Muuza Kangala
JF-Expert Member
- Jul 21, 2021
- 1,126
- 4,169
Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Mkoani Tanga Wakili Albert Msando amesema mkataba uliosainiwa baina ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia mamlaka ya usimamizi wa Bandari nchini (TPA) na serikali ya Dubai kupitia Kampuni ya DP World ni wa jumla kwakuwa kifungu cha Pili 'C' cha mkataba huo kinasema kutakuwa na mikataba midogo midogo (HGA) ambazo zitataja haki za kimkataba zote kuhusiana na yale ambayo pande hizo mbili zimekubaliana
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa Chama cha Mapinduzi (CCM) unaofanyika Wilayani Korogwe, Mkoani humo Wakili Msando amewashukia wanataaluma wa sheria wanaopotosha umma kwa kutafsiri tofauti vifungu na vipengele vilivyopo kwenye mkataba huo na kueleza kuwa hapo inaonesha utofauti ulipo kati ya watu waliosoma sheria na mawakili kama yeye
Aidha ameeleza kuwa mawakili pia wametofautiana kwenye utendaji kazi kwakuwa wapo waliobobea kwenye uwakili wa uwekezaji kama yeye lakini wengine ni mawakili wa mirathi, ndoa nk, hivyo ameshangazwa kuona mawakili wa mirathi wanakuwa wazungumzaji zaidi kuhusiana na masuala ya DP World na hivyo kujikuta wakifokafoka
Amesema makubaliano hayo yanaonesha umakini wa serikali kwa kumhakikishi muwekezaji kuwa kampuni itakayoanzishwa hapo ni lazima iwe kisheria na kwamba mojawapo ya jukumu walilonalo DP World ni pamoja na kuanzisha kampuni hapa nchini itakayotekeleza makubaliano hayo
Ameeleza kuwa DP World wakifungua kampuni hapa nchini maana yake ni kwamba kampuni hiyo itasimamiwa na kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria za Tanzania kwakuwa imesajiliwa hapa nchini
Ameendelea kuufafanua mkataba huo kwa kueleza kuwa, hakuna ardhi itakayohamishwa kwenda kwa kampuni iliyofunguliwa hapa nchini au Dubai.
Chanzo: Jambo Tv
Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa Chama cha Mapinduzi (CCM) unaofanyika Wilayani Korogwe, Mkoani humo Wakili Msando amewashukia wanataaluma wa sheria wanaopotosha umma kwa kutafsiri tofauti vifungu na vipengele vilivyopo kwenye mkataba huo na kueleza kuwa hapo inaonesha utofauti ulipo kati ya watu waliosoma sheria na mawakili kama yeye
Aidha ameeleza kuwa mawakili pia wametofautiana kwenye utendaji kazi kwakuwa wapo waliobobea kwenye uwakili wa uwekezaji kama yeye lakini wengine ni mawakili wa mirathi, ndoa nk, hivyo ameshangazwa kuona mawakili wa mirathi wanakuwa wazungumzaji zaidi kuhusiana na masuala ya DP World na hivyo kujikuta wakifokafoka
Amesema makubaliano hayo yanaonesha umakini wa serikali kwa kumhakikishi muwekezaji kuwa kampuni itakayoanzishwa hapo ni lazima iwe kisheria na kwamba mojawapo ya jukumu walilonalo DP World ni pamoja na kuanzisha kampuni hapa nchini itakayotekeleza makubaliano hayo
Ameeleza kuwa DP World wakifungua kampuni hapa nchini maana yake ni kwamba kampuni hiyo itasimamiwa na kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria za Tanzania kwakuwa imesajiliwa hapa nchini
Ameendelea kuufafanua mkataba huo kwa kueleza kuwa, hakuna ardhi itakayohamishwa kwenda kwa kampuni iliyofunguliwa hapa nchini au Dubai.
Chanzo: Jambo Tv