake wa Fb haya ndio aliyoandika.

By; Albert Msando

Kwa marafiki zangu,

Hatujashinda kesi dhidi ya chama. Hatushindani na chama au wanachama wa CHADEMA.

Natambua kwamba kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA mojawapo ya madhumuni ya chama ni kuendeleza na kudumisha Demokrasia katika mfumo wa vyama vingi vya siasa, kujenga utamaduni wa demokrasia katika jamii kwa kutambua haki za wengi katika maamuzi na pia kutambua haki za wachache kusikilizwa, kuheshimiwa na kulindwa, sambamba na kukubali ushindani huru, wa haki na wa wazi ....

Pia natambua kwamba kwa mujibu wa Katiba ya chama Wajibu wa mwanachama wa Chadema ni kuwa tayari kupambana na namna yeyote ya uonevu, ukandamizaji, udhalilishaji na ubaguzi.

Wajibu huu ni ndani na nje ya chama. Hatuwezi kutekeleza wajibu upande mmoja. Binafsi ninalo jukumu kutekeleza wajibu wangu kwa manufaa ya chama.

Kumekuwa na lawama, shutuma na malalamiko kwamba nilichokifanya kinadhoofisha chama. Napinga kwa nguvu zangu zote. Inawezekana kabisa nilichofanya kinadhoofisha watu wachache ndani ya chama ila sio CHAMA.

CHADEMA sio mtu binafsi. Ni taasisi. Wanachama wake ndio nguzo muhimu. Sio Zitto wala Mbowe wala Slaa. Hawa ni viongozi tu ambao wajibu wao ni kuendelea kujenga chama.

Uwezo wao upimwe kwa matokeo ya sasa. Sio kwa mvuto na haiba zao. Fundisho la haya yote ni moja: KUVUMILIANA SIO KUFICHIANA SIRI AU UDHAIFU. Kosa limetendeka na kukubali kosa sio dhambi.

Ni wazi kabisa kumekuwa na kutokuelewana kwa muda mrefu. Ni dhahiri viongozi wetu wamekuwa wanajua udhaifu wa kila mmoja wao. Lakini kwa sababu ambazo hazijawa wazi waliamua kukaa kimya. Au labda ilikuwa ni kwa kuamini kwamba yatamalizika bila athari. Sasa matokeo yake ndio haya.

Kinachohitajika sasa sio kutafuta mchawi. Ni jukumu la kila mmoja wetu kuwajibika ipasavyo na kuhakikisha suluhu inapatikana. Na niseme wazi kabisa, kama suluhu ni mtu kufukuzwa basi tuhakikishe hilo linafanyika kwa mujibu wa Katiba na Kanuni kwa kuzingatia haki za msingi kama ambavyo tumekuwa tukipigania.

Haki itendeke, na zaidi lazima ionekane imetendeka. Pamoja tunaweza.

Mwisho, tusiruhusu muendelezo wa 'ufuasi' wa watu ndani ya chama. Tuwe wafuasi wa misingi ya chama. Bado nafasi ipo ya kurekebisha pale tulipoangukia kama busara na hekima vitatumika.

Nawatakia kila kheri ndugu zangu.

"In a battle for the minority rights we have to promote the rights of the majority and we will remain united" AGM 2014.

Msando

Msando Una mmunya maneno kama amshindani na chadema garama zakesi anatoa nanani na mmemshinda nani?
 
BAADA YA SHAURI LA MH ZITTO KABWE KUPATIWA UAMUZI WA MAHAKAMA,,NAJIULIZAA,,HIVI NI KWELI KWAMBA KAMATI KUU YA CHADEMA HAIKUWA IKIFAHAMU KWAMBA:-

Ibara 6.3.6(d) ya Katiba ya Chama chao cha Chadema inasema;“Kiongozi aliyechukuliwa hatua za kinidhamu na mamlaka yake ya nidhamu anayo haki ya kukata rufaa ngazi ya juu ya ile mamlaka yake ya nidhamu na uamuzi wa ngazi hiyo utakuwa wa mwisho”.???

Kwamba Ibara 6.3.6(e) ya Katiba ya Chama;“Rufaa yoyote lazima ifanyike katika muda wa siku thelathini tangu tarehe ya kupokea rasmi kwa maandishi maamuzi ya mamlaka iliyotoa adhabu”.,,na kwamba ;Kanuni za Uendeshaji zinatoa
UTARATIBU ambao unatakiwa ufuatwe ili kiongozi aliyeadhibiwa aweze kutumia HAKI yake ya kukata rufani kwa maneno haya??

Kwamba Kanuni ya 6.5.8 ya Kanuni za Uendeshaji za chama hichohicho cha chadema,inasema;“Kiongozi aliyeadhibiwa atapewa taarifa ya msingi wa maamuzi ya mamlaka ya nidhamu ili kumuwezesha kuamua kukata rufani au la”??

Kwamba Kanuni ya 6.5.9 ya Kanuni za Uendeshaji;“Mwadhibiwa atakayeamua kukata rufani atatakiwa kufanya hivyo katika muda wa siku thelathini baada ya kuarifiwa uamuzi wa adhabu”??

Kwamba Kanuni ya 6.5.10 ya Kanuni za Uendeshaji;“Baada ya kutoa uamuzi kikao husika kinalazimika kuandaa taarifa kamili ya mwenendo wa shauri na kuwasilisha ngazi ya juu.??

Na kwamba Taarifa hiyo, lazima ifike katika muda wa siku kumi na nne baada ya kikao cha maamuzi”??

NITASHANGAA KAMA TUNDU ANTIPAS LISSU ATAACHWA AENDELEE KUWA MWANASHERIA MKUU WA CHADEMA,BAADA YA MAKOSA HAYA YA KITAALUMA

NI WAZI ATAKUWA BILA KUMUNG'UNYA MANENO,,AMESHINDWA KUISHAURI VEMA,NA KISHERIA,KAMATI KUU YA CHAMA CHAKE,ILI IONE JINSI AMBAVYO ILIKUWA INAVUNJA VIPENGELE HIVI VYA KATIBA AMBAYO NDIYO SHERIA MAMA

Wanayajuwa sana ndio maana alipelekwa mashitaka kumi na moja ili aya jibu Zitto na wakili wake hawakutaka kuwajibika kwa taratibu za chama wameamua mahakama iwaamuliye uanachama wao kwasababu wamekaidi taratibu za chama basi waendelee kujiongoza kwa sababu wako juu ya chama hata kama anaonewa angejenga precedance nzuri sana kama maamuzi yangeenda hovyo hovyo hata angefukuzwa angekata rufaa ingekuwa evidence nzuri ya kuenda mahakamani na umma hakika ungekaa nyuma yake sasa kabatizwa msaliti jina ataishi nalo milele kama Mrema mwache sasa awe mbunge wa Jaji JOhn Utamwa
 
Jadili mada sio vilema vya watu makengeza ya Mtei kwani yalimfanya ashindwe fanya kazi zake wewe hapa juzi umetangaza upambe wa gesi haitoki umeshindwa sasa unalipwa book 7 mwalimu mzima huku ukijua kabla hujafa hujaumbika kipofu na mfinyu wa ufikiri wewe

Eti,,mwalimu,,sijui nani kawaambia mimi ni mtaaluma hiyo..

Unajaribu ku-tabir lakin unashindwa na unahangaika sana,pole sana,

Even though siwez kuidharau na kuibeza taaluma hiyo,kwan bila walimu hao unaowadharau nisingefika hapa,au usingefika hapo,,lakin hiyo sio professional yangu,,vip unataka kuijua proff yangu??nikusaidie nikutoe kwenye hiyo tabu??

Mwehu kweli wewe,usiish maisha ya kulabdia labdia,,,watu tuna maisha yetu,,na hatutii huruma kama vikaragosi wa wanasiasa nyinyi,,

TUPO HAPA KWA KAZI MOJA TUH,KUPIGANIA RASILIMALI ZA TAIFA,KUWATESA WANASIASA NA KUKEMEA UKANDA UDINI NA UKABILA AT ANY COST AND BY ANYMEANS NECESSARY,,

WHETHER YOU LIKE IT OR NOT,YOU HAVE TO FACE IT MWEHU WEWE
 
Msando na ZZK wanacheza goma la CCM. Kazi ya Wassira hiyo, Jaji kwa simu kutoka ikulu kazi kweli kweli. Kesi CDM watashinda ila sio leo kitakachotokea ni kupigwa tarahe. Maneno ya ZZK -"Msando tufanye kila linalowezekana ili niweze kuwepo bungeni kwasasa kwani posho zitaongezeka mwaka huu hasa ukizingatia bunge la katiba litaongeza siku za vikao, Mkulu ameniahaidi tukifungua tu kesi, itakuwepo mahakamani mpaka mwaka 2016, ila lazima tuhakikishe tunaijeruhi CDM kinoma ili hawajamaa wasipate tabu uchaguzi 2015, tayari wameshaandaa kesi wewe nenda tu mahakamani kila kitu kipo poa" mwambieni abishe.
 
Daar,hapa ni kutaka kujikosha tuu
Kwani kwa kumpigania ZZK Msando anapromote vipi majority rights kama anavyojinasibu kwenye nukuu? At the end of day,Msando is another traitor!
 
Hivi mahakama si imekataza kujadili uanachama wa Zitto Zuberi Kabwe hadi kesi ya msingi isikilizwe? Mbona ndo kinafanyika au watu tukiwa siyo Kamati Kuu tunajadili mambo ya kimahakama si kuingilia waheshimiwa jamani??????? Naomba tutulizane tusubiri walioruhusiwa na mahakama wafanye hivyo. Cha ajabu aliyeshinda ndiye anaanzisha mjadala uliokatazwa ameshinda kushindwa?????
 
Huyu ndio anaeneza propaganda kwamba kashinda na sasa anataka suluhu ili aonekane mwema!,bado mnajaribu kushindana na chama na wanachama wake lkn hamta shinda.Ngoja kesi ianze na nakushauri mwambie Zito akachukue karatasi zake pale ofisini kuonyesha jinsi alivyovuliwa vyeo.Nendeni pamoja nae,nawe Msando diwani wa mabogini na huku hukai mabogini ulipewa kwa heshima ya chadema tu sasa subiri uone moto.
Sasa CDM mmefika mbali hata Albarto Msando hamumtaki tena kisa kumtetea ZZK? Hiyo siyo siasa ni vita sasa jamani! Kila mmoja aangalie mipaka yake na kuheshimiana, mnakoelekea siyo kuzuri na matokeo yake mtakuja kuyaona soon!

Hivi ni vita vya pazi furaha ya kunguru!
 
Back
Top Bottom