Al-Huda inaeneza uongo dhidi ya Kanisa Katoliki

Al-Huda inaeneza uongo dhidi ya Kanisa Katoliki

.
Haondoki mtu hapa! Tutawaeleza hata ukichukua! @Abdlhalim?? Wacha kujipendekeza. Yaliyo Vifuani.....

Kwani umefukuzwa? Ni haki yako kubaki katika hiki kijiwe cha wamisheni! Lakini ujue kuwa si wote wenye mawazo yaliyojaa udini kama yako. Na hawatasita kukuambia hivyo.

Amandla............
 
Kama The Citizen na Al Huda zote zimepotosha taarifa, huoni kuwa al Huda (gazeti la kidini) lina mchango na wajibu mkubwa zaidi wa kuleta taarifa sahihi kwa waumini wake? Je, hujui madhara ya upotoshaji yanayoweza kufanywa na gazeti la kidini? Msiwe mnapayuka bila kutafakari na kuleta sentensi za jumlajumla.

Acha kukurupuka na kushambulia watu wakati hujasoma mada yenyewe. anza mwanzo kusoma kisha ndo uchangie.

Kwanini asingesema Magazeti yaeneza uwongo dhidi ya Kanisa katoliki? na badala yake amesema Al-huda? na jee kweli kilichoandikwa ni uwongo?

Usiruhusu jazba zikuongoze katika maandishi yako au kauli zako.
 
Unauhakika gani kama hii taarifa ni mwendelezo wa The Sunday Citizen ? na mbona huja hoji kilichoandikwa na Mwana halisi toleo la Mei 20??

Wanachoongea Al-Huda kina ukweli maana hiyo ndo DINI-SIASA

Ndugu yangu AbbyBonge, itakugharimu nini kusoma nilichoandika na kukielewa na siyo kuelezea ambacho hujaelewa na sijakizungumza? Naomba usome tena nilichoandika na uelewe ujumbe wake.

Na tatizo la namna hii la kufanya hitimisho kabla hujaelewa kitu kilichozungumzwa ndilo linaloathiri wachangiaji wengi. At the end of the day, we end up discussing other things and forget about what has been said.
 
.
Haondoki mtu hapa! Tutawaeleza hata ukichukua! @Abdlhalim?? Wacha kujipendekeza. Yaliyo Vifuani.....

Nani amekwambia uondoke ndugu? Na sijui najipendekeza nini?

Naona hoja umeishiwa vimebaki vioja.
 
Acha kukurupuka na kushambulia watu wakati hujasoma mada yenyewe. anza mwanzo kusoma kisha ndo uchangie.

Kwanini asingesema Magazeti yaeneza uwongo dhidi ya Kanisa katoliki? na badala yake amesema Al-huda? na jee kweli kilichoandikwa ni uwongo?

Usiruhusu jazba zikuongoze katika maandishi yako au kauli zako.

Ndg naona unakuwa mkali kwa kuwa limetajwa al Huda badala ya kuangalia hoja aliyoleta mleta thread. Kwa msingi huo basi, wewe hasa ndiye ambaye hujasoma thread ina maudhui gani.

Hata hivyo, kama itakupendeza unaweza endelea kusimamia uonavyo wewe inakupendeza, kwamba ni sahihi au si sahihi kwa al Huda kuleta habari za kichochezi au la.
 
Unajua kuna watu wengine labda wana zile chuki za ndani ya damu, sababu Alhuda ndio wameandika ndio kwa upande wake upotoshaji, Je Mwanahalisi je? nadhani itakuwa ni uelimishaji sababu ni gazeti la kira raia, Ni bora tuwe tunatafakari saana kabla ya kutoa.

Ndugu yangu Isskia, naomba ufanye haya mambo matatu nitakayo kuomba uyafanye kabla ya kuchangia:

1. Tafuta The Sunday Citizen la Mei 3, halafu soma lead story yake.

2. Tafuta Al-Huda ya jana (Mei 28) na usome lead story yake.

3. Soma tena nilichoandika na ukielewe.

4. Halafu anza kuchangia. Vinginevyo, utakuwa unachangia kitu usichokijua na hutakuwa umenitendea haki.
 
When religious matters are mixed up with politics we get poligious in the sense that this word is ambiguous and it ends at confusing us,so good of us is to let all these two live freely and separately which i think it is better for everyone existance.
 
Alhuda sio wa kwanza kuindika habari hii kwanini umeliandama Alhuda tu? Na umenyamazia Mwanahalis, the sundy citzen? watu kama wewe ndio mnaoiletea sifa za udini jf na kuonekana ni kijiwe cha wakristo!

BinMgen, kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni au kusema kile kinachomkera. Naamini hata mimi siyo wa kwanza kusema kama nilivyosema kuhusu Al-Huda. Kwa nini hata wewe hujawaandama wengine na unaniandama mimi? Halafu, je, ni kweli umesoma hayo niliyoyaeleza vizuri na kuyaelewa kabla ya kuchangia au umeona uchangie kwanza kabla ya kusoma na kuelewa?
 
Sawa, wewe unalalamika juu ya upotoshaji, je wewe una maoni gani kuhusu mpango huo. Hebu tupe uchambuzi kidogo kuhusu yaliyomo. mimi nimesoma na ninaendelea kutafakari kwa kina. Je huku si kuchanganya dini na siasa?

Mpango wa Kanisa ni kujenga 'informed conscience' ili waumini wake au wanajamii wachague kile wanachoona ni chema bila kujali dini, itikadi ya chama au kabila la mtu.

Kwa kifupi, Kanisa Katoliki linahamasisha waumini wake (na pia watu wengine) waweze kutumia kura yao vizuri (to learn how to vote responsibly) kuepuka kuwachagua viongozi wasiowajibika au wanaoweka maslahi yao mbele na maslahi ya nchi nyuma - tuchague viongozi wanaotupunguzia na sio wanaotuongezea umaskini, maradhi na ujinga.

Tunataka tuchague viongozi bora - wawe, Wakristo, Waislamu au waumini wa dini za asili - sisi hilo hatujali. Tunajali kiongozi bora na mwenye uchungu na nchi yake na huyo anaweza kuwa Mkristo, Muislamu au anayeamini dini za jadi au dini nyingine.

Kama viongozi wa dini hawawezi kuwajenga waumini wao katika haki, amani na upendo hata sioni kwa nini kuwe na sababu ya kuwa dini au dhehebu. Kwa hiyo, kwa mambo yanayojenga jamii ya Watanzania na kuwafanya waendelee, Kanisa lazima lishiriki (contribute to) kwa hali na mali katika kufanikisha 'that common goal'. Hiyo ni 'moral obligation'.

Kanisa lisiposhiriki (yaani kama wanakanisa) hawashiriki katika kuleta maendeleo au kupata viongozi bora (wawajibikaji) basi Kanisa au dhehebu hilo halimfai mtu yeyote.

Kinachokatazwa ni kupigia debe kundi fulani la watu kwa vile Kanisa ni lazima liwe neutral - linawahusu waumini wote (na pia kama watu wengine wataona ina faa, basi watu wote). Tuwe tunajaribu kuona kama kitu fulani ni 'constructive' au 'destructive'.

Mimi ni Mkristo, lakini nikisikia mahubiri ya Waislamu yanayonijenga, ninayafuata kwa vile ni 'constructive' yanatoka kwa Mungu na sitajali yamesemwa na nani. Lakini pia nikisikia mchungaji, padre au askofu fulani (ingawa ni muumini mwenzangu) anahubiri kitu ninachoona hakijengi, sitakifuata kwa vile nitaona ni 'destructive'.

Truth is never contained in a particular faith system; it's beyond that. Hivyo, let's affirm what's good even if it is said by people we do not share the same faith system.
 
Kuwekana sawa ....... Kuna baadhi ya magazeti wakati unayasoma inabidi usome ukiwa na six sense organs ........!
 
Magobe, well said, well argued! A good and competent leader is that one who understands, appreciates and listens the woos and hurrays of his or her people. Faith is none of the virtues of a good leader. Being religious however can improve the leadership talents, can add up but not the basic requirements. Catholics fromthe recent published documentary appear to push for this line of thinking. Sasa kwa kuwa wamesema wakatoliki tu, isiwe hoja ya kukataa ushauri mzuri, bali ituchochee hata sis hapa JF tutafute jinsi ya kuwafikia watu, kuwawezesha wajue virtues zipi wanazitafuta kwa wale wenye kuomba kura. CCM alijichimbia vijijini Busanda, taking full advantage of the ignorance of the villagers, luring them to vote for their candidate. Taasis za dini zimesomesha na ziendelee kusomesha. BASI
 
Nimekuwa nikisoma gageti la Al-Huda lakini naona baadhi ya habari zake ni za uongo - hasa kama zinahusu Ukristo au Kanisa Katoliki. Huwa najiuliza kwa nini mtu mwenye akili timamu akae chini na aanze kuandika kitu anachoamini siyo kweli na ni kwa maslahi ya nani?

Katika toleo Na. 281 (Alhamisi Mei 28-Juni 3, 2009) ukurasa wa mbele gazeti hili limeandika:

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2010...
Kanisa Katoliki laanza mchakato kuweka utawala mpya Tanzania
. Lapita nyumba kwa nyumba kuhamasisha
. Ladai kutoa mwongozo kwa waamini wake

Ukisoma habari hii, utaona ni mwendelezo wa upotoshaji ulioanzishwa na gazeti la The Sunday Citizen la Mei 3 mwaka huu. Katika ukurasa wa mbele wa The Sunday Citizen lilichachapisha 'story' kuhusu Kanisa Katoliki na kuipa kichwa cha habari ambacho ni 'twisted'.

Kilisema hivi: 'Catholic church pushes for choice of next president' na kueleza: 'The Catholic Church in Tanzania has launched a comprehensive project whose aim is to influence the 2010 electorate process, and ensure that the country gets a leader of the Church’s choice.'

Ukisoma kijitabu kinachozungumzwa na kile ambacho gazeti hilo lilitaka kieleweke kwa wasomaji na pia kile ambacho gazeti la Al-Huda linapigia debe ni vitu tofauti kabisa na nia na maelezo ya kijitabu/vijitabu vyenyewe au Kanisa lenyewe. For how long are we going to continue doing this?

Kwa nini mwandishi/mhariri wa Al-Huda asisome hicho kijitabu au vijitabu kwanza kuliko kuendeleza uongo au kuna maslahi katika uongo? Pamoja na mambo mengine, moja ya uongo ulisomemwa na gazeti hili unaonekana katika 'quotation' iliyotumiwa na gazeti hilo na inaenda hivi:

"In the last two years Council of Elders thrice met the President of Tanzania to press issues of common interest." Haya ni maneno gazeti la Al-Huda linasema limeyatoa kwenye tovuti ya Kanisa Katoliki na limeyatafsiri hivi: 'Katika kipindi cha miaka miwili iliyopita Baraza la Wazee lilikutana na Rais wa Tanzania mara tatu kushinikiza masuala yenye maslahi kwa Kanisa.'

Sasa, tafsiri ya 'issues of common interest' ni kweli 'masuala ya maslahi kwa Kanisa'?

Nia ya chombo chochote cha habari ni kuielemisha jamii juu ya mambo yanayowahusu na kutafuta njia za kuyatatua (kama ni matatizo), kuyakabili (kama ni changamoto) na kuyandeleza (kama yanajenga) na siyo kusema uongo dhidi ya dhehebu au dini fulani.

Watanzania lazima tubadilike. Dini maana yake ni chombo kinachoendeleza 'spiritual values' ili waumini wake wawe na imani na kutenda mema. Dini siyo chombo cha malumbano na tukitumia imani zetu kupotosha umma hatufanyi hivyo kwa sababu ya dini zetu bali ubinafsi wetu. Kuendelea kiimani au kijamii ni kupiga hatua katika ukweli, uwajibikaji, haki, kuunganisha watu na siyo kuwafanya wawe maadui.

Hili ni gazeti ambalo Mkuchika alitakiwa alifungie. Natatizwa na akili ya Wamiliki na waandishi wa Gazeti hili.

Leo asubuhi kupitia Radio Iman nimewasikia wakisoma maoni ya Mhariri wa gazeti hili; anadai kuwa kwa kuondoa misamaha ya kodi kwa Taasisi za Kidini ni kulinufaisha Kanisa! Ina maana Kanisa ndo taasisi pekee ya kidini inayofaidika na Mismaha ya kodi? Taasisi za Kiislamu zinazotoa huduma kwa jamii kama Hospitali hazifaidiki? Uzushi wa ajabu! Yaani ile Cement iliyosamehewa kodi na iliyokuwa itumike kwa ujezi wa Msikiti Mwanza lakini ikauzwa mitaani inafaidisha Kanisa!

Kichwa cha Mhariri wa Al-Huda ni kitupu na hakina kitu bali kutimiza matakwa ya JIHAD dhidi ya Kanisa na Wakristo kwa manufaa ya Wafadhili na Wamiliki wa Al-Huda. Anchoangalia Mhariri huyo ni mradi mkono uende kinywani tu. Shame on him/her!
 
Hili ni gazeti ambalo Mkuchika alitakiwa alifungie. Natatizwa na akili ya Wamiliki na waandishi wa Gazeti hili.

Leo asubuhi kupitia Radio Iman nimewasikia wakisoma maoni ya Mhariri wa gazeti hili; anadai kuwa kwa kuondoa misamaha ya kodi kwa Taasisi za Kidini ni kulinufaisha Kanisa! Ina maana Kanisa ndo taasisi pekee ya kidini inayofaidika na Mismaha ya kodi? Taasisi za Kiislamu zinazotoa huduma kwa jamii kama Hospitali hazifaidiki? Uzushi wa ajabu! Yaani ile Cement iliyosamehewa kodi na iliyokuwa itumike kwa ujezi wa Msikiti Mwanza lakini ikauzwa mitaani inafaidisha Kanisa!

Kichwa cha Mhariri wa Al-Huda ni kitupu na hakina kitu bali kutimiza matakwa ya JIHAD dhidi ya Kanisa na Wakristo kwa manufaa ya Wafadhili na Wamiliki wa Al-Huda. Anchoangalia Mhariri huyo ni mradi mkono uende kinywani tu. Shame on him/her!

Inasikitisha jinsi watu wengine wanavyofikiri. Ni kitu cha ajabu sana! Au ni kwa sababu ya ilimu na siyo elimu?
 
Asante Telesphori. Japo hukukamilisha daraja la upadirisho, hi kazi nzuri unayoifanya ni Zaidi ya mapadiri.
Asante, ubarikiwe sana.
 
Mpango wa Kanisa ni kujenga 'informed conscience' ili waumini wake au wanajamii wachague kile wanachoona ni chema bila kujali dini, itikadi ya chama au kabila la mtu.

Kwa kifupi, Kanisa Katoliki linahamasisha waumini wake (na pia watu wengine) waweze kutumia kura yao vizuri (to learn how to vote responsibly) kuepuka kuwachagua viongozi wasiowajibika au wanaoweka maslahi yao mbele na maslahi ya nchi nyuma - tuchague viongozi wanaotupunguzia na sio wanaotuongezea umaskini, maradhi na ujinga.

Tunataka tuchague viongozi bora - wawe, Wakristo, Waislamu au waumini wa dini za asili - sisi hilo hatujali. Tunajali kiongozi bora na mwenye uchungu na nchi yake na huyo anaweza kuwa Mkristo, Muislamu au anayeamini dini za jadi au dini nyingine.

Kama viongozi wa dini hawawezi kuwajenga waumini wao katika haki, amani na upendo hata sioni kwa nini kuwe na sababu ya kuwa dini au dhehebu. Kwa hiyo, kwa mambo yanayojenga jamii ya Watanzania na kuwafanya waendelee, Kanisa lazima lishiriki (contribute to) kwa hali na mali katika kufanikisha 'that common goal'. Hiyo ni 'moral obligation'.

Kanisa lisiposhiriki (yaani kama wanakanisa) hawashiriki katika kuleta maendeleo au kupata viongozi bora (wawajibikaji) basi Kanisa au dhehebu hilo halimfai mtu yeyote.

Kinachokatazwa ni kupigia debe kundi fulani la watu kwa vile Kanisa ni lazima liwe neutral - linawahusu waumini wote (na pia kama watu wengine wataona ina faa, basi watu wote). Tuwe tunajaribu kuona kama kitu fulani ni 'constructive' au 'destructive'.

Mimi ni Mkristo, lakini nikisikia mahubiri ya Waislamu yanayonijenga, ninayafuata kwa vile ni 'constructive' yanatoka kwa Mungu na sitajali yamesemwa na nani. Lakini pia nikisikia mchungaji, padre au askofu fulani (ingawa ni muumini mwenzangu) anahubiri kitu ninachoona hakijengi, sitakifuata kwa vile nitaona ni 'destructive'.

Truth is never contained in a particular faith system; it's beyond that. Hivyo, let's affirm what's good even if it is said by people we do not share the same faith system.
Wewe huyo au...!?
 
Duuuuuh. Tz sasa kazi kweli kweli
Ila Al-Huda naona ndivyo walivyo elewa huo waraka maana tunatofautiana kuelewa mambo, sasa maadam huo uelewa siyo wa wote, hiyo hai myimi al-huda kutoa maoni !ila kuyafuata au kuyapuuza ni hiari ya kila mtu.
Binafsi mimi nimeusoma waraka na sioni udini ndani yake ila dokezo kadhaa za namna ya kuitumia kura yangu vyema hapo 2010. Na ndivyo nitakavyo fanya kwa hakika.
 
Hili ni gazeti ambalo Mkuchika alitakiwa alifungie. Natatizwa na akili ya Wamiliki na waandishi wa Gazeti hili.

Leo asubuhi kupitia Radio Iman nimewasikia wakisoma maoni ya Mhariri wa gazeti hili; anadai kuwa kwa kuondoa misamaha ya kodi kwa Taasisi za Kidini ni kulinufaisha Kanisa! Ina maana Kanisa ndo taasisi pekee ya kidini inayofaidika na Mismaha ya kodi? Taasisi za Kiislamu zinazotoa huduma kwa jamii kama Hospitali hazifaidiki? Uzushi wa ajabu! Yaani ile Cement iliyosamehewa kodi na iliyokuwa itumike kwa ujezi wa Msikiti Mwanza lakini ikauzwa mitaani inafaidisha Kanisa!

Kichwa cha Mhariri wa Al-Huda ni kitupu na hakina kitu bali kutimiza matakwa ya JIHAD dhidi ya Kanisa na Wakristo kwa manufaa ya Wafadhili na Wamiliki wa Al-Huda. Anchoangalia Mhariri huyo ni mradi mkono uende kinywani tu. Shame on him/her!

Simple ni suala la hesabu. Waislamu wana Taasisi ngapi zinazofaidika na msamaha, La kuzingatiwa ni kuwa Wabunge wetu na wengi wetu tuna msimamo kuwa Pato la Taifa lisitumike kufaidia dini fulani. Ukitia maanani hilo basi utaona kuwa hao Redio Imani hawakukosea.
 
Mimi naona kama mtu yupo makini na mada imemgusa kwa aina yoyote ile (kwa mazuri au mabaya) una haki kamili kabisa ya kumwandikia muhariri au kupeleka maoni yako na kumuomba muhariri ayaweke gazetini kwake yote kwa faida ya wasomaji.

Hata mimi nakumbuka mwaka 2006 july, nilipokuja tanzania nilisoma mada moja kwenye gazeti la kiongozi, iliyo elezea kuhusu uislam. hakika mimi niliijibu na kuipeleka kwa njia ya email kwa mhariri wa Kiongozi. naye pamoja na kunipa sababu zake za kushindwa kuitoa gazetini lakini alinijibu kwa email. Tuliandikiana sana kuhusu mada husika mpaka nikajiridhisha. Ndipo nikaituma kwa Annur wakaitoa.

sasa nashauri ni njia muafaka kujibu hoja kwa kupitia gazeti lenyee na sio kulalama.

Labda mlioko Tanzania tupeni anuani na mail address ya Al Huda
 
magazeti yote ya kiislam hayana jipya, ndomaana huwa tunayadharau tu na kuendelea na safari. siku zote huwa yanakuwa na maneno makali, na zaidi ili kuhamasisha waislam waone kama wanaonewa fulani hivi. THE MORE YOU ISOLATE YOURSELVES, THE MORE YOU WILL CONTINUE TO BE ILLITERATE AND POORER. mtakuja mkute siku moja hatusaidiani wala hatupokeleani kwenye mashule, mahospitali na hata maduka, kwasababu ya chuko ndani ya misikiti na redio za kiislam.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom